Kauli hizi za Magufuli

Kauli hizi za Magufuli

Ngolombwe

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2013
Posts
267
Reaction score
76
Habari za siku wanajukwaa hili, tangu ndugu Magufuli aanze mbio za kuusaka Urais kwa tiketi ya ccm amekuwa na kauli ambayo haachi kuisema kila anapohutubia, "SITAWAANGUSHA" , nimekuwa nikijiuliza sana huwa anawaambia nani hasa? na maana yake hasa ni nini?.
Najaribu kuuangalia mfumo nzima wa utawala ndani ccm, umejaa rushwa, kulindana, kupeana madaraka, wizi kila idara, kutoheshimu katiba na hata taratibu, je hivi ndivyo mh. Magufuli anavyodai hatawaangusha?.
Jamani mwenye tafakuri pana zaidi atusaidie kauli hii ya mgombea huyu wa ccm ambayo kila kukicha haachi kuisema kwenye kila hotuba yake maana yake hasa ni nini? SITAWAANGUSHA!!!!.
 
Kwa kuwa ccm walimchagua kwa kumuamin...hivyo hatawaabisha /hataonekana mzembe kazin
 
hata waangusha mafisadi wenzie. mbona simple sana kumuelewa!
 
Mheshimiwa anasema "hatawaangusha, kwamaana ya kuwa atafanya kazi kwa weledi na kwa kujituma na hata weza waangusha." Keep it up

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Mmekosa matumaini na viongozi waliopita yeye HATOWAANGUSHA
 
ni kweli hatawangusha mana hata yy mwenyewe watampeleka puta akiwafuatilia.jua watu wa chini bila kujali itikadi tutaumi
 
Nilikuja kimya kimya, nikachukua fomu kimya kimya, nikamuomba Mungu kimya kimya, nikarudisha fomu kimya kimya...nikashinda Kupeperusha bendera ya CCM kimya kimya....


Sitawaangushaaa, sitawaangushaaa, kimya kimya, eboooooooooo....!!!

Tell us ur policies, ur areas of priorities, tell us utatufanyia nn..? Just hints, natambua kampeni bado officially, but tupe hints utatufanyia nn, ACHA KUSEMA UTAFUATA ILANI TU YA CCM....yaani utaimeza na kukariri ilani yote ya CCM...? ebooo, ww huna chochote, unameza tu unavyopewa..? Tht is most dangerous...!!!
 
Tingatinga anadai hatatuangusha ilhali wanaomuendesha wameshatuangusha na wamekuwa wakitukanyaga kwa zaidi ya miaka 50 sasa...!!!
 
Alinselema.......aleja,......cjui maana yake nini
 
tingatinga anajua wananchi wanachukia nini ktk tawala zilizopita na wanahitaji nini ndo maana anasema hatatuangusha
 
Najua Magufuli ni mtendaji, ila lazima awe
na 1, 2, 3, 4........ kama mgombea urais, lazima aseme hata kidogo tu, he is like not prepared at all, nataka kujua his areas priorities, ana plan gani, ILANI YA CCM hawezi kumeza tu, yeye anagombea urais sio ubunge, lazima atupe vionjo of his A,B Cs kama akichaguliwa atafanya nn, sio maneno ya jumla jumla hapa...
 
Alikua miongoni mwa wale walio kanyaga maoni ya raia,amekua mbunge zaidi ya miaka nane Haliwai kusikia Richmond alizungumza mini alisikia EPA alifanyaje wakati alikua waziri enzi hizo? Tayari magufuli kasha tuangusha mi naona Alisha waangusha watanzania na kukanyaga katiba yetu
 
Nilikuja kimya kimya, nikachukua fomu kimya kimya, nikamuomba Mungu kimya kimya, nikarudisha fomu kimya kimya...nikashinda Kupeperusha bendera ya CCM kimya kimya....


Sitawaangushaaa, sitawaangushaaa, kimya kimya, eboooooooooo....!!!

Tell us ur policies, ur areas of priorities, tell us utatufanyia nn..? Just hints, natambua kampeni bado officially, but tupe hints utatufanyia nn, ACHA KUSEMA UTAFUATA ILANI TU YA CCM....yaani utaimeza na kukariri ilani yote ya CCM...? ebooo, ww huna chochote, unameza tu unavyopewa..? Tht is most dangerous...!!!

Jay One umeksirika Kimya kimya eboooo!!!! Hivi hujui ILANI ya CCM kweli kabisa!!!!Ndani ya moyo kabisa mimi nitakushangaa ukiniambia kimya kimya eti hujui ILANI yetu Ebooooo.

Basi kimya kimya ILANI ya chama chetu Ni hii:

1.Kuhakikisha rushwa inakuwa zaidi ya hapa ilipofikia maana tunayaendeleza yale ya yule aliyeondoka.

2.Tunafungua soko kuu la madawa ya kulevya actually tunafikiria kufungua kiwanda na kuhakikisha sheria ya kuruhusu dawa za kulevya kutumiwa na kupitishwa kwa kishindo cha kura za ndiyoooooo kushinda bila kupingwa.

3.Kuhakikisha Ufisadi na wizi wa mali za umma unahalalishwa kwa kila mtu kula kadiri ya urefu wa kamba yake na ole wake CAG alete ripoti tofauti.

4.Nyumba zilizobaki zote za serikali kuuzwa na.mojawapo ile nyumba yangu ndogo haikupata nyumba so this time itapata nzuri zaidi.

4.Wawemezaji kupewa kipaumbele haijalishi anataka ardhi ya mlalahoi au mbuga ya wanyama kama ni ya mlala hoi akatafute eneo jingine kwani ardhi ni mali ya serikali hakuna malipo.

5.Sheria ya wapigwe tu itakuwa halali popote pale hata ikibidi bungeni wapinzani wakigoma kupitisha miswada.

6.Miswada yote inayotetea Utaifa kufutwa kwani pesa itakuwa kigezo cha kupata uongozi na masklikini wote yaani watanzania wasio na uwezo wakatafute maeneo mengine ya kuishi na hasa ukwa siyo wa Chama Chetu cha Mafisadi.

7.Wakaskazini wote wajiandae kuondoka hapa siyo nchi yao.

Hii ndiyo ilani ya chama chetu kitukutu cha mabwepande.....
 
Back
Top Bottom