Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) imeelezwa kupoteza mwelekeo hivyo kuna kazi ya kufanya kuiweka sawa.
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally alitoa kauli hiyo jana Ijumaa Mei 3 katika mkutano na wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari jijini Dodoma.
Dk Bashiru alisema iko haja ya kufanya mageuzi ndani ya jumuiya hiyo ambayo inategemewa kwa kiasi kikubwa na CCM.
Aliwaambia waandishi kuwa kwa sasa CCM kinaandaa vyuo vyake vya Ihemi na Zanzibar ili waanze kuwapika vijana kuwa viongozi wazuri.
Hata hivyo, alisema vijana wanaotakiwa kupikwa katika vyuo hivyo siyo lazima wawe wana CCM tu bali hata na wengine watapikwa ili wakasaidie maeneo yao.
Alisema katika kipindi cha sasa, atatumia watu mbalimbali atakaowakaribisha ili waweze kuzungumza na vijana hao kuwakumbusha misingi na umuhimu wa jumuiya hiyo.
Katibu huyo aliwataka waandishi kutumia kalamu zao kuisaidia CCM kwa kuikosoa inapobidi na kutaja mema pale inapobidi.
Kwa upande mwingine aliwataka waandishi kuandika mema hata kwa vyama vya upinzani kwa sababu hawawezi kujua kwamba chama chochote kinaweza kuwa chama tawala hivyo watoe haki kwa wote bila upendeleo.
Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally alitoa kauli hiyo jana Ijumaa Mei 3 katika mkutano na wahariri na wamiliki wa vyombo vya habari jijini Dodoma.
Dk Bashiru alisema iko haja ya kufanya mageuzi ndani ya jumuiya hiyo ambayo inategemewa kwa kiasi kikubwa na CCM.
Aliwaambia waandishi kuwa kwa sasa CCM kinaandaa vyuo vyake vya Ihemi na Zanzibar ili waanze kuwapika vijana kuwa viongozi wazuri.
Hata hivyo, alisema vijana wanaotakiwa kupikwa katika vyuo hivyo siyo lazima wawe wana CCM tu bali hata na wengine watapikwa ili wakasaidie maeneo yao.
Alisema katika kipindi cha sasa, atatumia watu mbalimbali atakaowakaribisha ili waweze kuzungumza na vijana hao kuwakumbusha misingi na umuhimu wa jumuiya hiyo.
Katibu huyo aliwataka waandishi kutumia kalamu zao kuisaidia CCM kwa kuikosoa inapobidi na kutaja mema pale inapobidi.
Kwa upande mwingine aliwataka waandishi kuandika mema hata kwa vyama vya upinzani kwa sababu hawawezi kujua kwamba chama chochote kinaweza kuwa chama tawala hivyo watoe haki kwa wote bila upendeleo.