Kigwangalajnr aikataa kamati ya utekelezaji Tabora!

Kigwangalajnr aikataa kamati ya utekelezaji Tabora!

Zyansiku

Member
Joined
Jul 27, 2009
Posts
49
Reaction score
10
Katika kile kinachoonekana kuwa familia ya Mbunge wa viti maalumu wilaya ya Nzega Mh Kigwangala ina matatizo ya asili, jana mdogo wake Lumola Maziku anaewania Uenyekiti wa Uvccm mkoa wa Tabora alitoa mpya pale alipokataa kuhojiwa(Kusailiwa) na kamati ya utekelezaji mkoa wa Tabora eti hana imani nayo hivyo haiwezi kumtendea haki na kutaka yeye akahojiwe na kamati ya utekelezaji Taifa bila kujua hatua za usaili zikoje kwani lazima uhojiwe na kamati hiyo kisha mapendekezo lazima yapitie kamati ya siasa mkoa na baadae Taifani,

Lumola Maziku hata hivyo baada ya kulamishwa leo kakubali kuhojiwa nakamati hiyo akitoa tambo nyingi kuwa hakuna kama yeye ilhali nae akimuiga kaka yake kutembea na kifimbo cheusi(Kutisha watu) kama ishara ya ulinzi sijui
 
Tukisema CCM wamejaza ndugu, marafiki watu wanatokwa jasho! Mtu wa kawaida hata una kipaji au Professional yako ni masuala la uongozi sahau kupata uongozi ndani ya CCM labda ujipendekeze pendekeze!!
 
Back
Top Bottom