Katibu Mkuu Kiongozi ni cheo kilicho juu ya fikra za udini

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,487
13,611
Nimekuwa nikayatazama majina ya makatibu wakuu viongozi tangu tupate uhuru, sijaona jina la muislam. Lakini katika marais wanne walioiongoza nchi hii mpaka leo hii kuna waislam wawili. Mzee Mwinyi alimuamini Paul Rupia, akampatia cheo cha katibu mkuu kiongozi. Mzee Kikwete alimuamini Mzee Philemon Luhanjo na akampatia wadhifa huo wa CS.

Humu jamii forum watu hutokwa povu kila wanapotazama vyeo vya mashirika makubwa. Watu wanaandaa excel sheets zinazoonyesha wingi wa wakristo kulinganisha na waislam. Inajengwa hoja kwamba ipo aina fulani ya dhuluma dhidi ya wasomi waislam. Lakini miaka 20 ya urais wa Mwinyi na Kikwete, uliwategemea makatibu wakuu viongozi ambao ni wakristo. Mzee Mwinyi na Mzee Kikwete waliwaamini wakristo, wala hawakuongozwa na fikra za kidini, walitazama utendaji kazi badala ya kutazama dini zao.

Fikra za kidini ni fikra muflis, hazifai kabisa kuendekezwa, na mara nyingi huashiria uvivu wa mtu kufikiria mambo ya maana yenye tija maishani mwake. Baba yangu mzazi aliwahi kuniambia kwamba tarehe 8 desemba 1961 yaani siku moja kabla ya uhuru, nchi hii ilikabidhiwa kwa Mungu, waislam waliikabidhi nchi kwa Mungu kivyao, na wakristo wakaikabidhi kwa Mungu kivyao. Ulikuwa ni uamuzi uliotazama mbali sana, la sivyo Tanzania ingeshameguka vipande vipande kwa sababu ya fikra potofu za udini.

Watoto wasome kwa nguvu zao zote ili baadae CV zao ziweze kuwapatia ajira, wawe wanaswali Ijumaa au wanasali Jumapili, sio kigezo cha wao kuajiriwa. Njia za mkato maishani mara nyingi humjaza mtu hasira, kwani zinaweza kumpeleka mtu mahali ambapo hakutaka kwenda. Mungu ibariki Tanzania.
 
Nimekuwa nikayatazama majina ya makatibu wakuu viongozi tangu tupate uhuru, sijaona jina la muislam. Lakini katika marais wanne walioiongoza nchi hii mpaka leo hii kuna waislam wawili. Mzee Mwinyi alimuamini Paul Rupia, akampatia cheo cha katibu mkuu kiongozi. Mzee Kikwete alimuamini Mzee Philemon Luhanjo na akampatia wadhifa huo wa CS.

Humu jamii forum watu hutokwa povu kila wanapotazama vyeo vya mashirika makubwa. Watu wanaandaa excel sheets zinazoonyesha wingi wa wakristo kulinganisha na waislam. Inajengwa hoja kwamba ipo aina fulani ya dhuluma dhidi ya wasomi waislam. Lakini miaka 20 ya urais wa Mwinyi na Kikwete, uliwategemea makatibu wakuu viongozi ambao ni wakristo. Mzee Mwinyi na Mzee Kikwete waliwaamini wakristo, wala hawakuongozwa na fikra za kidini, walitazama utendaji kazi badala ya kutazama dini zao.

Fikra za kidini ni fikra muflis, hazifai kabisa kuendekezwa, na mara nyingi huashiria uvivu wa mtu kufikiria mambo ya maana yenye tija maishani mwake. Baba yangu mzazi aliwahi kuniambia kwamba tarehe 8 desemba 1961 yaani siku moja kabla ya uhuru, nchi hii ilikabidhiwa kwa Mungu, waislam waliikabidhi nchi kwa Mungu kivyao, na wakristo wakaikabidhi kwa Mungu kivyao. Ulikuwa ni uamuzi uliotazama mbali sana, la sivyo Tanzania ingeshameguka vipande vipande kwa sababu ya fikra potofu za udini.

Watoto wasome kwa nguvu zao zote ili baadae CV zao ziweze kuwapatia ajira, wawe wanaswali Ijumaa au wanasali Jumapili, sio kigezo cha wao kuajiriwa. Njia za mkato maishani mara nyingi humjaza mtu hasira, kwani zinaweza kumpeleka mtu mahali ambapo hakutaka kwenda. Mungu ibariki Tanzania.
Well Said Mkuu, Fikra za kidini ni mufilisi
 
Povu mlianza kutoa nyinyi juu ya NSSF, sasa jana mtu amekuja na data juu ya hali ilivyo TANESCO mnajaribu kufukia ukweli! issue kuwa waislam hawajasoma ni issue ilopitwa na wakati sana sana, na ni uongo kuiendeleza, a lot of PhD, Masters na Bachelor graduateds wa kiislam wapo tu mtaani, i know hundreads of them!
kawasaidie sasa hao waislamu wenzako
 
Mkulo alikwa mwislamu wakati anaongoza NSSF mbona hakuna mtu aliyemlaumu kwa udini tatizo linakuja pale mtu anapotumia dini kama kigezo ila dini siyo kigezo cha kufanya mtu ateuliwa bali sifa na uwezo wake wengi wanaojadili dini ni watu ambao hawajaelimika
 
Tukitaka ukweli UDINI UPO TANZANIA, ukiangalia takwimu za Serikali zote zilizotawala Tanzania tokea tupate UHURU basi nafasi nyingi Serekalini zimekuwa zikianguka mikononi mwa Wakitisto hii kama kwamba wao kiidadi ya watu wapi wengi hapa Tanzania wakati ni kinyume chake. Waisilamu wasomi na wenye sifa za kukamata nafasi muhimu serekalini wapo wengi tu. Lakini sifikirii kama hili suala linatokezea kwa bahati mbaya bali hii ni mipango inayofanywa kwa makusudi na cha kushangaza unapoongea ukweli kuhusu mada hii huwa unaambiwa unaleta UDINI kwa maana fumba mdomo wako na endelea kuridhika na upendeleo wa Wakiristo tu
 
Mkulo alikwa mwislamu wakati anaongoza NSSF mbona hakuna mtu aliyemlaumu kwa udini tatizo linakuja pale mtu anapotumia dini kama kigezo ila dini siyo kigezo cha kufanya mtu ateuliwa bali sifa na uwezo wake wengi wanaojadili dini ni watu ambao hawajaelimika

kwani bado issue ya udini wa nnsf inaendelea mmeambiwa leteni ushahidi kama mwenzenu aliyeleta wa Tanesco.Na kuhusu mkulo hakufanya cha maana nssf kama dau
 
Miaka 20 ya rais muislam bado mkristo akaonekana anafaa. Maana yake hawa wanaouza wazo la udini ni watu waliofilisika vichwani. Ndugu yangu utoto wangu mimi ulikuwa ni enzi za Nyerere. Darasani tulikuwa mchanganyiko wa waislam na wakristo, na waislam niliosoma nao leo hii ni watu wa maana nchini mwetu. Pelekeni watoto zenu shuleni, punguzeni kuiamini sana elimu ya madrasa, katika dunia ya ushindani wa sayansi na teknolojia elimu ya madrasa wala haina mashiko. Ni wale waliofilisika vichwani ndio wenye kuweza kudhani kwamba hawapati kazi kwa sababu ya dini zao. Tunaishi katika mfumo wa kisekula, hivyo msipojichanganya imekula kwenu mazima.
Kwa hiyo Dr dau na maafisa Wengine waliopo pale NSSF ambao ni waislamu hawakupelekwa shule bali wana elimu ya madarasa tu na ndio maana mnalaumu kuwa NSSF Kuna udini!
 
Udini sijui ukabila ni upumbavu..... naskia kichefuchefu kujadili sijui waislam this wakristo that....

Na hapa ni jamiiforums ambapo kuna presumption kuwa ni hom of great thinkers... je kule facebook?
 
Nimekuwa nikayatazama majina ya makatibu wakuu viongozi tangu tupate uhuru, sijaona jina la muislam. Lakini katika marais wanne walioiongoza nchi hii mpaka leo hii kuna waislam wawili. Mzee Mwinyi alimuamini Paul Rupia, akampatia cheo cha katibu mkuu kiongozi. Mzee Kikwete alimuamini Mzee Philemon Luhanjo na akampatia wadhifa huo wa CS.

Humu jamii forum watu hutokwa povu kila wanapotazama vyeo vya mashirika makubwa. Watu wanaandaa excel sheets zinazoonyesha wingi wa wakristo kulinganisha na waislam. Inajengwa hoja kwamba ipo aina fulani ya dhuluma dhidi ya wasomi waislam. Lakini miaka 20 ya urais wa Mwinyi na Kikwete, uliwategemea makatibu wakuu viongozi ambao ni wakristo. Mzee Mwinyi na Mzee Kikwete waliwaamini wakristo, wala hawakuongozwa na fikra za kidini, walitazama utendaji kazi badala ya kutazama dini zao.

Fikra za kidini ni fikra muflis, hazifai kabisa kuendekezwa, na mara nyingi huashiria uvivu wa mtu kufikiria mambo ya maana yenye tija maishani mwake. Baba yangu mzazi aliwahi kuniambia kwamba tarehe 8 desemba 1961 yaani siku moja kabla ya uhuru, nchi hii ilikabidhiwa kwa Mungu, waislam waliikabidhi nchi kwa Mungu kivyao, na wakristo wakaikabidhi kwa Mungu kivyao. Ulikuwa ni uamuzi uliotazama mbali sana, la sivyo Tanzania ingeshameguka vipande vipande kwa sababu ya fikra potofu za udini.

Watoto wasome kwa nguvu zao zote ili baadae CV zao ziweze kuwapatia ajira, wawe wanaswali Ijumaa au wanasali Jumapili, sio kigezo cha wao kuajiriwa. Njia za mkato maishani mara nyingi humjaza mtu hasira, kwani zinaweza kumpeleka mtu mahali ambapo hakutaka kwenda. Mungu ibariki Tanzania.
Mkuu haya mawazo yako mbona hatukuyaona kwenye nyuzi za Dr.Dau na tuhuma za udini?

Baada ya kuona orodha ya Wakirsto walivyojazana kwenye mashirika ya umma ndiyo umekuja na haya mawazo.

Mkui acha unafiki hii nchi imejaa udini ingawa unajitia upofu sehemu wakijaa Wakirsto mnasema wasomi sehemu wakiwa Waislam watu mnasema udini.

Tafsiri yenu ya udini uwa ipo kwa Waislam tu siyo kwa Wakirsto.
 
kwani bado issue ya udini wa nnsf inaendelea mmeambiwa leteni ushahidi kama mwenzenu aliyeleta wa Tanesco.Na kuhusu mkulo hakufanya cha maana nssf kama dau
Mkulo inaonekana hakufanya cha maana kwa sababu ni mtu anayejua zile pesa ni za wafanyakazi inabidi zilindwe hivi unajua ni kiasi gani pesa za mfuko huo zilivyotumika vibaya angalia uwekezaji wa machinga complex
 
Mkuu haya mawazo yako mbona hatukuyaona kwenye nyuzi za Dr.Dau na tuhuma za udini?

Baada ya kuona orodha ya Wakirsto walivyojazana kwenye mashirika ya umma ndiyo umekuja na haya mawazo.

Mkui acha unafiki hii nchi imejaa udini ingawa unajitia upofu sehemu wakijaa Wakirsto mnasema wasomi sehemu wakiwa Waislam watu mnasema udini.

Tafsiri yenu ya udini uwa ipo kwa Waislam tu siyo kwa Wakirsto.
nimezaliwa na kukua na waislamu nimesoma nao na nimekuwwa nikishirikiana kwa mambo mbalimbali ya kijamii hata wakati wa mfungo nimekuwa wakinialika kufuturu pamoja na kwamba mimi sijafunga hata siku moja hatujawahi kukaa na kujadili udini siku zote tumekuwa tukijadili mambo mbalimbali ikiwemo siasaa,mpira mambo ya kijamii bila kuingiza udini ila nachoshangaa humu kuna watu wenye akili finyu ambao kwa mtazamo wao hasi wamekuwa wakileta mijadala ya kujenga chuki na kutenganisha utaifa wetu
 
Back
Top Bottom