Kauli ambazo Magufuli pamoja na Trump wanaweza "kuzijutia"!

Kauli ambazo Magufuli pamoja na Trump wanaweza "kuzijutia"!

jmushi1

Platinum Member
Joined
Nov 2, 2007
Posts
26,375
Reaction score
25,453
Wanajamvi,

Kauli za wakuu wa nchi ni nzito sana!Na huwa kauli zozote wanazozitoa, huwa zinachukuliwa kwa uzito wa juu. Iwe ni kutamka kwa mdomo, ama hata kupitia mtandao mfano twitter.

Kwa kiasi kikubwa, kauli ambazo wanazizingumza, huwa zinachukuliwa hatua kwa namna moja ama nyingine. Kutegemeana na mazingira, yaweza kuwa vyombo vya usalama, ama makundi ya “vigilantes”(watu wa kujitolea). Rais Trump na pia Maghufuli, kuna kauli ambazo kwa maoni yangu zitawacost. Pia niseme kuwa kwa kiasi Fulani nakubaliana na baadhi ya washabiki wa Magufuli wanaomfananisha na Trump kweye huo upande wa uzungumzaji! Yani wanasema wanachojisikia kusema wakati wowote mahali popote bila kujali chochote. Trump yeye huwa ni mubashara pamoja na twitter!


Trump kama ilivyo kwa Maghufuli, alizungumza na mara nyingine kwa namna ambayo wanasema ni kwa kutumia “codes”. Yani ikiwa na maana ya kiongozi kuzungumza kwa namna ambayo anataka jambo flani lifanyike, lakini bila ya kusema moja kwa moja. Kwa wamarekani, wale mabosi wa mafia ndiyo walikuwa vinara wa kutumia lugha hizo za codes, pale ambapo wanataka mtu flani auwawe ama kazi flani ifanyike nk.
Mifano ya Trump.

1551745519695.png


Trump yuko matatani sana, lakini sitaki kuzungumzia matatizo yake ambayo hayaendani na mustakabali wa dhana ama hoja ya bandiko hili.

Mwanasheria binafsi wa Trump ambaye alifanya naye kazi kwa miaka takriban kumi, alisema kuwa Trump alimuagiza amlipe muigizaji wa filamu za ngono, anayeitwa Stormy Daniels, ambaye Trump aliwahi kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi wakati akiwa ameoa na mke wake akiwa amejifungua motto wao wa kiume aitwaye Baron. Baada ya huyo mwanasheria wake anayeitwa Michael Cohen kumalizana na mwanasheria wa porn star,pamoja na gazeti la the enquirer, Trump alimwandikia mwanasheria wake cheki kadhaa kwa malipo ya mikupuo minne, ili ioneane kama vile alikuwa akimlipa malipo ya kazi zake.(retention fees). Lakini kumbe ni malipo ambayo walikubaliana ya jumla ya usd 130,000/=. Michael Cohen alitoa ushahidi wake kwenye congress, na alikuja hadi na copy ya cheque ambayo Trump alimuandikia akiwa tayari ni rais na ina saini yake!
190227-donald-trump-michael-cohen-check-2-cs-752a_72b910b14ad7f13a08237951da0cfdda.nbcnews-ux-2880-1000.jpg

Mojawapo ya cheki ambazo rais Trump alimuandikia Michael Cohen kwenye malipo ya kwenda kwa kuigizaji wa filamu za ngono ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Trump. Malipo yalikuwa ni ya kumfunga mdomo huyo mwigizaji pamoja na kulilipa gazeti lile ili kuweza kuinunuwa habari ile kisha kuizika. Cheki hii aliiandika baada ya kuwa rais. Hakumwambia mwanasheria wake moja kwa moja nini kifanyike, bali alitoa kauli za kulalamika na kutokufurahishwa na suala hilo. Hiyo ikawa ni kama amri ya kuwa lishughulikiwe ili lisije kumuharibia mbio za urais. Ikawa ni habari ambayo waliinunuwa kisha wakaizika. Gazeti la "The enquirer" pia linahusika. Gazeti ambalo lilitumika sana na Trump kwa propaganda na kashfa za uongo dhidi ya wapinzani wake. Ni kama ilivyo Tanzanite ya Musiba na Musiba mwenyewe. Ila bosi wa enquirer yeye yuko matatani huko mbele kwasababu demokrasia inafanya kazi.

Pia Trump aliwahi kutamka kuwa anawataka warusi wamsaidie kuzileta email za mgombea wa Democrats! Na haikupita muda, warusi wakatimiza matakwa yake. Hayo yako kwenye uchunguzi hadi sasa. Na kauli yake ni mojawapo ya ushahidi unaotumika dhidi yake na pia iliyopelekea uchunguzi unaoendelea. Pia amekuwa akisema “no collusion” kila mara, na kumsema vibaya yule Mueller!Hizo kauli zake sasa zinachukuliwa kama “obstruction of justice”, na pia ndizo zinasemekana kuwa alimtimuwa yule mkuu wa idara ya FBI, kwasababu alitaka issue ya uchunguzi wa Russia kumsaidia kwenye uchaguzi izikwe na uchunguzi ufe. Kwahiyo hizo kauli zake zinawapa wakati mgumu viongozi aliowateuwa, na hii ni kwasababu ni taifa la demokrasia! Kuna yule aliyekuwa mwanasheria mkuu anayeitwa Jeff Sessions, ambaye Trumo alimfukuza kazi. Na alikuwa akilalamika kwasababu aliji “recuse” kuhusiana na uchunguzi wa Mueller. Hiyo ina maana kuwa hataweza kuitumia nafasi yake ya uanasheria mkuu kumlinda Trump na maovu yake!

Mifano ya kauli za Trump zitakazomponza ni mingi tu, ukifuatilia yale mahojiano ya Michael Cohen kwenye congress, utagundua hilo.

1551745453845.png



Mifano ya Maghufuli

Kwa upande wa rais Maghufuli, kwanza kabisa ni kauli yake ya kuhusu “usaliti”, ambapo alikuwa akimrefer Tundu Lissu kama msaliti, kasha akasema ni msaliti wa nyakati za “vita ya kiuchumi”, msaliti dawa yake ni kuuwawa! Haukupita muda, Lissu akashambuliwa kwenye jaribio la kutaka kumuuwa!

Rais Maghufuli pia alisema “I wish I could be IGP”, ambapo ni kama vile alimaanisha kwamba IGP hafanyi kazi inavyotakiwa. Na ni kwasababu wale waliotuhumiwa na Makonda kuwa wanauza madawa ya kulevya, wakati ule pale central akiwa Gwajima pamoja na yule Yusuph Manji, ambapo yeye gari lake lilioshwa, na wale wanakwaya wa Gwajima wakawa wanaimba pale nje! Mh rais alichukizwa kabisa kuwa kwanini wale wananchi waliruhusiwa kufanya yale. Lakini ukweli ni kwamba hawakuvunja sheria yoyote ile ya nchi. Bali rais alitaka wawe wanyama zaidi. Matokeo yake, mkuu wa mkoa wa Dar kwa kutumia rungu lake la “mwenyekiti wa kamati ya usalama ya mkoa”, akaanza kumuendesha Mambosasa. Nadhani alipata sana uchungu baba yake aliposema yale maneno. Kama makonda huyu huyu ndo yule aliyekuwa mpambe wa Rizmoko, hadi akafuta viatu vyake ama sijui kufunga kamba hadharani, hakuna ajuaye anachokifanya anapokuwa haonekani. Pengine ni mtu hatari sana. Hakuna jambo lolote linalotokea ama kuhusishwa kwa Maghufuli nay eye hayumo. Lakini nilishangazwa na kauli ya rais kuwa “Mambosasa nawaona watanzania wajinga sana”, kuhusiana na ile issue ya kutekwa kwa Mo.

Hata ule uvamizi wa clouds ulianzia huko huko. Kumbuka kuwa ilikuwa ni nia ya Makonda kutaka kipindi kirushwe, ambacho kinahusu mwanamke ambaye anadaiwa kuzaa na Gwajima. Kwa kauli alizokuwa anazisema the late Ruge, utagunduwa alikuwa hataki hayo mambo. Sina uhakika kama walitaka kirushwe kwenye kipindi pendwa cha mh rais cha Shilawadu! Inavyosemekana, mkulu mwenyewe alishajipanga na popcorns kabisa! Ilipobuma, akamwambia “kijana piga kazi”!, baada ya kelele kuzidi, “akawapatanisha” kule Tanga ambapo walishikana mikono. Lakini baada ya hapo uahasama uliendelea kama kawaida. Kwenye ile press conference ya TEF wote tuliona.

Kama kuna wengine ambao mnakumbuka kauli ambazo zitawaponza hawa viongozi hao, ambao mashabiki wa rais Maghfuli wanapenda kuwafananisha, please share with us.


Rais Trump akiwa na Michael Cohen aliyekuwa mtu anayefahamu siri zote za Trump zile chafu!

1551745933952.png

Rais Maghufuli na Makonda, need I say more?

Hitimisho.
Tofauti iliyopo kati ya situation hizo mbili, ni kuwa marekani, “No one is above the law”
1551745855687.png
 
MAGUFULI.

Askari Polisi mnapokuwa mnapambana na majambazi, kwanini hamuwanyang'anyi silaha haraka haraka. Nadhani mmenielewa.

Kuanzia sasa sitaki kusikia Askari Polisi anafunguliwa mashtaka yoyote kwa kosa lolote atakalofanya akiwa kwenye majukumu yake. RIP Akwilina

Pesa wanayochukua traffic barabarani ni pesa ya kubrush viatu.

Lowassa nenda kawaambie wataishia jera.

Wafungwa walime na mnatakiwa kuwa mnawapiga mateke, hakuna kula bure. Nataka wamenyeke kweli kweli. Serikali haiwezi kulisha wafungwa. Nataka wamenyeke hasa.

Kuna mijitu mingine inaongea inapokuwa bungeni inadhani nitaiteua, sitaiteua.

Kama walitaka kuandamana, wangeamana waone ningeanza kupiga shangazi zao. Na ningefukuza wote, hata wewe waziri mkuu kukufukuza sioni kazi. #Korosho.

TRUMP

Show me any country that is led by a black president that ain't shithole ?

Why is North Korea Kim Jung-un isulting me by calling me OLD when i would never call him SHORT and FAT ?
Oh, well i try so hard to be his friend.
 
MAGUFULI.

Askari Polisi mnapokuwa mnapambana na majambazi, kwanini hamuwanyang'anyi silaha haraka hara. Nadhani mmenielewa.

Kuanzia sasa sitaki kusikia Askari Polisi anafunguliwa mashtaka yoyote kwa kosa lolote atakalofanya akiwa kwenye majukumu yake. RIP Akwilina

Pesa wanayochukua traffic barabarani ni pesa ya kubrush viatu.

Lowassa nenda kawaambie wataishia jera.

Wafungwa walime na mnatakiwa kuwa mnawapiga mateke, hakuna kula bure. Nataka wamenyeke kweli kweli. Serikali haiwezi kulisha wafungwa. Nataka wamenyeke hasa.
right on money! Hata Trump aliwahi kusema hao polisi wanawabembeleza sana watuhumiwa wanapowakamata! Sasa ikaja ikatokea rafiki yake ambaye aliwahi kuwa meneja wake wa kampeni,anaitwa Paul Manafort, na ambaye anasubiria hukumu kubwa pengine jela kwa maisha yake yote, pamoja na mshauri wake Trump mkuu anayeitwa Roger Stones! Ambaye ndiye aliyemshawishi kugombea urais! Walivamiwa na FBI kama vile magaidi wanavyovamiwa! Trump analalamika vibaya! 😂kumbe alitaka wafanyiwe wale tu ambao siyo watu wake!😳
 
right on money! Hata Trump aliwahi kusema hao polisi wanawabembeleza sana watuhumiwa wanapowakamata! Sasa ikaja ikatokea rafiki yake ambaye aliwahi kuwa meneja wake wa kampeni,anaitwa Paul Manafort, na ambaye anasubiria hukumu kubwa pengine jela kwa maisha yake yote, pamoja na mshauri wake Trump mkuu anayeitwa Roger Stones! Ambaye ndiye aliyemshawishi kugombea urais! Walivamiwa na FBI kama vile magaidi wanavyovamiwa! Trump analalamika vibaya!
Ukuta atakwama ingawa analazimisha sana.

Akomae na China labda ataacha legacy yoyote.


Hayo ndio madhara ya kukomaa na sera za VIJIWENI.
 
Mleta mada umetoa mifano mizuuuri sana kwa TRUMP ila kwa MAGUFULI umeonesha wewe ni NYUMBU jike pia.
Duh! Labda unamaanisha sijatoa mifano ya kutosha kuhusu jiwe? Stupid wewe!
 
Wewe KANYAMA , hii ninJF, kuna watu huwa wanaona mbele kuliko wengine! Ndiyo maana kuna kitu kinaitwa “Makaburi”, kwa wale musio na uwezo wa kuona right away, mtakuja kufukua makaburi. Tutajazia nyama kwenye skeleton!
 
Wanajamvi,

Kauli za wakuu wa nchi ni nzito sana!Na huwa kauli zozote wanazozitoa, huwa zinachukuliwa kwa uzito wa juu. Iwe ni kutamka kwa mdomo, ama hata kupitia mtandao mfano twitter.

Kwa kiasi kikubwa, kauli ambazo wanazizingumza, huwa zinachukuliwa hatua kwa namna moja ama nyingine. Kutegemeana na mazingira, yaweza kuwa vyombo vya usalama, ama makundi ya “vigilantes”(watu wa kujitolea). Rais Trump na pia Maghufuli, kuna kauli ambazo kwa maoni yangu zitawacost. Pia niseme kuwa kwa kiasi Fulani nakubaliana na baadhi ya washabiki wa Magufuli wanaomfananisha na Trump kweye huo upande wa uzungumzaji! Yani wanasema wanachojisikia kusema wakati wowote mahali popote bila kujali chochote. Trump yeye huwa ni mubashara pamoja na twitter!


Trump kama ilivyo kwa Maghufuli, alizungumza na mara nyingine kwa namna ambayo wanasema ni kwa kutumia “codes”. Yani ikiwa na maana ya kiongozi kuzungumza kwa namna ambayo anataka jambo flani lifanyike, lakini bila ya kusema moja kwa moja. Kwa wamarekani, wale mabosi wa mafia ndiyo walikuwa vinara wa kutumia lugha hizo za codes, pale ambapo wanataka mtu flani auwawe ama kazi flani ifanyike nk.
Mifano ya Trump.

View attachment 1038150

Trump yuko matatani sana, lakini sitaki kuzungumzia matatizo yake ambayo hayaendani na mustakabali wa dhana ama hoja ya bandiko hili.

Mwanasheria binafsi wa Trump ambaye alifanya naye kazi kwa miaka takriban kumi, alisema kuwa Trump alimuagiza amlipe muigizaji wa filamu za ngono, anayeitwa Stormy Daniels, ambaye Trump aliwahi kuwa na mahusiano naye ya kimapenzi wakati akiwa ameoa na mke wake akiwa amejifungua motto wao wa kiume aitwaye Baron. Baada ya huyo mwanasheria wake anayeitwa Michael Cohen kumalizana na mwanasheria wa porn star,pamoja na gazeti la the enquirer, Trump alimwandikia mwanasheria wake cheki kadhaa kwa malipo ya mikupuo minne, ili ioneane kama vile alikuwa akimlipa malipo ya kazi zake.(retention fees). Lakini kumbe ni malipo ambayo walikubaliana ya jumla ya usd 130,000/=. Michael Cohen alitoa ushahidi wake kwenye congress, na alikuja hadi na copy ya cheque ambayo Trump alimuandikia akiwa tayari ni rais na ina saini yake!
190227-donald-trump-michael-cohen-check-2-cs-752a_72b910b14ad7f13a08237951da0cfdda.nbcnews-ux-2880-1000.jpg

Mojawapo ya cheki ambazo rais Trump alimuandikia Michael Cohen kwenye malipo ya kwenda kwa kuigizaji wa filamu za ngono ambaye alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Trump. Malipo yalikuwa ni ya kumfunga mdomo huyo mwigizaji pamoja na kulilipa gazeti lile ili kuweza kuinunuwa habari ile kisha kuizika. Cheki hii aliiandika baada ya kuwa rais. Hakumwambia mwanasheria wake moja kwa moja nini kifanyike, bali alitoa kauli za kulalamika na kutokufurahishwa na suala hilo. Hiyo ikawa ni kama amri ya kuwa lishughulikiwe ili lisije kumuharibia mbio za urais. Ikawa ni habari ambayo waliinunuwa kisha wakaizika. Gazeti la "The enquirer" pia linahusika. Gazeti ambalo lilitumika sana na Trump kwa propaganda na kashfa za uongo dhidi ya wapinzani wake. Ni kama ilivyo Tanzanite ya Musiba na Musiba mwenyewe. Ila bosi wa enquirer yeye yuko matatani huko mbele kwasababu demokrasia inafanya kazi.

Pia Trump aliwahi kutamka kuwa anawataka warusi wamsaidie kuzileta email za mgombea wa Democrats! Na haikupita muda, warusi wakatimiza matakwa yake. Hayo yako kwenye uchunguzi hadi sasa. Na kauli yake ni mojawapo ya ushahidi unaotumika dhidi yake na pia iliyopelekea uchunguzi unaoendelea. Pia amekuwa akisema “no collusion” kila mara, na kumsema vibaya yule Mueller!Hizo kauli zake sasa zinachukuliwa kama “obstruction of justice”, na pia ndizo zinasemekana kuwa alimtimuwa yule mkuu wa idara ya FBI, kwasababu alitaka issue ya uchunguzi wa Russia kumsaidia kwenye uchaguzi izikwe na uchunguzi ufe. Kwahiyo hizo kauli zake zinawapa wakati mgumu viongozi aliowateuwa, na hii ni kwasababu ni taifa la demokrasia! Kuna yule aliyekuwa mwanasheria mkuu anayeitwa Jeff Sessions, ambaye Trumo alimfukuza kazi. Na alikuwa akilalamika kwasababu aliji “recuse” kuhusiana na uchunguzi wa Mueller. Hiyo ina maana kuwa hataweza kuitumia nafasi yake ya uanasheria mkuu kumlinda Trump na maovu yake!

Mifano ya kauli za Trump zitakazomponza ni mingi tu, ukifuatilia yale mahojiano ya Michael Cohen kwenye congress, utagundua hilo.

View attachment 1038149


Mifano ya Maghufuli

Kwa upande wa rais Maghufuli, kwanza kabisa ni kauli yake ya kuhusu “usaliti”, ambapo alikuwa akimrefer Tundu Lissu kama msaliti, kasha akasema ni msaliti wa nyakati za “vita ya kiuchumi”, msaliti dawa yake ni kuuwawa! Haukupita muda, Lissu akashambuliwa kwenye jaribio la kutaka kumuuwa!

Rais Maghufuli pia alisema “I wish I could be IGP”, ambapo ni kama vile alimaanisha kwamba IGP hafanyi kazi inavyotakiwa. Na ni kwasababu wale waliotuhumiwa na Makonda kuwa wanauza madawa ya kulevya, wakati ule pale central akiwa Gwajima pamoja na yule Yusuph Manji, ambapo yeye gari lake lilioshwa, na wale wanakwaya wa Gwajima wakawa wanaimba pale nje! Mh rais alichukizwa kabisa kuwa kwanini wale wananchi waliruhusiwa kufanya yale. Lakini ukweli ni kwamba hawakuvunja sheria yoyote ile ya nchi. Bali rais alitaka wawe wanyama zaidi. Matokeo yake, mkuu wa mkoa wa Dar kwa kutumia rungu lake la “mwenyekiti wa kamati ya usalama ya mkoa”, akaanza kumuendesha Mambosasa. Nadhani alipata sana uchungu baba yake aliposema yale maneno. Kama makonda huyu huyu ndo yule aliyekuwa mpambe wa Rizmoko, hadi akafuta viatu vyake ama sijui kufunga kamba hadharani, hakuna ajuaye anachokifanya anapokuwa haonekani. Pengine ni mtu hatari sana. Hakuna jambo lolote linalotokea ama kuhusishwa kwa Maghufuli nay eye hayumo. Lakini nilishangazwa na kauli ya rais kuwa “Mambosasa nawaona watanzania wajinga sana”, kuhusiana na ile issue ya kutekwa kwa Mo.

Hata ule uvamizi wa clouds ulianzia huko huko. Kumbuka kuwa ilikuwa ni nia ya Makonda kutaka kipindi kirushwe, ambacho kinahusu mwanamke ambaye anadaiwa kuzaa na Gwajima. Kwa kauli alizokuwa anazisema the late Ruge, utagunduwa alikuwa hataki hayo mambo. Sina uhakika kama walitaka kirushwe kwenye kipindi pendwa cha mh rais cha Shilawadu! Inavyosemekana, mkulu mwenyewe alishajipanga na popcorns kabisa! Ilipobuma, akamwambia “kijana piga kazi”!, baada ya kelele kuzidi, “akawapatanisha” kule Tanga ambapo walishikana mikono. Lakini baada ya hapo uahasama uliendelea kama kawaida. Kwenye ile press conference ya TEF wote tuliona.

Kama kuna wengine ambao mnakumbuka kauli ambazo zitawaponza hawa viongozi hao, ambao mashabiki wa rais Maghfuli wanapenda kuwafananisha, please share with us.


Rais Trump akiwa na Michael Cohen aliyekuwa mtu anayefahamu siri zote za Trump zile chafu!

View attachment 1038153
Rais Maghufuli na Makonda, need I say more?

Hitimisho.
Tofauti iliyopo kati ya situation hizo mbili, ni kuwa marekani, “No one is above the law”View attachment 1038152
Hakuna kauli tata yoyote ya Magufuli na hakuna popote utasimama kisheria ukashinda. Utata unaletwa na propaganda za bavicha. Wao kila kauli ya jpm ni tata na imejaa chuki. Hakuna sehem wananchi wameondoka kwa huzuni au kukasirishwa baada ya jpm kuhutubia. Chuki zinaanza pale speech ya jpm ikipitia ufipa na kuhaririwa kwa propaganda.Kuna mwenzio leo nimemwambia alete clip jpm akisema matajiri wataishi kama mashetani na kashindwa lkn kwenye Hansard za ufipa zipo. Ni kauli nyingi sana za jpm huwa mnazipotosha kwa makusudi ili mjenge chuki za kisiasa.

Hili la makonda kuhusu clouds nimelijibu jana na nilitegemea uje na hoja zako lkn kwakua ni mwendelezo wa propaganda uchwara ukaingia mitini.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
 
Hakuna kauli tata yoyote ya Magufuli na hakuna popote utasimama kisheria ukashinda. Utata unaletwa na propaganda za bavicha. Wao kila kauli ya jpm ni tata na imejaa chuki. Hakuna sehem wananchi wameondoka kwa huzuni au kukasirishwa baada ya jpm kuhutubia. Chuki zinaanza pale speech ya jpm ikipitia ufipa na kuhaririwa kwa propaganda.Kuna mwenzio leo nimemwambia alete clip jpm akisema matajiri wataishi kama mashetani na kashindwa lkn kwenye Hansard za ufipa zipo. Ni kauli nyingi sana za jpm huwa mnazipotosha kwa makusudi ili mjenge chuki za kisiasa.

Hili la makonda kuhusu clouds nimelijibu jana na nilitegemea uje na hoja zako lkn kwakua ni mwendelezo wa propaganda uchwara ukaingia mitini.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
Mimi niingie mitini? Maisha!

Kuhusu hizo kauli, hata Trump anasema kuwa alikuwa “anatania”, hakumaanisha warusi wafanye kweli!

Kwenye ile thread ya makonda, hukujibu wala kuelezea upande wa Makonda ambao alisema haujasikilizwa na ndiyo maana hataki kuomba radhi! Sasa ule waraka ulioubandika, haukujibu chochote zaidi ya kuelezea matatizo ya Nape!

Mimi huwa lazima nijibu kutokana na bandiko lako, yani hoja kwa hoja!

Mimi sina nia ya kujenga chuki za kisiasa. Nimeweka kauli zote hapa ambazo zinahusiana na hoja yangu. Sasa kama kauli hizo zilikuwa na maana nyingine, unachotakiwa kufanya ni kujibu kwa kuelezea maana yake. Na kuelezea kwanini tafsiri yangu mimi ni potofu na ya kwako wewe ni sahihi! Ndo JF ninayoufahamu inavyo operate!
 
Mimi niingie mitini? Maisha!

Kuhusu hizo kauli, hata Trump anasema kuwa alikuwa “anatania”, hakumaanisha warusi wafanye kweli!

Kwenye ile thread ya makonda, hukujibu wala kuelezea upande wa Makonda ambao alisema haujasikilizwa na ndiyo maana hataki kuomba radhi! Sasa ule waraka ulioubandika, haukujibu chochote zaidi ya kuelezea matatizo ya Nape!

Mimi huwa lazima nijibu kutokana na bandiko lako, yani hoja kwa hoja!

Mimi sina nia ya kujenga chuki za kisiasa. Nimeweka kauli zote hapa ambazo zinahusiana na hoja yangu. Sasa kama kauli hizo zilikuwa na maana nyingine, unachotakiwa kufanya ni kujibu kwa kuelezea maana yake. Na kuelezea kwanini tafsiri yangu mimi ni potofu na ya kwako wewe ni sahihi! Ndo JF ninayoufahamu inavyo operate!
Hawezi kujibu hoja zako...so far alishakula kona

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna kauli tata yoyote ya Magufuli na hakuna popote utasimama kisheria ukashinda. Utata unaletwa na propaganda za bavicha. Wao kila kauli ya jpm ni tata na imejaa chuki. Hakuna sehem wananchi wameondoka kwa huzuni au kukasirishwa baada ya jpm kuhutubia. Chuki zinaanza pale speech ya jpm ikipitia ufipa na kuhaririwa kwa propaganda.Kuna mwenzio leo nimemwambia alete clip jpm akisema matajiri wataishi kama mashetani na kashindwa lkn kwenye Hansard za ufipa zipo. Ni kauli nyingi sana za jpm huwa mnazipotosha kwa makusudi ili mjenge chuki za kisiasa.

Hili la makonda kuhusu clouds nimelijibu jana na nilitegemea uje na hoja zako lkn kwakua ni mwendelezo wa propaganda uchwara ukaingia mitini.

The problem with the world is that the intelligent people are full of doubts, while the stupid ones are full ofconfidence.
Kuna watu wanadhani watanzania ni wajinga sana.
Hawajui kila uchwao wanazidi kupata akili

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom