Kifo cha mwandishi wa Channel Ten: Kauli za Polisi na mwitikio wa Wanahabari

Katiba iliyopo kwasasa inampa mamlaka makubwa sana Rais kuhusiana na uteuzi ninaamini nafasi kama hiyo isingekuwa na mamikono ya wanasiasa tusingekuwa tunashuhudia mauaji na vitendo vya kikatiri namna hii, Polisi wengi wanaumizwa na maagizo yanayotolewa na viongozi wao ambao kimsingi wanateuliwa na mwenyekiti wa CCM taifa. Kwa mfano kuna Polisi inasemekana kwenye ile Operation ya Morogoro aligomea kwenda kufanya ukatili kama alivyoagizwa mpaka huu mda inasemekana amewekwa pembeni akisubiri uhamisho wake.
 
Wakuu, ni wazi kuwa sasa ukombozi wa pili unakaribia!

Ukombozi wa kiuchumi, ambao utamuwezesha mtanzania kufaidika na rasilimali alizopewa na Mola. Magamba wamepaniki, wanatafuta kila njia kujiokoa, hata kwa kutumia njia haramu na kuua.

Kamanda aliyepoteza maisha yake, RIP. Msiba wake uwe chachu ya ukombozi na kuzidi kuunganisha nguvu.

Kwa hatua hii, hakuna tena kurudi nyuma, ni kumzika kamanda, na kuendelea na M4C.

Wakuu, tuelewe na kuzingatia kuwa ukombozi uko mikononi mwetu wenyewe. Mataifa ya nje, yanaona, lakini hakuna muda wa kupoteza kuzidi kubisha hodi kwao na kuomba omba. Wengi wanapenda kuendelea kufanya kazi na wajinga wasiojua umuhuhimu wa hazina kubwa tuliyonayo na rasilimali nyingi, waendelee kuwasainisha mikataba ya kijinga ya muda mrefu kwa kuwapatia senti kidogo na kuwafichia Uswisi.

Hawa, hawawezi kwa sasa kujitokeza kwa uwazi na kuunga mkono harakati hizi, juhudi binafsi, hizo zinawezekana. Watasubiri. Wakiona kweli sasa Watanzania wako serious, watasimama, kupaza sauti zao na kuingilia kati.

Kinachotakiwa, ni kuendeleza kutoa ujumbe wa ukombozi kupitia M4C.

Viongozi toeni matamko mapema ya kuongoza umma from time to time, na kuwaandaa wanachi wanachotakiwa kufanya wanapotendewa kinyume na haki za binadamu. Camarade Marando, nadhani unanielewa.

Utengenezwe mkakati pia wa kuwa na vyombo vyenu huru vya habari, wazo hili limetolewa muda mrefu, watu wana nia njema ya kuchangia.

Aluta Continua!
 
masikini ameambiwa kupambana na kuwazuia cdm lakini aliyeuawa ni mwandishi wa Channel Ten na na wala sio 'mwajiliwa' wa adui wao cdm.
Basi hata kama ni maelekezo kutoka juu basi watumie akili katika kuua maana hata Morogoro, Arusha waliouawa sio 'adui' yao bali ni wananchi wapenda amani!
RIP ndugu yetu Mtz
 
wanasikia kwani? lakini hata wakifa, lazima siku moja makaburi yao watachalazwa viboko tu
 
Kwahiyo anafikiri akistaafu ndio mwisho?Lisu alisema
Wawe wamevaa magwanda au wamevua hawataachwa.Anaelewa
Maana ya huo ujumbe?
 
Naombeni mnipe mfano mmoja tu ambapo mwananchi/wananchi wamefanyiwa unyama na hii serikali halafu maneno yakasaidia!! Mfano mmoja tu ambapo reasoning ili fanya kazi Tanzania!! Mimi sikumbuki kwa kweli, Hivyo wananchi wakiwa tayari kukamata mitutu ndio mnishtue.
 

Penye red unauliza majubu, Unakumbuka Tibaigana akiwa madarakani alisema yeye si mwanachama wa Chama chochote na hashabikii chama chochote? lakini alipostaafu akataka kugombea Ubunge kwa ticket ya CCM kama mwanachama Mkongwe
 
Siku yaja atamtaja aliyempa hayo maelekezo, kama ni wasira, nape mukama, lukuvi, mkuchika, mwigulu au pinda!!!! Tutajua na tutawapunguza kuwa udongo.
 
Akihojiwa na kituo fulani cha redio kwa njia ya sim leo hasubuhi, kamanda kamuhanda amesema kuwa mwandishi huyo ameuwawa na mlipuko uliotokea kusiko julikana, na amevilaumu vyombo vya habari kuripoti habari zisizo za kweli tofautitofauti, amesema ripoti kamili ataitoa leo baadae.
nawasilisha.
 
Mkuu ni kweli ipo siri, nadhani polisi hasa wa kada ya chini wana agenda yao dhidi ya wakuu wao na serikali pia, kwa kuua raia waio na hatia, wanataka serikali ichukiwe na jeshi la polisi lichukiwe na wananchi , kitu ambacho wameshafanikiwa sana katika agenda hiyo. Imefika wakati sasa viongozi wa pilisi na serikali kukaa kuangali hayo badala ya kuendelea kutupa sababu zisizo na mshiko. Fuatilia matukio ya polisi kujiua, kuwaua wenzao na haya yote utaona kuna kitu, kuna agenda ya kufanyia kazi. Nabaki na imani na JWTZ lakini si Polisi katika kulinda wananchi.Inanikumbusha pia enzi za Soweto, askari wa makaburu ndio waliokuwa wakisababisha fujo na mauaji na si wananchi, hii ndiyo inatokea sasa hapa kwetu. Tusiishie kusema MUNGU IBARIKI TANZANIA, tujiulize aibariki katika lipi.
 

tume zote zilizoundwa before hazijawahi kuja na mapendekezo ya namna nyingine ya kukabiliana na raia wasio kuwa na silaha ili kuzuia maafa kama yaliyotokea,nini mchango wa izo tume sasa?manake kila siku naona tunarudia makosa yale yale na sababu zile zile kwa malengo ya kujustify kwamba always raia ndio wanakuwa wakaidi ktk kutii sheria.
 
Last edited by a moderator:
Mi simo katika maneno ya police Mungu nisamehe kama nimeyasikia kwa bahati mbaya kwani halikuw kusudio langu kusikiliza uongo ule
 
Penye red unauliza majubu, Unakumbuka Tibaigana akiwa madarakani alisema yeye si mwanachama wa Chama chochote na hashabikii chama chochote? lakini alipostaafu akataka kugombea Ubunge kwa ticket ya CCM kama mwanachama Mkongwe

mahita nae,,,ingawa hakufanikiwa malengo,lets wait kwa KOVA
 
Kwahiyo anafikiri akistaafu ndio mwisho?Lisu alisema
Wawe wamevaa magwanda au wamevua hawataachwa.Anaelewa
Maana ya huo ujumbe?

mkuu naona siasa zimezuia uwezo wao wa kufikiri,lazima wajue na watambue kuwa one day they will be held accountable for what they have done today.
 
Its hard to take mpaka sasa wana kura za WAHINDI tu 2015 wanaoogopa kufukuzwa KUA SIO RAIA.
 

ripoti tena inatoka kwake????
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…