Kiranja wa jamii
JF-Expert Member
- Jan 2, 2023
- 963
- 2,198
Ukisoma maoni ya wengi mitandaoni na hata Tundu Lisu mwenyewe amewahi "kudhani" mara kadhaa kuwa amefunguliwa kesi ya uhaini "kimchongo" ili kupisha kipindi cha kampeni na huenda baada ya uchaguzi kesi ikatupiliwa mbali; huu ni mtazamo wa wengi
Hata hivyo ukitafakari kwa kina zaidi na kufuatilia mwenendo wa nchi yetu sasa unaweza kuona sio rahisi hicho kitu kutokea kwasababu kadhaa;
Kwanza kabisa, kama hiyo kesi ilifunguliwa ili kumdhibiti asilete usumbufu na kero ya kufafanua fafanua mambo mazito kwa mgombea wa CCM kipindi cha kampeni, kwanini mdhani hatadhibitiwa ili asilete usumbufu pia wakati wa utawala wa atakayeshinda?
Kama kweli swala ni kumdhibiti Tundu Lisu, kwanini watu wadhani mamlaka zimejipanga kumdhibiti tu kipindi cha kampeni ambacho ni kifupi kuliko kumdhibiti kipindi cha utawala ambacho ni kirefu?
Ni mtazamo wangu kuwa kama kweli hii kesi ipo "kimchongo mchongo" kama wengi wanavyoisema, haiwezi kuisha "kimchongo mchongo" baada ya kampeni kwasababu hata baada ya kampeni Lisu hawezi kupoa, moto wake wanaufahamu vizuri sana.
Matumaini yasijengwe kwamba baada ya kampeni kesi itaisha, kama lipo la kufanywa na kundi lake la mawakili lifanyike mapema na kama halipo kujiandaa kisaikolojia ni muhimu zaidi
Hata hivyo ukitafakari kwa kina zaidi na kufuatilia mwenendo wa nchi yetu sasa unaweza kuona sio rahisi hicho kitu kutokea kwasababu kadhaa;
Kwanza kabisa, kama hiyo kesi ilifunguliwa ili kumdhibiti asilete usumbufu na kero ya kufafanua fafanua mambo mazito kwa mgombea wa CCM kipindi cha kampeni, kwanini mdhani hatadhibitiwa ili asilete usumbufu pia wakati wa utawala wa atakayeshinda?
Kama kweli swala ni kumdhibiti Tundu Lisu, kwanini watu wadhani mamlaka zimejipanga kumdhibiti tu kipindi cha kampeni ambacho ni kifupi kuliko kumdhibiti kipindi cha utawala ambacho ni kirefu?
Ni mtazamo wangu kuwa kama kweli hii kesi ipo "kimchongo mchongo" kama wengi wanavyoisema, haiwezi kuisha "kimchongo mchongo" baada ya kampeni kwasababu hata baada ya kampeni Lisu hawezi kupoa, moto wake wanaufahamu vizuri sana.
Matumaini yasijengwe kwamba baada ya kampeni kesi itaisha, kama lipo la kufanywa na kundi lake la mawakili lifanyike mapema na kama halipo kujiandaa kisaikolojia ni muhimu zaidi