Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinapenda kutoa taarifa ya awali ili kuweka kumbukumbu sawa kuhusu kikao kilichokuwa kimeitishwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB), kabla ya kuahirishwa hadi hapo kitakapoitishwa tena.
Kama ilivyotaarifiwa siku chache zilizopita kupitia vyombo kadhaa vya habari na njia zingine za upashanaji habari, THBUB iliandika barua kuitisha kikao leo Agosti 10, 2016, katika ofisi za tume hiyo jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa kikao hicho walialikwa kwa majina na nafasi yao na kwa mujibu wa barua ya wito kutoka THBUB, walikuwa ni wafuatao;
1. Mhe. George Masaju (MB)
Mwanasheria Mkuu wa
Serikali
2. Jaji Francis S.K. Mutungi
Msajili wa Vyama
3. Mr. Abdulrahman Kinana
Katibu Mkuu CCM
4. Dr. Vincent Mashinji
Katibu Mkuu CHADEMA
5. Katibu Mkuu
Tanzania Centre for
Democracy
6. Bw. Ernest Jumbe Mangu
(IGP)
Mkuu wa Jeshi la Polisi
Tanzania
Kwa mujibu wa barua ya wito, dhumuni kuu la kikao ilikuwa ni kujadili "MUSTAKABALI WA MIKUTANO NA MAANDAMANO YA VYAMA VYA SIASA". Vile vile THBUB ilipenda kujadili tangazo la CHADEMA kuhusu kile kinachoitwa "Ukuta" na mikutano iliyopangwa kufanyika tarehe 01 Septemba, 2016 nchi nzima.
CHADEMA ilihudhuria kikao hicho mahali na muda kama ilivyoelezwa kupitia barua ya wito, ikiwakilishwa na Katibu Mkuu Dkt. Mashinji aliyeambatana na wasaidizi wawili.
Hadi muda ambao kikao kilipaswa kuanza, ukumbini kulikuwa na wajumbe 3 pekee ambao ni, Mwenyekiti wa THBUB Bahame Nyanduga, Dkt. Mashinji na Jaji Mutungi.
Baada ya mazungumzo kati ya wajumbe hao watatu, ikakubalika kuwa kikao kiahirishwe kwa sababu kisingeweza kufanyika na kufikia makubaliano au maazimio yoyote yale, huku upande wa Serikali (Mwanasheria Mkuu na IGP) ukiwa haupo, pamoja na CCM.
Wajumbe waliokuwepo walikubaliana kuwa aliyeitisha kikao (THBUB) aandae kikao kingine pamoja na utaratibu (modality) wa kuwakutanisha wajumbe hao tena.
Kupitia taarifa hii ya awali, Chama kinapenda kutaarifu umma wa Watanzania ambao wanafuatilia mijadala ya ujenzi wa demokrasia nchini na kupigania haki zao, ikiwemo operesheni ya UKUTA inayoendelea nchi nzima sasa kuelekea siku ya Septemba 1, kuwa; hakukuwa na makubaliano au maazimio juu ya jambo lolote kadri ya madhumuni ya kuitishwa kwake, kwa kuwa kimsingi kikao hakikufanyika hadi hapo (iwapo) kitakapoitishwa tena.
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA
Kama ilivyotaarifiwa siku chache zilizopita kupitia vyombo kadhaa vya habari na njia zingine za upashanaji habari, THBUB iliandika barua kuitisha kikao leo Agosti 10, 2016, katika ofisi za tume hiyo jijini Dar es Salaam.
Wajumbe wa kikao hicho walialikwa kwa majina na nafasi yao na kwa mujibu wa barua ya wito kutoka THBUB, walikuwa ni wafuatao;
1. Mhe. George Masaju (MB)
Mwanasheria Mkuu wa
Serikali
2. Jaji Francis S.K. Mutungi
Msajili wa Vyama
3. Mr. Abdulrahman Kinana
Katibu Mkuu CCM
4. Dr. Vincent Mashinji
Katibu Mkuu CHADEMA
5. Katibu Mkuu
Tanzania Centre for
Democracy
6. Bw. Ernest Jumbe Mangu
(IGP)
Mkuu wa Jeshi la Polisi
Tanzania
Kwa mujibu wa barua ya wito, dhumuni kuu la kikao ilikuwa ni kujadili "MUSTAKABALI WA MIKUTANO NA MAANDAMANO YA VYAMA VYA SIASA". Vile vile THBUB ilipenda kujadili tangazo la CHADEMA kuhusu kile kinachoitwa "Ukuta" na mikutano iliyopangwa kufanyika tarehe 01 Septemba, 2016 nchi nzima.
CHADEMA ilihudhuria kikao hicho mahali na muda kama ilivyoelezwa kupitia barua ya wito, ikiwakilishwa na Katibu Mkuu Dkt. Mashinji aliyeambatana na wasaidizi wawili.
Hadi muda ambao kikao kilipaswa kuanza, ukumbini kulikuwa na wajumbe 3 pekee ambao ni, Mwenyekiti wa THBUB Bahame Nyanduga, Dkt. Mashinji na Jaji Mutungi.
Baada ya mazungumzo kati ya wajumbe hao watatu, ikakubalika kuwa kikao kiahirishwe kwa sababu kisingeweza kufanyika na kufikia makubaliano au maazimio yoyote yale, huku upande wa Serikali (Mwanasheria Mkuu na IGP) ukiwa haupo, pamoja na CCM.
Wajumbe waliokuwepo walikubaliana kuwa aliyeitisha kikao (THBUB) aandae kikao kingine pamoja na utaratibu (modality) wa kuwakutanisha wajumbe hao tena.
Kupitia taarifa hii ya awali, Chama kinapenda kutaarifu umma wa Watanzania ambao wanafuatilia mijadala ya ujenzi wa demokrasia nchini na kupigania haki zao, ikiwemo operesheni ya UKUTA inayoendelea nchi nzima sasa kuelekea siku ya Septemba 1, kuwa; hakukuwa na makubaliano au maazimio juu ya jambo lolote kadri ya madhumuni ya kuitishwa kwake, kwa kuwa kimsingi kikao hakikufanyika hadi hapo (iwapo) kitakapoitishwa tena.
Tumaini Makene
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano
CHADEMA