PreGE2025 Kigoma: Ujenzi wa barabara ya Kasulu - Kabingo yenye urefu wa Kilometa 260, wafikia 83%

PreGE2025 Kigoma: Ujenzi wa barabara ya Kasulu - Kabingo yenye urefu wa Kilometa 260, wafikia 83%

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
726
Reaction score
953
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) leo Machi 18, 2025, imepokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara ya Kasulu - Kabingo yenye urefu wa Kilometa 260, inayotekelezwa kwa awamu nne (Lot 1 - Lot 4) kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 400.

Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Augustine Vuma, amesema kamati imejiridhisha na maendeleo ya ujenzi huo, ambao umefikia asilimia 83.

Ameeleza kuwa ujenzi wa loti zote nne kwa wakati mmoja katika mkoa mmoja ni jambo la kipekee, na ameitaka Wizara ya Ujenzi na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameeleza kuwa, miradi hiyo inagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambapo mikataba ilisainiwa kati ya mwaka 2020 na 2022, na muda wa utekelezaji umepangwa kuwa miezi 36 kwa kila loti.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), utekelezaji wa ujenzi wa barabara hizo umeendelea kwa viwango tofauti. Barabara ya Kasulu - Manyovu yenye urefu wa kilomita 68.25 imefikia asilimia 84.63 na inatarajiwa kukamilika Mei 30, 2025. Ujenzi wa barabara ya Kanyani Junction - Mvugwe yenye urefu wa kilomita 70.5 umefikia asilimia 75.38 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2025.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Aidha, ujenzi wa barabara ya Mvugwe - Nduta Junction yenye urefu wa kilomita 59.35 umefikia asilimia 90.75 na utakamilika Mei 7, 2025. Kwa upande wa barabara ya Nduta Junction - Kabingo yenye urefu wa kilomita 62.50, ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 100.

Miradi hii ya barabara inatarajiwa kuimarisha uchumi wa mkoa wa Kigoma kwa kuboresha usafiri wa ndani na wa kimataifa, kwani barabara hizo ni sehemu ya mtandao wa ushoroba wa Magharibi unaounganisha Tanzania na nchi jirani za Burundi, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kamati ya PIC imeipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi hii muhimu, ambayo imesaidia kuondoa vumbi katika barabara za Kigoma na kurahisisha usafiri wa wananchi

IMG-20250318-WA0352.jpg
IMG-20250318-WA0316.jpg
IMG-20250318-WA0314.jpg
IMG-20250318-WA0312.jpg
IMG-20250318-WA0348.jpg
IMG-20250318-WA0344.jpg
IMG-20250318-WA0338.jpg
IMG-20250318-WA0330.jpg
IMG-20250318-WA0320.jpg
IMG-20250318-WA0304(1).jpg
IMG-20250318-WA0300(1).jpg
IMG-20250318-WA0296.jpg
 
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) leo Machi 18, 2025, imepokea na kujadili taarifa ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa barabara ya Kasulu - Kabingo yenye urefu wa Kilometa 260, inayotekelezwa kwa awamu nne (Lot 1 - Lot 4) kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 400.

Mwenyekiti wa Kamati, Mheshimiwa Augustine Vuma, amesema kamati imejiridhisha na maendeleo ya ujenzi huo, ambao umefikia asilimia 83.

Ameeleza kuwa ujenzi wa loti zote nne kwa wakati mmoja katika mkoa mmoja ni jambo la kipekee, na ameitaka Wizara ya Ujenzi na Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Dkt. Charles Msonde, ameeleza kuwa, miradi hiyo inagharamiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) ambapo mikataba ilisainiwa kati ya mwaka 2020 na 2022, na muda wa utekelezaji umepangwa kuwa miezi 36 kwa kila loti.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), utekelezaji wa ujenzi wa barabara hizo umeendelea kwa viwango tofauti. Barabara ya Kasulu - Manyovu yenye urefu wa kilomita 68.25 imefikia asilimia 84.63 na inatarajiwa kukamilika Mei 30, 2025. Ujenzi wa barabara ya Kanyani Junction - Mvugwe yenye urefu wa kilomita 70.5 umefikia asilimia 75.38 na unatarajiwa kukamilika Oktoba 30, 2025.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Aidha, ujenzi wa barabara ya Mvugwe - Nduta Junction yenye urefu wa kilomita 59.35 umefikia asilimia 90.75 na utakamilika Mei 7, 2025. Kwa upande wa barabara ya Nduta Junction - Kabingo yenye urefu wa kilomita 62.50, ujenzi wake umekamilika kwa asilimia 100.

Miradi hii ya barabara inatarajiwa kuimarisha uchumi wa mkoa wa Kigoma kwa kuboresha usafiri wa ndani na wa kimataifa, kwani barabara hizo ni sehemu ya mtandao wa ushoroba wa Magharibi unaounganisha Tanzania na nchi jirani za Burundi, Rwanda, Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

Kamati ya PIC imeipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za utekelezaji wa miradi hii muhimu, ambayo imesaidia kuondoa vumbi katika barabara za Kigoma na kurahisisha usafiri wa wananchi
View attachment 3275710View attachment 3275711View attachment 3275712View attachment 3275713View attachment 3275716View attachment 3275717View attachment 3275719View attachment 3275720View attachment 3275724View attachment 3275725View attachment 3275726View attachment 3275728
Mafanikio makubwa kwa wanakigoma.....

Ushoroba wa magharibi unakaribia kukamilika kwa barabara za vumbi kubaki historia mkoani Kigoma !

Pongezi kwa serikali yetu adhimu !

#Taifa Kwanza chini ya Samia !
 
Kazi ya marehemu hiyo
Anajikombea tu mathawabu aaamin!

Tunamtaja kwa wema na tunavitaja vitu vyema alivyotuachia !!

Huo ndio ukweli na Allah kamwe hatoacha kumlipa wema kwa mema aliyotufanyia raia wenzake !!

Mwenyezi Mungu mrehemu rais wetu John Magufuli ,aaaamen!

#Taifa kwanza!
 
Anajikombea tu mathawabu aaamin!

Tunamtaja kwa wema na tunavitaja vitu vyema alivyotuachia !!

Huo ndio ukweli na Allah kamwe hatoacha kumlipa wema kwa mema aliyotufanyia raia wenzake !!

Mwenyezi Mungu mrehemu rais wetu John Magufuli ,aaaamen!

#Taifa kwanza!
Marehemu wenu alikuwa anasema amebana mafisadi na barabara zinajengwa kwa fedha za ndani kumbe mikopo.

Unakosa kuwashukuru Benki inayotoa hela unashukuru Marehemu ambaye hajatoa hata Shilingi kumi. Alikufa hata barabara ikiwe kwenye 6% ya Ujenzi sasa imefika 83% ya Ujenzi. Nani kafanya kazi kubwa?
62f0e-1.jpg

Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Doto James kulia akisaini mkataba wa Mkopo wa Masharti nafuu wenye thamani ya Shilingi bilioni 589.26 kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika AfDB iliyowakilishwa na Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo hapa nchini Dkt. Alex Mubiru (kushoto akisaini) katika hafla iliyofanyika katika ofisi za Hazina jijini Dar es Salaam.

Fedha hizo zitatumika katika ujenzi wa barabara ya kiwango cha lami kutoka Kabingo(Kakonko)-Kasulu-Manyovu km 260 mkoani Kigoma.
 
Back
Top Bottom