Greatest Of All Time
JF-Expert Member
- Jan 1, 2017
- 20,713
- 45,090
Beki bora kwa miaka 10 iliyopita kwangu mimi ni Kelvin Yondani Cotton Injinia Vidic.
Licha ya umri kuanza kumtupa mkono sasa, Kelvin Yondani katika ubora wake alikuwa ni mwamba usiotikisika. Yondani anaweza akacheza mpira wa kutumia akili pia Yondani anaweza akacheza mpira wa nguvu na ubabe.
Amekuwa tishio kwa washambuliaji wengi nchini hata kwa marefa ambao wamekuwa wakimuogopa kumpa kadi pale anapocheza undava. Kwangu mimi beki unatakiwa uwe katika kariba ya Yondani.
Yondani ana ball control, anajua kupoza mashambulizi, anajua kuusoma mchezo vizuri, anajua kuanzisha mashambulizi kutokea nyuma hasa kwa zile pasi zake ndefu zenye macho pia amekuwa akifunga magoli muhimu kwa timu yake. Kitu pekee alichoshindwa ni nidhamu.
Kelvin Yondani, beki bora wa kati kumshuhudia hasa baada ya zama za Victor Costa kuisha.
Kwako mdau, unamzungumziaje Yondani?
Licha ya umri kuanza kumtupa mkono sasa, Kelvin Yondani katika ubora wake alikuwa ni mwamba usiotikisika. Yondani anaweza akacheza mpira wa kutumia akili pia Yondani anaweza akacheza mpira wa nguvu na ubabe.
Amekuwa tishio kwa washambuliaji wengi nchini hata kwa marefa ambao wamekuwa wakimuogopa kumpa kadi pale anapocheza undava. Kwangu mimi beki unatakiwa uwe katika kariba ya Yondani.
Yondani ana ball control, anajua kupoza mashambulizi, anajua kuusoma mchezo vizuri, anajua kuanzisha mashambulizi kutokea nyuma hasa kwa zile pasi zake ndefu zenye macho pia amekuwa akifunga magoli muhimu kwa timu yake. Kitu pekee alichoshindwa ni nidhamu.
Kelvin Yondani, beki bora wa kati kumshuhudia hasa baada ya zama za Victor Costa kuisha.
Kwako mdau, unamzungumziaje Yondani?