Kigugumizi

amulson

Member
Nov 18, 2010
54
12
Nilikuwa kwenye daladala, kiti cha dirishani na pembeni yangu kulikuwa na jamaa amevaa saa. Kituo cha mbele kidogo jamaa alipanda basi na kusimama kando ya jamaa aliyekaa. Kumbe jamaa ana kigugumizi hali ikawa hivi;
aliyepanda; sssssamahani bbro ni sssaaa ngapi?
Aliyeketi; akamwangalia na hakumjibu
Aliyepanda; sssi nnnakuuliza jamaa yangu ni ssssaa nngapi?
Aliyeketi akaendelea kunyamaza
Mara jamaa wengine wakadakia, mshikaji si anakuuliza muda vipi unamchnia, au bubu?
Aliyepanda; wwwatu wengine bbwana, ssssaaa tu analinga mmhh!
Mara Yule aliyepanda akashuka, baadae mwenye saa akawajibu
Aliyeketi: mmmmimi sssikumjibu ttttungegombana tu…..
Watu hahahaaa kumbe naye anakigugumizi…….kweli wangepigana maana angedhani anamuiga
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom