Kauli hii ya Mh. James Lembeli, Ni kweli au?

Kauli hii ya Mh. James Lembeli, Ni kweli au?

frema120

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2012
Posts
5,098
Reaction score
1,341
Wakati jana, akichangia hoja ya inayoendelea bungeni alisema hivi.

"Nchi hii kuna Taasisi mbili tu au tatu zinazoaminika sasa na wananchi, ambazo ni bunge la JMT na JWTZ tu" nilipata mshangao sana wa kauli, hivi ni kweli hakuna taasisi nyingine zinazoaminika na wananchi.....

Kama zipo tuzitaje......
 
Hata hilo BUNGE limeshapoteza CREDIBILITY yake,kwa sasa wataweza kuirudisha kama tu wataliweka sakata hili lijadiliwe kwa UWAZI.wameshindwa watuwekee kwenye Magazeti tujadili wenyewe na mwisho tutoe suluhisho.Lakini kwa sasa hata hizo mbili na zenyewe zipo kwenye ORANGE.
 
Wakati jana, akichangia hoja ya inayoendelea bungeni alisema hivi.

"Nchi hii kuna Taasisi mbili tu au tatu zinazoaminika sasa na wananchi, ambazo ni bunge la JMT na JWTZ tu" nilipata mshangao sanaaa wa kauli, hivi ni kweli hakuna taasisi nyingine zinazoaminika na wananchi.....

Kama zipo tuzitaje......
Utafiti wake sijui kautoa wapi lakini TO BE HONEST JAMES LEMBELI ni mmoja wa wabunge ambao hawaaminiki na si wa kuwaamini.
 
mimi nathani,hakuna zaidi ya jeshi kwani hata bunge, hakuna kitu japo nakiri kuna wabunge smart,ila itikadi za vyama zinafanya tupunguze imani,hasa spika kuwa na chama ndo imani inakwisha kabisa.
 
Alimaanisha hata Ikulu haiaminiki kwa wananchi. Kama mlikuwa mkifuatilia body language, Ndugai alishtuka na ni kama vile alitaka kumkosoa!
 
sina imani jeshi la polisi waccm
 
Wakati jana, akichangia hoja ya inayoendelea bungeni alisema hivi.

"Nchi hii kuna Taasisi mbili tu au tatu zinazoaminika sasa na wananchi, ambazo ni bunge la JMT na JWTZ tu" nilipata mshangao sana wa kauli, hivi ni kweli hakuna taasisi nyingine zinazoaminika na wananchi.....

Kama zipo tuzitaje......

....hili ni dongo la kirejareja kwa JK
 
Sidhani kaka bunge linaaminika kiivyo, makando kando ya ushabiki wa kivyama wa kivyama wa kuacha kutetea maslahi ya chama badala ya maslahi ya taifa ndio yanayoua mchi. Dalili za maovu zinapojitokeza kunakuwa na kejeli hata matusi. Mambo yakiharibika ndipo wanaposhtuka. Hii si sawa!
 
ukweli ndo huo ikulu haiaminiki kaka wala lembeli hakukosea,we fikiria kipindi cha nyuma wanyonge walikua wanategemea kutetewa na kiongozi wa nchi kama alivyokua mwalimu nyerere,alikua anasema kabisa tena bila kutafuna neno kwa ikulu ni mahali patakatifu,na ujue sehemu takatifu ndo sehemu zenye kukimbiliwa na wanyonge,lkn leo ikulu ni ya mabepari na walowezi,
 
hakuna taasisi inayoaminika hao wanajeshi amewaogopa tu, bunge kalitetea kwa sababu naye mbunge ila hakuna nasema tena hakuna.
 
Back
Top Bottom