Kero 5 kabisa za akina dada/mama mtaani

Kero 5 kabisa za akina dada/mama mtaani

Texas Tom.

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2013
Posts
510
Reaction score
273
1. Unakwenda dukani kwa mangi kukopa (kuongezea deni) ukijua kabisa mangi anakudai na atakusimanga simanga, wengine wanataa kununua kondom, mwingine kaiba mayai 2 kwa jirani anakuja kuuza unakuta mdada ameegesha hapo hanunui kitu anapiga story zisizo na maana na kuchunguza huyu ananunua nini na yule nini.


2. Usumbuliwa na tumbo la kuendesha na unaishi nyumba ya kupanga yenye vyumba zaidi ya 12 choo kimoja unakuta akina dada wanasukana jirani kabisa na mlango wa choo kutwa nzima

3. Una njaa, umenunua karobo kuku unataka kulirusha kama la gerezani mara mtoto anakuja na libakuli anasema dada kasema inanukia vizuri anataka kuonja!

4. Umeopoa kimwana chako wa heshima unakatiza nae mtaa kwa adabu zote unapishana na genge la akina dada wanaokujua then wanaangua kicheko

5. Jirani/rafiki yako ambaye pia ulishawahi kumsadia (yeye na mkewe) msururu wa matatizo ya kimaisha aliekua nayo, sasa amezipata na amefungua duka kubwa inayochanganya kiukweli, mkewe ndo akawa mtendaji mkuu pale dukani !! - utakoma kumjua!!!
 
imekaa kiuswazi zaidi, Nyamhongoro, Shamaliwa hakuna vitu vya namna hiyo.
 
Alafu uswazi watu hawalali..kila muda ukishtuka usingizini watu wanaongea...uswazi mchana hapalaliki mikelele mtindo mmoja..yaani uswazi noma.
 
yaani tabia za ajabu sana,ika hata huku kwetu wapo

watu kukaa vibarazani,ukiwapa kisogo ndo unakuwa
talk of kijiwe,yaani watu wanakujua zaidi ya ujijuavyo!!!!!
 
Back
Top Bottom