Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 173
- 671
Kesi ya Habeaus Corpus iliyofunguliwa na Sije Emmanuel Mbugi, mke wa kada wa Chadema, Mpaluka Mdude Nyagali ilishikilizwa Juni 30 katika Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala ya Mbeya.
Mdude alitekwa nyumbani kwake Mei 2 usiku na watu wasiojulikana, ambapo kabla ya kumchukua walimpiga na kumjeruhi.
Soma zaidi: Chadema, kambi ya kumtafuta Mdude
Jeshi la Polisi lilikanusha kumchukua Mdude na likasema linafanya uchunguzi lakini mpaka sasa hakuna taarifa iliyotolewa.
Akifafanua undani wa shauri hilo, Wakili Boniface Mwabukusi, anayewaongoza mawakili wenzake Hekima Mwasipu na Solomon Kimunyu amesema, “Habeaus Corpus maana yake ni ulete mwili mbele ya mahakama. Kwa hiyo tunawataka tunaowashitaki kuuleta mwili mbele ya Mahakama.
Mwabukusi ambaye pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS), amesema uamuzi wa shauri hilo utatolewa Julai 9, 2025.