PostGE2025 Kihongosi: Chama kilichosusia uchaguzi hakipaswi kuhoji CCM imeshindaje. Hatuna muda kujibishana na walioshindwa

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Mwizukulu wa Buganda

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2024
Posts
638
Reaction score
1,771
Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Kenani Kihongosi amesema ushindi wa chama hicho katika uchaguzi unatokana na nguvu na mizizi iliyoanzia ngazi za chini, hivyo haupaswi kuwa ajenda ya kuhojiwa na vyama vya upinzani.

Akizungumza kwenye Kikao cha Shina Namba Moja, Singida Mjini leo Januari 19, 2026, Kihongosi amekitaka chama chochote kilichosusia kushiriki uchaguzi kuacha kuuliza kuhusu matokeo, akisisitiza kuwa hakina uhalali wa kufanya hivyo.

“Kuna chama kiligoma kushiriki uchaguzi, vyama vingine vikashiriki, CCM kikashinda kwa kishindo wanahoji ‘mmeshindaje shindaje?’ Wewe hujashiriki uchaguzi unauliza kama nani? Umesusa, umekataa, watu wameshinda unaanza kunung’unika. Raha ya ngoma ni kuingia kucheza,” amesema.

Your browser is not able to display this video.
 

Hivi huko CCM ni kundi la Wajinga ama...!!?

Kwa hiyo anataka kusema kama hukushiriki uchanguzi hutakiwi kuhoji matokeo...!! Hiyo ndiyo ilikuwa sababu ya kuwaondoa wapinzani na kuwaweka vibaraka wao kwa kuwapa mpaka maV Eighty kuzunguka nayo kwa miezi miwili ili kujihalalishia uhuni wao!! WAMEBUA .... ICC wako busy wanaandaa makaratasi.
 
Msijibizane na K
 
Mlialikwa kwenye mkutano wa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi mkasusa na kuendelea kuandika humu jukwaani 'no reform no election' hiyo election imefanyika mnakuja na kauli nyingine za kipuuzi.

Mtazeeka mkiburuzwa hivyo hivyo.
 
Reactions: Tui
Hawa hiki kiburi dawa yao ni moja tu. ICC na Mahakama nyingine za nje.

Msiendelee kubishana nao maana kiburi walichokuwa nacho saivi ni cha kunywa damu za watu hadharani alafu wanatangaza kabisa na kujisifia kuwa tumekunywa damu zenu na hamna cha kutufanya.

Binadamu akifikia level hii ya kiburi dawa yake ni kushughulikia nae kupitia wenye nguvu zaidi yake.

Kwa kuwa wametuona Wananchi mapoyoyo tusioweza kuwafanya lolote sisi nguvu zetu sasahivi tunahamishia kwa Wazungu. Ni mwendo wa ICC na Mahakama za Nje tu maana hata wanajeshi tuliwategemea wamekuwa wapumbavu.

Ngoja Arrest Warrant zianze kutoka ndo utaelewa kuwa hawa ccm sio lolote.
 
Mlialikwa kwenye mkutano wa mwenyekiti wa tume ya uchaguzi mkasusa na kuendelea kuandika humu jukwaani 'no reform no election' hiyo election imefanyika mnakuja na kauli nyingine za kipuuzi.

Mtazeeka mkiburuzwa hivyo hivyo.
Imefika mwisho huo uhuni, na kwa taarifa yako tunaandaa maandamano makubwa mwaka kesho kwenye miji yote itakayoandaliwa michuano ya AFCON, hadi mjue kuchezea haki za watu haikubaliki.
 
Imefika mwisho huo uhuni, na kwa taarifa yako tunaandaa maandamano makubwa mwaka kesho kwenye miji yote itakayoandaliwa michuano ya AFCON, hadi mjue kuchezea haki za watu haikubaliki.
Mtakuwa kichekesho kama kawaida yenu. AFCON itafanyika na itapendeza.

Adhabu ya wahaini mnaifahamu kwa vitendo.
 
Reactions: Tui
Hii inaonyesha CCM inaongozwa wenye uwezo wa chini ktk kupambanua masuala
 
Faki zati sonofabitch!
 
Yako wapi kwani
 
Final ya AFCON jana imetoa message loud&clear
1.Bila hakhi hakuna amani
2.Hakhi inadaiwa hata ikibidi kwa nguvu
3.Kila jambo lina ukomo- baada ya kubebwa kwenye mechi nyingi jana Morocco wamekwaa kisiki na kupata aibu ya milele.
 
Wafundisheni adabu hao vijana mliowajaza ujinga wakaingia barabarani siku ile.

Ushahidi wa upuuzi mwingi wa siku ile upo, usione watu wapo kimya ukadhani wajinga wanajua kila hatua mliyopitia katika kuhamasisha ule uasi.
 
Final ya AFCON jana imetoa message loud&clear
1.Bila hakhi hakuna amani
2.Hakhi inadaiwa hata ikibidi kwa nguvu
3.Kila jambo lina ukomo- baada ya kubebwa kwenye mechi nyingi jana Morocco wamekwaa kisiki na kupata aibu ya milele.
Mliikebehi Taifa Stars baada ya kunyimwa ile penati mkasema amani ni bora kuliko haki.

Jana waonevu Morocco wamekutana na mkono wa Mungu wakaaibika, Senegal wakapata haki yao.

Mungu akiamua kumpa mtu anachostahili atakipata tu, huwezi ukawa unashinda kwa kununua waamuzi kila mechi.
 
Yaani mbona mtaomba poo. Hatutaki kutetewa na mashirika ya kimataifa tunataka katiba mpya, na hatuombi bali ni lazima.
Jeuri hiyo hamna mkuu Tindo, huwa mnapochezea vichapo mnaanza kujitilisha huruma kwa jamaa wa haki za binadamu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…