Mpeni sifa Yesu
JF-Expert Member
- May 23, 2010
- 646
- 129
TAFADHALI samahani kwa wale waliofungua wakifikiri ni kazi. Kuna kundi la watu wametangaza kuwa wao ni Barrick Tanzania na wakatangaza nafasi za kazi nyingi sana mkoani shinyanga kule KAHAMA etc. watz wengi waliapply inavyosemekana na wamekuwa kwenye mawasiliano nao mara kwa mara. kutokana na hilo, ili wapate kazi kuna jobless wengi wametakiwa kulipa wengine 500,000/= wengine millioni etc na inasemekana wametoa pesa hizo. kuna kikundi cha wana usalama tunashirikiana nao shinyanga kwaajili ya suala hilo tu special, tunaomba yafuatayo kwa wote ambao wamedhurumiwa.
- JAMBO LA KWANZA, kama umedhulumiwa kwa namna hii, tafadhali tunaomba uwasiliane namimi bila kuchelewa ili niwasilishe majina ya watu hao polisi.
- kama unazo namba za simu ambazo labda umekuwa ukiwatumia pesa kwa njia ya mpesa etc, utuletee namba hizo kama ushahidi nami nitawasilisha kwa wanausalama.
- kama umedhulumiwa na unao ushahidi wa kutosha either kwa njia ya simu uliyowasiliana nao na pengine mlishaonana uso kwa uso, wasiliana nami au fika kituo chochote cha polisi watasaidia kuwasiliana nasi, na mimi nitafoward suala lako kwa wahusika.
- wasiliana nami kwa kupitia email mpani.sifa.yesu@gmail.com, bila kuchelewa.