Kama unapata kichefuchefu pima mkojo unaweza kuwa na ujauzito mchanga.Huwa napata kichfuchefu kuona mipaja iliyokunjamana vibaya hivyo au rangi za buluu na nyekundu za kujichubua .Samahani kusema binadamu wanatia kinyaa wakiamua kujiweka vibaya.Kwanini asingevaa hata suruali ndefu.
Mwenyewe anasema anasikia kichechefu mtoto wa kiume huyo unategemea nini.We mlevi ulikua wapi. Kitambo sjakuona au ulifichwa na yule mbaba wa kipare
hii naona EMT hakuinasa hii!kua mbongo noma cku hz.
Kwa waandishi wa Shigongo usikute hii ilikuwa oparesheni ya kukamata wanawake wanaojiuza halafu sisi tunapigwa fix wakati mavazi tu ya huyo mwanamke inaonekana alikuwa anauza K.
Aha..na mama yako akapime nini?Kwani umeambiwa kila anayetapika ni wa kupima mkojo.Wanaopata Malaria nao wangepima mkojo na si Damu, walio ktk boat nao wangapima mkojo kabla ya kupanda.Mizaha ya kiswahili inawa reflect ufupi wa akili zao.Ndio maana mna vimisemo vy akipuuzi sijui akiji ni nywele, sijui mgaa gaa na pwani....uvivu kuanzia ktk akili hadi a maisha.Ndio maana hata ktk ngono mnayoifikia huwa mnazimishwa na wanawake.Si ndio unaobebwa na wanawake kuogeshwa..wengine kwa wanawake wanabebwa.Unagaa na pwani badala ya kuingia ktk maji..Ndio maana waswahili unaweza kwenda kazini unawaacha kibarazani,unarudi unafua na mengine wanakuangalia, halfu wanakuomba hela baadae.Mtaliwa bure kima nyie.Kama unapata kichefuchefu pima mkojo unaweza kuwa na ujauzito mchanga.
Haha..hawa jamaa si fedha.Ni kondoo wa kafara.Anayejua Hela huwa anajua kupima risk na success rate,huku akijua kuwa 100 atafanikiwa mission.Km sivyo huwa wanaojua hela wanajua haitoshi hiyo hela.Hawa makenge sidhani km wanajua hilo.Aiseee acha pesa iitwe pesa yani mtu yupo radhi kuweka maisha yake rehani kisa pesa duuh?
Haha..umeangalia kitu nzuri ya kuwakumbusha waandishi wa kibongo kuwa ktk mbwembwe zao basi wapime kila kitu kwa akili halisi.Hat akatuni wenyewe wanauhasilia sana.Katuna utakuta wanafauata principal za physics, na jamii sana na maadili,uandishi km zinapinda basi,hupindisha ili kufurahisha.huyu mwandishi ilibidi aweke source ya habari ,ili kuleta uhasilia aipataje na aliyeandika ni nani hadi ajieleze km si wa ukanda huu.Otherwise aiweke sawa kuwa mtu ambaye hakuwepo mwingine kushihudia zaidi ya kundi la waandishi.Habari za Udaku bana,Wanasema mnyetishaji sasa sijui alikuwa Mchina? Maana ukirejea anasema hakukuwepo na ndg wala Mtu mweusi,Bali sura za kichna tu.
Aha..na mama yako akapime nini?Kwani umeambiwa kila anayetapika ni wa kupima mkojo.Wanaopata Malaria nao wangepima mkojo na si Damu, walio ktk boat nao wangapima mkojo kabla ya kupanda.Mizaha ya kiswahili inawa reflect ufupi wa akili zao.Ndio maana mna vimisemo vy akipuuzi sijui akiji ni nywele, sijui mgaa gaa na pwani....uvivu kuanzia ktk akili hadi a maisha.Ndio maana hata ktk ngono mnayoifikia huwa mnazimishwa na wanawake.Si ndio unaobebwa na wanawake kuogeshwa..wengine kwa wanawake wanabebwa.Unagaa na pwani badala ya kuingia ktk maji..Ndio maana waswahili unaweza kwenda kazini unawaacha kibarazani,unarudi unafua na mengine wanakuangalia, halfu wanakuomba hela baadae.Mtaliwa bure kima nyie.
Mleta mada you are just plsin crazy!!!HATIMAYE modo maarufu Bongo
, Jacqueline Fitzpatrick Jack
Patrick amepandishwa kortini kwa mara ya kwanza huko Macau nchini China, Aprili 10, mwaka huu kwa kukutwa na madawa ya kulevya tumboni aina ya heroin kete 57 au kilo 1.1 yakiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni 223 huku ishu kubwa kwa muda wote aliokuwa mahakamani ikiwa ni kuangua kilio kila wakati.
Jack alipandishwa kwenye korti hiyo ikiwa ni mara
yake ya kwanza tangu alipokamatwa na madawa ya kulevya unga Desemba mwaka jana akitokea Bongo kupitia Thailand na kuingia nchini humo.
ILIKUWAJE?
Kwa mujibu wa chanzo chetu makini kilichopo Macau, Jack alifikia hatua hiyo dakika 15 baada ya kupanda kizimbani na kukutana na nyuso za Wachina tu zikimwangilia
Yeye alijua angekuta Wabongo au hata watu weusi wakimpa kampani, lakini matokeo yake alikutana na sura za Wachina tu, kilisema chanzo chetu.
Kikaendelea: Unajua kwa kawaida mtu anapopanda kizimbani mara zote anafarijika sana endapo atawaona anaowafahamu, hasa ndugu zake ambao watafika kumtia moyo, sasa yeye hakulipata hilo.
DAKIKA 10 ZATUMIKA KUMSOMEA MASHITAKA
Kuna madai kwamba, msoma mashitaka wa mahakama hiyo alitumia dakika 10 kutokana na taratibu za kisheria za huko huku akitakiwa kusema ndiyo au hapana tu kabla keshi hiyo kupigwa kalenda hadi Mei 23, mwaka huu
KUNA MADAI ALIZOMEWA
Chanzo hicho kiliendelea kudai kwamba, mbali na kukutana na upweke huo mahakamani, pia Jack alipata kisanga kingine pale baadhi ya raia wa nchi hiyo walipomzomea kwa sauti ya chini wakati akitoka kortini.
Inadaiwa kuwa, kwa Wachina kumzomea au kumsema vibaya mtu aliyedakwa na madawa ya kulevya ni kawaida kwani hakuna biashara, inapigwa vita nchini humo kama ya unga wakiamini unaangamiza nguvu kazi ya kizazi kijacho.
NDUGU WADAIWA KUMKATIA MAWASILIANO
Habari nyingine kutoka chanzo chetu zilidai kwamba, kwa sasa Jack amebaki yeye na Mungu wake baada ya nduguze waishio Bongo kumkatia mawasiliano kwa kile walichodai kuwa kitendo alichokifanya kimeiaibisha familia nzima.
Unajua ndugu zake walikata mawasiliano kabisa? Nchi nzima au tuseme dunia nzima kilio ni jinsi vijana wanavyoharibika kwa madawa ya kulevya, sasa kule kubainika kwamba Jack alibeba unga tumboni kwenda kuuza kumeifanya familia kujisikia vibaya sana, kiliongeza chanzo hicho kikiomba chondechonde kisitajwe gazetini.
KAMA ATARUDI BONGO SALAMA
Habari zaidi zinadai kwamba modo huyo ambaye pia ni Miss Ilala No 3, 2005, aliwahi kumwambia mshirika wake mmoja akiwa mahabusu kwamba, kama atabahatika kurejea Bongo salama,
atakwenda kupiga dua juu ya kaburi la mama
yake ili amsimamie katika kumwondolea nuksi kama siyo mabalaa. Baba
wa Jack anadaiwa kuishi nje ya nchi.
TUJIKUMBUSHE
Jack alikamatwa Desemba 19, mwaka jana kwenye Uwanja wa Ndege wa Macau nchini China akitokea jijini Bangkok
nchini Thailand
kuelekea Guangzhou, Mji Mkuu wa Jimbo la Guangdong Kusini mwa China ambako ilidaiwa ndiko alikokuwa anafikisha unga huo.
Ilidaiwa kuwa miongoni mwa mambo yaliyochangia kukamatwa kwake ni kuonesha uso wenye uchovu, kuanza kuwa na hali mbaya ya mwili, kushindwa kujibu maswali vizuri na hati yake ya kusafiria, yaani passport
kukutwa imegongwa mihuri ya kuingia nchini humo kila mara jambo ambalo wakaguzi waliliona si la kawaida kwa msichana kama yeye