Kete ya CCM kwa sasa KUFITINISHA ACT Wazalendo na CHADEMA

Mwanaukweli

JF-Expert Member
May 18, 2007
4,786
1,710
Wakuu salamu.

Tumeshuhudia juhudi kubwa iliyofanywa na dola kupandikiza mgogoro ndani ya CUF, mgogoro uliolenga kumpoteza na kummaliza kisiasa Maalim Seif Shariff Hamad. Kilele cha mgogoro huo ni matukio yaliyofuatana kwa karibu (si kwa bahati mbaya) mkutano mkuu wa CUF Lipumba, na maamuzi ya Mahakama Kuu ya kumtambua Lipumba kuwa Mwenyekiti halali wa CUF. Haya yote mawili yameshangiliwa sana na wanalumumba.

Yaliyofuata baada ya hapo, Lumumba imepigwa na butwaa, baada ya Maalim Seif na wanaomuunga mkono KUTUPA MZIGO, na kuhamia ACT Wazalendo. Tukio hili laweza kufungua ukurasa mpya kwa upinzani Tanzania, jambo ambalo Lumumba ni habari mbaya.

Kwenu ACT Wazalendo, na kwenu CHADEMA, mtambue kuwa vita mpya ya CCM SASA, si tena ndani ya CUF (mbaya wao hayupo tena). Hofu ya Lumumba ni uhusiano wa kisiasa Kati ya CHADEMA na ACT.

Tutarajie nyuzi nyingi humu za kuwafitinisha viongozi wa vyama hivi viwili, ikiwa ni pamoja na kufufua tofauti zao za zamani. Tutarajie siasa za majitaka dhidi ya Mbowe, Maalim na Zitto. Tutarajie uchonganishi wa CCM Kati ya Zitto na Maalim. Tutarajie propaganda za udini zirudi. CCM hawawi na raha iwapo upinzani hakuna mgogoro.

Kwa wapenda mabadiliko, propaganda hizo tusizishangae, na zisituyumbishe. Tushikamane zaidi na kusonga mbele.

Aluta Continua...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Acheni uongo Kila kitu kusingizia CCM

Akina Yericko Baada ya kugundua tu Kuwa Zitto Kabwe karekebisha vyema Makosa aliyofanya Kwenye kunasa 'saini' ya Lowassa 2015 Safari hii akafanikiwa kupata asaini ya Seif Basi Propaganda Chafu Za Kidini zikaanzishwa Leo mnakuja kusingizia CCM


CCM Haina haja ya 'kumchoma kisu' Mgonjwa aliepo ICU ambae anasubiri Kikao Cha Ndugu kuamua ama waZime Mashine Au waendelee kusubiri
 
Upinzani wa kweli Tanzania ni CHAUMA ya hashim rungwe tu

CDM Imejaa mapandikizi

ACT ni CCM "B" (hawa wapo kimkakati zaidi)

Sent using my iPhone using jamiiforum app
 
Acheni uongo Kila kitu kusingizia CCM

Akina Yericko Baada ya kugundua tu Kuwa Zitto Kabwe karekebisha vyema Makosa aliyofanya Kwenye kunasa 'saini' ya Lowassa 2015 Safari hii akafanikiwa kupata asaini ya Seif Basi Propaganda Chafu Za Kidini zikaanzishwa Leo mnakuja kusingizia CCM


CCM Haina haja ya 'kumchoma kisu' Mgonjwa aliepo ICU ambae anasubiri Kikao Cha Ndugu kuamua ama waZime Mashine Au waendelee kusubiri
Chenga aliyopiga Maalim Seif, hata Messi hawezi - JamiiForums

Ghafla Zitto Kabwe amegeuka adui wa CHADEMA, Kila dalili ya ACT kuwa chama kikuu cha upinzani bungeni baada ya uchaguzi mkuu 2020 - JamiiForums

Zitto tangu akisoma chuo UDSM,alikuwa upande wa Serikali,chondechonde Maalim, - JamiiForums

Maalim Seif kaona Mbali CHADEMA ijitafakari - JamiiForums

Maalim Seif anakwenda ACT? Litakuwa kosa la karne kwa Wazanzibar na Zanzibar HURU. - JamiiForums

Kimenuka! Mbowe kafula kama mbogo ! - JamiiForums

Uamuzi wa Maalim Seif wamuibua Mbowe

Swali kwa Maalimu Seif, kwanini ACT na siyo CHADEMA? - JamiiForums
Hizo tayari zimeletwa humu leo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata hao wanaohangaika kuhamia act wazalendo eti kumfuata seif jamani tatizo kwa demokrasia. WajitafKari.
 
Acheni uongo Kila kitu kusingizia CCM

Akina Yericko Baada ya kugundua tu Kuwa Zitto Kabwe karekebisha vyema Makosa aliyofanya Kwenye kunasa 'saini' ya Lowassa 2015 Safari hii akafanikiwa kupata asaini ya Seif Basi Propaganda Chafu Za Kidini zikaanzishwa Leo mnakuja kusingizia CCM


CCM Haina haja ya 'kumchoma kisu' Mgonjwa aliepo ICU ambae anasubiri Kikao Cha Ndugu kuamua ama waZime Mashine Au waendelee kusubiri
Huna Jipya kila Uzi unapita Ukitangs Tanga Na Propaganda Zako Mfu, TULIA ULAMBE DAWA....

"Mopao Mokonzi"
 
Huna Jipya kila Uzi unapita Ukitangs Tanga Na Propaganda Zako Mfu, TULIA ULAMBE DAWA....

"Mopao Mokonzi"

Ndio kawaida yangu kila uzi lazima nisome naku comment nikijskia hivyo

Baada ya kugundua Kuwa unateseka sasa ndio nazidisha
 
Uongo gani? Hujaona nyuzi humu leo za mazwazwa wenzio zikianza uzushi usiokuwepo?

Acheni uongo Kila kitu kusingizia CCM

Akina Yericko Baada ya kugundua tu Kuwa Zitto Kabwe karekebisha vyema Makosa aliyofanya Kwenye kunasa 'saini' ya Lowassa 2015 Safari hii akafanikiwa kupata asaini ya Seif Basi Propaganda Chafu Za Kidini zikaanzishwa Leo mnakuja kusingizia CCM


CCM Haina haja ya 'kumchoma kisu' Mgonjwa aliepo ICU ambae anasubiri Kikao Cha Ndugu kuamua ama waZime Mashine Au waendelee kusubiri
 
Acheni uongo Kila kitu kusingizia CCM

Akina Yericko Baada ya kugundua tu Kuwa Zitto Kabwe karekebisha vyema Makosa aliyofanya Kwenye kunasa 'saini' ya Lowassa 2015 Safari hii akafanikiwa kupata asaini ya Seif Basi Propaganda Chafu Za Kidini zikaanzishwa Leo mnakuja kusingizia CCM


CCM Haina haja ya 'kumchoma kisu' Mgonjwa aliepo ICU ambae anasubiri Kikao Cha Ndugu kuamua ama waZime Mashine Au waendelee kusubiri
Jenga hoja yenye nguvu,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uongo gani? Hujaona nyuzi humu leo za mazwazwa wenzio zikianza uzushi usiokuwepo?

Hizo nyuzi unasema zimeletwa Leo sasa Mie nakuambia Pitia oage Za YericKo Nyerere kuanzia Wiki iliyopita usome Halafu rudi u comment
 
Kwani Yericko ni msemaji wa chadema? Tangu lini?

Tusipokubaliana kwa hoja sio Upumbavu


Yericko Ni CCM? Maana nae toka Juzi anamshambulia Zitto Na kumuonya Seif asiende ACT?,
 
Back
Top Bottom