GE2025 Kifo cha Ndugai Charudisha Mchakato wa Kura za Maoni Jimbo la Kongwa; Fomu kuchukuliwa leo Jumanne Agosti 12, 2025

GE2025 Kifo cha Ndugai Charudisha Mchakato wa Kura za Maoni Jimbo la Kongwa; Fomu kuchukuliwa leo Jumanne Agosti 12, 2025

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,436
Reaction score
5,234
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kongwa kimetangaza kuanza tena mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kongwa, kufuatia kifo cha aliyekuwa Spika wa Bunge na Mbunge wa jimbo hilo, Job Ndugai kilichotokea Agosti 6, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Wilaya ya Kongwa, Julius Lepupuma zoezi hilo litakuwa la siku moja na litafanyika Agosti 12, 2025 kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi jioni, ambapo fomu zitapatikana katika ofisi ya CCM Wilaya ya Kongwa na zitatolewa na Katibu wa Wilaya.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa gharama za fomu zitaendelea kuwa kama zilivyoanishwa kwenye Kanuni za Uongozi katika Vyombo vya Dola toleo la 2025, huku ikisisitiza masharti kwa waombaji ikiwemo kuwa wanachama hai wa CCM wenye akili timamu na waliolipia ada.

"Ni kweli tunatoa fomu kwa siku moja ya leo (Agosti 12,2025) baada ya hapa tunaendelea na taratibu za kawaida ambapo Jumapili ya terehe 17,2025 wajumbe watapiga kura za maoni," amesema Mkaugala

Aidha, imekataza wanachama kuandaa misafara ya magari, pikipiki, baiskeli, ngoma au matarumbeta kwa ajili ya kumsindikiza mgombea kuchukua fomu, pamoja na kuwaleta wapambe kwa lengo la kufanya sherehe.
 
Doh kwa hiyo Ndugai alitaka mpaka siku ya mwisho awe mbunge? Mtu amekalia kiti kwa miaka 25 na bado alitaka tena.

Watanzania ni wajinga sana walahi, huyu mtu walikuwa wanampitisha tena kugombea ubunge.

All in all, hatuna uchaguzi mwaka huu. Kauli ni moja tu, no reforms no election.
 
Kufuatia kifo cha aliyeongoza kura za maoni Jimbo la Kongwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Job Ndugai, kura hizo sasa zitapigwa upya Jumapili Agosti 17, 2025.

Katika matokeo ya awali, Ndugai aliongoza kwa kupata kura 5,692, akifuatiwa na Isaya Mngurumi (2,602), Deus Seif (1,260), Dk Samora Mshang’a (544), Dk Simon Ngatunga (517), Elias Mdao (435), Philip Chiwanga (558), Paschal Mahinyila (331), Balozi Emmanuel Mbennah (232) na Ngaya Mazanda aliyepata kura 195.

Katibu wa CCM Wilaya ya Kongwa, Joyce Mkaugala amesema mchakato wa kuchukua fomu utafanyika kwa siku moja ambayo ni leo Jumanne Agosti 12, 2025.

Mkaugala amesema na kura zitapigwa leo kwa utaratibu wa wajumbe ngazi ya kata kama ilivyofanyika Agosti 4, 2025 na baadaye vikao vya kawaida vitaendelea.

"Ni kweli tunatoa fomu kwa siku moja ya leo (Agosti 12,2025) baada ya hapa tunaendelea na taratibu za kawaida ambapo Jumapili ya terehe 17,2025 wajumbe watapiga kura za maoni," amesema Mkaugala.

Katibu amesema gharama za fomu ni kama ilivyokuwa awali, watalipia Sh500,000 na si vinginevyo.

Hata hivyo, hakuweka wazi kama kutakuwa na kampeni za kuzunguka kwa wajumbe kwa ajili ya kuwanadi wagombea kama awali akisema wanachama wasubiri wataelezwa utaratibu.
 
Kufuatia kifo cha aliyeongoza kura za maoni Jimbo la Kongwa kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Job Ndugai, kura hizo sasa zitapigwa upya Jumapili Agosti 17, 2025.

Katika matokeo ya awali, Ndugai aliongoza kwa kupata kura 5,692, akifuatiwa na Isaya Mngurumi (2,602), Deus Seif (1,260), Dk Samora Mshang’a (544), Dk Simon Ngatunga (517), Elias Mdao (435), Philip Chiwanga (558), Paschal Mahinyila (331), Balozi Emmanuel Mbennah (232) na Ngaya Mazanda aliyepata kura 195.

Katibu wa CCM Wilaya ya Kongwa, Joyce Mkaugala amesema mchakato wa kuchukua fomu utafanyika kwa siku moja ambayo ni leo Jumanne Agosti 12, 2025.

Mkaugala amesema na kura zitapigwa leo kwa utaratibu wa wajumbe ngazi ya kata kama ilivyofanyika Agosti 4, 2025 na baadaye vikao vya kawaida vitaendelea.

"Ni kweli tunatoa fomu kwa siku moja ya leo (Agosti 12,2025) baada ya hapa tunaendelea na taratibu za kawaida ambapo Jumapili ya terehe 17,2025 wajumbe watapiga kura za maoni," amesema Mkaugala.

Katibu amesema gharama za fomu ni kama ilivyokuwa awali, watalipia Sh500,000 na si vinginevyo.

Hata hivyo, hakuweka wazi kama kutakuwa na kampeni za kuzunguka kwa wajumbe kwa ajili ya kuwanadi wagombea kama awali akisema wanachama wasubiri wataelezwa utaratibu.
Mkuu, kwa nini huyo No. 2 asichue nafasi hiyo, kama ilivyo kawaida kwa mujibu wa Katiba yetu?
 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kongwa kimetangaza kuanza tena mchakato wa kuchukua na kurejesha fomu za kuwania nafasi ya Ubunge wa Jimbo la Kongwa, kufuatia kifo cha aliyekuwa Spika wa Bunge na Mbunge wa jimbo hilo, Job Ndugai kilichotokea Agosti 6, 2025.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu wa Siasa na Uenezi wa CCM Wilaya ya Kongwa, Julius Lepupuma zoezi hilo litakuwa la siku moja na litafanyika Agosti 12, 2025 kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa kumi jioni, ambapo fomu zitapatikana katika ofisi ya CCM Wilaya ya Kongwa na zitatolewa na Katibu wa Wilaya.


Taarifa hiyo imeeleza kuwa gharama za fomu zitaendelea kuwa kama zilivyoanishwa kwenye Kanuni za Uongozi katika Vyombo vya Dola toleo la 2025, huku ikisisitiza masharti kwa waombaji ikiwemo kuwa wanachama hai wa CCM wenye akili timamu na waliolipia ada.

"Ni kweli tunatoa fomu kwa siku moja ya leo (Agosti 12,2025) baada ya hapa tunaendelea na taratibu za kawaida ambapo Jumapili ya terehe 17,2025 wajumbe watapiga kura za maoni," amesema Mkaugala

Aidha, imekataza wanachama kuandaa misafara ya magari, pikipiki, baiskeli, ngoma au matarumbeta kwa ajili ya kumsindikiza mgombea kuchukua fomu, pamoja na kuwaleta wapambe kwa lengo la kufanya sherehe.
Daah... Pamoja na mbwembwe, dharau na kiburi chote kile leo washa-mdispose na sasa wanamreplace!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom