funaku
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 38,534
- 31,198
Katika hili nitsimama na Rais Samia na kumpongeza sana.
Fedha za covid zililengwa kutumika katika ununuzi na utekekezaji wa mambo yasiyoonekana kwa wananchi.
Nchi nyingi zilitumia fedha hii kulipa perdiems ,utafiti usioeleweka,harakati za chanjo au ununuzi wa medical supplies ambapo leo hii ukitrace hutapata jibu la maana.
Kwa upande wa Tanzania Rais Samia analo la kuonesha namna alivyotumia fedha za Covid 19.
Yapo madarasa mengi sana yaliyojengwa nchi nzima kupitia fedha hizi. Yapo majengo ya huduma za dharura ngazi zote yaani rufaa,mkoa na wilaya. pia yapo majengo ya huduma za mahututi yaani ICU yaliyojengwa kwa fedha hizi.
Ni muhuni tu ndio anayeweza kusema fedha hizi hazijaacha alama hapa nchini na duniani.
Nenda Kenya uulize fedha za Covid 19 zipo wapi?
MUHUNI KALISHWA TANGO PORI NA YEYE KALIMEZA ZIMA ZIMA!
zaidi muhuni mkuu anawaumbua waliompa taarifa.
HAPA CHINI NI SEHEMU YA TAARIFA ILIYOTOLEWA BUNGENI NA WIZARA YA FEDHA......
"Serikali imetumia fedha za UVIKO-19 kiasi cha shilingi trilioni 1.29 zilizotolewa kama mkopo nafuu na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kutekeleza mirandi katika sekta za maji, elimu, utalii, afya na uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Hayo yameelezwa bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalaum, Mhe. Nusrat Shaaban Hanje, aliyetaka kufahamu miradi iliyotekelezwa kwa fedha za Uviko – 19
Mhe. Chande alisema kuwa katika Sekta ya Maji, fedha za mkopo zilitumika kununua mitambo 25 ya kuchimba visima, seti tano za mitambo ya kuchimba na kujenga mabwawa, seti nne za vifaa vya uchunguzi wa maji chini ya ardhi na miradi ya maji 172 vijijini na miradi 46 mijini.
Alisema Sekta ya elimu yalijengwa madarasa 12,000 (shule za sekondari) na 3,000 (shule za msingi shikizi), ukamilishaji wa vyuo vinne vya VETA ngazi ya mikoa na vyuo 25 ngazi ya wilaya na ununuzi wa vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwenye vyuo 11 vya elimu ya juu.
Sekta zingine zilizotumia mkopo wa Uviko – 19 ni pamoja na Sekta ya Utalii ambapo mitambo mitano (5) ilinunuliwa kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu kwenye hifadhi 13 za Taifa na kuimarisha mifumo ya utangazaji wa fursa za utalii ikiwemo The Royal Tour.
Kwa upande wa sekta ya Sekta ya Afya, Mhe. Chande alisema miradi iliyotekelezwa ni ujenzi na ukarabati wa vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali 70 na miundombinu ya kutolea Huduma za Dharura (EMD) katika hospitali 101, ununuzi wa X-ray 169, CT-Scan 29, MRI nne na mashine za huduma za uchunguzi wa moyo -Echo Cardiography 7 na ujenzi wa nyumba 150 za wafanyakazi.
“Fedha za mkopo zilitumika katika uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ambapo Serikali imeboresha miundombinu na mazingira ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogo (wamachinga) eneo la Bahi Road Dodoma, Halmashauri za Majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Tanga, Mbeya, Morogoro pamoja na Halmashauri za Manispaa ya Kinondoni, Temeke na Ubungo mkoani Dar es Salaam” Aliongeza Mhe. Chande
Naibu Waziri Mhe. Chande alisema shilingi bilioni 5.542 zimetumika kusaidia kaya maskini 51,290 zilizotambuliwa katika halmashauri 35 kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF)."
Fedha za covid zililengwa kutumika katika ununuzi na utekekezaji wa mambo yasiyoonekana kwa wananchi.
Nchi nyingi zilitumia fedha hii kulipa perdiems ,utafiti usioeleweka,harakati za chanjo au ununuzi wa medical supplies ambapo leo hii ukitrace hutapata jibu la maana.
Kwa upande wa Tanzania Rais Samia analo la kuonesha namna alivyotumia fedha za Covid 19.
Yapo madarasa mengi sana yaliyojengwa nchi nzima kupitia fedha hizi. Yapo majengo ya huduma za dharura ngazi zote yaani rufaa,mkoa na wilaya. pia yapo majengo ya huduma za mahututi yaani ICU yaliyojengwa kwa fedha hizi.
Ni muhuni tu ndio anayeweza kusema fedha hizi hazijaacha alama hapa nchini na duniani.
Nenda Kenya uulize fedha za Covid 19 zipo wapi?
MUHUNI KALISHWA TANGO PORI NA YEYE KALIMEZA ZIMA ZIMA!
zaidi muhuni mkuu anawaumbua waliompa taarifa.
HAPA CHINI NI SEHEMU YA TAARIFA ILIYOTOLEWA BUNGENI NA WIZARA YA FEDHA......
"Serikali imetumia fedha za UVIKO-19 kiasi cha shilingi trilioni 1.29 zilizotolewa kama mkopo nafuu na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF), kutekeleza mirandi katika sekta za maji, elimu, utalii, afya na uwezeshaji wananchi kiuchumi.
Hayo yameelezwa bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalaum, Mhe. Nusrat Shaaban Hanje, aliyetaka kufahamu miradi iliyotekelezwa kwa fedha za Uviko – 19
Mhe. Chande alisema kuwa katika Sekta ya Maji, fedha za mkopo zilitumika kununua mitambo 25 ya kuchimba visima, seti tano za mitambo ya kuchimba na kujenga mabwawa, seti nne za vifaa vya uchunguzi wa maji chini ya ardhi na miradi ya maji 172 vijijini na miradi 46 mijini.
Alisema Sekta ya elimu yalijengwa madarasa 12,000 (shule za sekondari) na 3,000 (shule za msingi shikizi), ukamilishaji wa vyuo vinne vya VETA ngazi ya mikoa na vyuo 25 ngazi ya wilaya na ununuzi wa vifaa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu kwenye vyuo 11 vya elimu ya juu.
Sekta zingine zilizotumia mkopo wa Uviko – 19 ni pamoja na Sekta ya Utalii ambapo mitambo mitano (5) ilinunuliwa kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu kwenye hifadhi 13 za Taifa na kuimarisha mifumo ya utangazaji wa fursa za utalii ikiwemo The Royal Tour.
Kwa upande wa sekta ya Sekta ya Afya, Mhe. Chande alisema miradi iliyotekelezwa ni ujenzi na ukarabati wa vyumba vya wagonjwa mahututi (ICU) katika hospitali 70 na miundombinu ya kutolea Huduma za Dharura (EMD) katika hospitali 101, ununuzi wa X-ray 169, CT-Scan 29, MRI nne na mashine za huduma za uchunguzi wa moyo -Echo Cardiography 7 na ujenzi wa nyumba 150 za wafanyakazi.
“Fedha za mkopo zilitumika katika uwezeshaji wa wananchi kiuchumi ambapo Serikali imeboresha miundombinu na mazingira ya kufanyia biashara kwa wafanyabiashara wadogo (wamachinga) eneo la Bahi Road Dodoma, Halmashauri za Majiji ya Dar es Salaam, Mwanza, Arusha, Tanga, Mbeya, Morogoro pamoja na Halmashauri za Manispaa ya Kinondoni, Temeke na Ubungo mkoani Dar es Salaam” Aliongeza Mhe. Chande
Naibu Waziri Mhe. Chande alisema shilingi bilioni 5.542 zimetumika kusaidia kaya maskini 51,290 zilizotambuliwa katika halmashauri 35 kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Tanzania (TASAF)."