Kifo Cha CCM ni matarajio ya WaTanzania

Kifo Cha CCM ni matarajio ya WaTanzania

Mwiba

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2007
Posts
7,607
Reaction score
1,760
Kama kuna kitu wanachokisubiri na kukingojea Watanzania walio wengi basi ni anguko la CCM litakalopelekea kifo chake,vingi ya vyama vilivyopigania uhuru wa Nchi zao sasa vimebakia kama ni historia .

Matarajio ambayo huenda yakaanza kuonesha dalili za kifo cha CCM ni uchaguzi mkuu hapo mwezi wa kumi,masikio ya WaTz kwa sasa yameanza kugeukia mwezi huo na kujiandaa kusikia kuwa CCM imeaga Tanzania kama si dunia.

Aminia siku hizi kuonekana wewe mwananchi wa kawaida ni ccm imekuwa noma sana ,baadhi huwa wanajitokeza siku za sherehe za ccm na makongamano yao ndio utawaona wakivaa sare za kiccm ,tofauti na kuta wananchi wa vyama vingine ambao huvaa sare za vyama vyao bila hata ya kuwepo na dalili za mkutano na imekuwa kawaida kutembea nazo ,ila kwa wanaojiita wanaccm ni mtihani mkubwa kuivaa sare na kutembea nayo ,hiyo ni dalili tosha kuwa chama kimepoteza mvuto na imekuwa ni chama aibu.
 
Huo ndio ukweli,CHAMA CHAKAVU(CCM) KIMEFIKIA MWISHO!!!,MAGAMBA IBENI VYA MWISHO MWISHO ILA VITAWATOKEA PUANI.
R.I.P MAFIDADI NA CHAMA CHENU.
 
Hapo zamani za kale kilikuwepo Chama cha siasa kikiitwa ccm ,tunajua zaidi ya wanavyotaka kujipapatua bado mtaimbo umezama na unazidi kuzama ,wapenda siasa za kweli wengi kuihama CCM katika siku chache zijazo na hizi tulizo nazo ,we wacha tu.
 
haaa haaa haaa .... Mwiba nakukubali .... upo humu jamvini kitambo tangu 2010 nakusoma humu ukiipinga CDM .... lakini sasa upo UKAWA ... safi sana
 
Last edited by a moderator:
Nitafungua champaign kusherehekea kifo cha CCM.
 
Kila kitu mungu amekiwekea mwanzo na mwisho waki, CCM unataka iongoze milele? Mwisho wake umefika kubali katana, weweseka usiweweseke 25 Oct 15 bye bye, soma nyakati.....
 
ccm inajiona bd ni imara kwa sababu inasubiri lubuva ameshapewa maelekezo.(bao la mkono)
 
Back
Top Bottom