Katiba: Nashauri Bunge Lililopo Livunjwe!, Liundwe Bunge Kweli La Katiba Lenye "Peoples Mandate!.

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,468
113,583
Wanabodi,

Demokrasia ni very expensive!, kama tunataka demokrasia ya kweli, hatuwezi kuepuka gharama, kuigharimia ili kuipata!.

Natoa ushauri huu, baada ya kuusoma mchango wa mwana jf mwenzetu huyu, akichangia mjadala fulani humu, amesema hivi na hapa ninanukuu.
Hivyo, ni muhimu process ya kutengeneza ya katiba mpya iongozwe na some normative principles. Vinginevyo, ni sawa na kuwa na sheria ambayo haina policy backing. Hizo normative principles ni pamoja na

  • Process ya kutengeneza katiba lazima ifanywe na bunge la katiba lililochaguliwa na wananchi moja kwa moja.
  • Hili bunge la katiba lazima liwe na unlimted power in the constitutional making. Litakuwa na unlimited power kwa sababu ilitakuwa limechaguliwa directly na wananchi ambao ndiyo wenye mamlaka ya mwisho na nchi yao.
  • Mchakato mzima wa kutengeneza katiba mpya lazima uwe inclusive and participatory.
  • Kufuatia hoja hii, kama ni kweli "all that starts well, ends well!", huu mchakato wa katiba unaoendelea, did not starts well, and its not likely to end well!. Its very unlikely, something that did not start well, to end up well!, hivyo nashauri hili Bunge la Katiba linalokutana Dodoma livunjwe kabla halijaundwa rasmi! (before being constituted!) kwa sababu halina "Mandate" of the People of Tanzania" kufuatia kuundwa bila ushirikishwaji wa wananchi directy but only by proxy!, tuunde Bunge la kweli la Katiba, lenye mandate of the people ndipo tuandike Katiba yetu Mpya!.
Utengenezaji wa Katiba is a process!, yaani ni mchakato unaotakiwa kupitia hatua mbali mbali zifuatazo.
  1. Mkutano wa Kitaifa, "National Convention" ambao ungeshirikisha wajumbe kutoka makundi yote ya jamii (Wajumbe 3,000-5,000), ili kujadili na kuweka "dira" na "dhima" au "misingi" au "tunu" za Taifa, kujua Tanzania tunataka kujenga taifa la namna gani!.
  2. Baada ya kuwa na "Dira" ndipo tunaunda "Tume ya Wataalam" kukusanya maoni ya wananchi kuhusu ni nini wanataka katika katiba yao ili kuitekeleza ile dira na dhima ya Taifa ( Tume ya Warioba). Hii tume inakusanya maoni yote na ya wote, ikiwemo wanaotaka serikali moja, mbili, tatu, uchifu, ufalme, usultani etc.
  3. Baada ya Tume kukamilisha kazi yake, inaundwa tume ndogo ya wataalamu wa katiba, kuyachambua maoni hayo na kutoa rasimu ya katiba.
  4. Unaitishwa uchaguzi wa nchi nzima kwa wananchi kuwachagua wajumbe wa bunge la katiba (constituent assembly), kitendo cha wananchi kuwachagua wajumbe wao wa katiba, kunawapa mandate wabunge hawa kuwawakilisha wananchi kwenye bunge la katiba.
  5. Bunge hili la katiba, ndilo linapitia rasimu, likiwa na "peoples mandate", kuboresha, kuongeza, kupunguza au hata kuiweka kando rasimu nzima na kuunda mpya na katiba hiyo itaanza na maneno "we the people of Tanzania ..."
  6. Hatua ya mwisho ya wananchi kuipigia kura ya ndio au hapana kuipitisha, na hivyo kupata katiba mpya yenye uhalali wa wananchi!.
Kwa mchakato unaoendelea sasa, hakuna mjumbe yoyote mwenye "uhalali" wa wananchi kuwatungia katiba yao!.
Wale wabunge la JMT na Wawakilishi wa BLW, wamegeuka wajumbe wa bunge la katiba by virtue ya ubunge wao kule JMT na BLW ambayo ni mabaraza ya kutunga sheria, lakini sio katiba!. Wananchi waliwachagua kuwa wawakilishi wao katika mabaraza hayo, kwa kuwatuma kwenda kuwatungia sheria!, nani aliyewatuma kwenda kuwatungia katiba?!, au sasa kutunga sheria ndio sawa na kutunga katiba?!.

Kiukweli kabisa kutoka ndani ya moyo wangu, na kiuhalisia, wabunge hao wa Bunge la JMT na wajumbe wa BLW, hawana "peoples mandate" yoyote ya kuwatungia Watanzania katiba!. Uamuzi wa kuwageuza wabunge na wawakilishi kuwa wajumbe wa bunge la katiba, umefanywa kuokoa gharama za kuitisha uchaguzi wa wabunge wa bunge la katiba!, "its a process to save money!, hivyo ni kweli kabisa serikali yetu imeamua kuukubali ule msemo, "if you think education is expensive, try ignorance!", hivyo imeamua "to save money" because democray is expensive!.

Kama process hiyo ingefanyika, kusingelikuwa hata na haja ya wale wateule wa rais amba ni wawakilishi "viini macho" wa wananchi!. Nimewaita "viini macho", kwa sababu logic ya uteuzi wao, toka makundi mbalimbali ya jamii, ni kuhalalisha kuwa "wananchi" wamewakilishwa!, jee ni wananchi gani waliowachagua hata kuwawakilisha?!.

Hoja ya hao wajumbe 201 itatetewa na sheria kuwa "wale wawakilishi wa wananchi, tuliowatuma kwenda kutunga sheria, pia walitunga sheria iliyompa mamlaka rais wa JMT. kuwateulia "wawakilishi" wao kwenda kuwatungia katiba yao, hivyo rais wa JMT amepata hiyo mandate ya kuwachagulia wananchi, wajumbe wa bunge la katiba by proxy iliyotolewa na wawakilishi wao, waliotumwa tuu kutunga sheria na sio katiba, na ni katika utungaji huo wa sheria, wakatunga sheria halali kumuwezesha rais kuwachagulia wawakilishi wao na kutunga katiba ambayo wao hawakutumwa!.

Najua fika hoja yangu hii itakuwa ni ngumu kueleweka na huu uzi utapata wachangia wachache kufuatia si wengi wenye uwezo wa kuzama deep kwenye issues kama hizi!.

Wasalaam.

Pasco.
 
Naunga mkono hoja,kwasasa kinachoendelea Dodoma ni ubatili na wala hakuna katiba ya wananchi. Ngoja mijadala ianze ndio utaona ushabiki wa kisiasa tofauti kabisa na maoni ya wananchi walio wengi.
 
hilo jambo toka mwanzo lilionekana ndio maana sitegemei kuona katiba anayoitaka mtanzania kwanza kitendo cha wabunge wa muungano na baraza la wawakilishi kulazimisha kuemo kwenye bunge la katiba,uteuzi wa makada wa vyama vya siasa kwa kifupi wanasiasa wamechukua sehemi kubwa wakati ilitakiwa bunge la katiba liwakilishe makundi maalumu ya wananchi ndio maana unaona mijadala mingi imejikita kwenye siasa na kuacha mambo mengi muhimu na mbaya zaidi wanatumia kodi zetu
 
nashauri tuachane na mambo ya katiba mpya tufanya marekebisho tu kwenye katiba iliyopo mapema kama alivyo shauri mh.celina kombani
 
Watanzania hatukuwa tayari kuandika katiba, wengi wetu hatukuwa na uelewa wa ndani namna katiba inavyotakiwa kuandikwa; CCM nayo haikuwa na nia ya dhati ya kuandika katiba hii na ndiyo maana hata kwenye ilani yao ya uchaguzi ya 2010 hakukuwapo kipengele chochote cha uandishi wa katiba mpya kwa watanzania - haya yote uliyoanisha hapa ndugu Pasco CCM wanayajua lakini hawakutaka kuyafuata kwa sababu wanazozijua wao.

Sasa mambo yalipofikia hapa hakuna namna tena tunaweza kuachana na mchakato huu - cha msingi ni kuomba kudra za mwenyezi Mungu amwepushe muovu shetani asiingilie mchakto huu ili tupate katiba tunayoitaka, vinginevyo tutakuwa tumetumia resources nyingi sana for nothing.
 
...

Sasa mambo yalipofikia hapa hakuna namna tena tunaweza kuachana na mchakato huu - cha msingi ni kuomba kudra za mwenyezi Mungu amwepushe muovu shetani asiingilie mchakto huu ili tupate katiba tunayoitaka, vinginevyo tutakuwa tumetumia resources nyingi sana for nothing.


Mkuu mchakato tayari tumeshaukabidhi wenyewe kwa Shetani halafu tumwombe Mungu amwepushe Shetani kivipi? Nadhani hata Mungu atatushangaa; na Shetani ndio anauchezea kama mwanasesere anavyotaka.

Tukubali tulishaingia chaka; la msingi tuwe wapole huu upepo upite then huko mbele ya safari ajenda ya Katiba Mpya iwe ni ajenda ya kudumu hadi hapo tutakapopata Katiba Mpya ya ukweli itakayofuata process sahihi zinazotakiwa za ushirikishwaji wanachi kikamilifu.
 
Wanabodi,

Demokrasia ni very expensive!, kama tunataka demokrasia ya kweli, hatuwezi kuepuka gharama, kuigharimia ili kuipata!.

Natoa ushauri huu, baada ya kuusoma mchango wa mwana jf mwenzetu huyu, akichangia mjadala fulani humu, amesema hivi na hapa ninanukuu.

Kufuatia hoja hii, kama ni kweli "all that starts well, ends well!", huu mchakato wa katiba unaoendelea, did not starts well, and its not likely to end well!. Its very unlikely, something that did not start well, to end up well!, hivyo nashauri hili Bunge la Katiba linalokutana Dodoma livunjwe kabla halijaundwa rasmi! (before being constituted!) kwa sababu halina "Mandate" of the People of Tanzania" kufuatia kuundwa bila ushirikishwaji wa wananchi directy but only on proxy!, tuunde Bunge la kweli la Katiba, ndipo tuandike Katiba yetu Mpya!.

Utengenezaji wa Katiba is a process!, yaani ni mchakato unaotakiwa kupitia hatua mbali mbali zifuatazo.
  1. Mkutano wa Kitaifa, "National Convention" ambao ungeshirikisha wajumbe kutoka makundi yote ya jamii (Wajumbe 3,000-5,000), ili kujadili na kuweka "dira" na "dhima" au "misingi" au "tunu" za Taifa, kujua Tanzania tunataka kujenga taifa la namna gani!.
  2. Baada ya kuwa na "Dira" ndipo tunaunda "Tume ya Wataalam" kukusanya maoni ya wananchi kuhusu ni nini wanataka katika katiba yao ili kuitekeleza ile dira na dhima ya Taifa ( Tume ya Warioba). Hii tume inakusanya maoni yote na ya wote, ikiwemo wanaotaka serikali moja, mbili, tatu, uchifu, ufalme, usultani etc.
  3. Baada ya Tume kukamilisha kazi yake, inaundwa tume ndogo ya wataalamu wa katiba, kuyachambua maoni hayo na kutoa rasimu ya katiba.
  4. Unaitishwa uchaguzi wa nchi nzima kwa wananchi kuwachagua wajumbe wa bunge la katiba (constituent assembly), kitendo cha wananchi kuwachagua wajumbe wao wa katiba, kunawapa mandate wabunge hawa kuwawakilisha wananchi kwenye bunge la katiba.
  5. Bunge hili la katiba, ndilo linapitia rasimu, likiwa na "peoples mandate", kuboresha, kuongeza, kupunguza au hata kuiweka kando rasimu nzima na kuunda mpya na katiba hiyo itaanza na maneno "we the people of Tanzania ..."
  6. Hatua ya mwisho ya wananchi kuipigia kura ya ndio au hapana kuipitisha, na hivyo kupata katiba mpya yenye uhalali wa wananchi!.
Kwa mchakato unaendelea sasa, hakuna mjumbe yoyote mwenye "uhalali" wa wananchi kuwatungia katiba yao!.
Wale wabunge la JMT na Wawakilishi wa BLW, wamegeuka wajumbe wa bunge la katiba by virtue ya ubunge wao kule JMT na BLW ambayo ni mabaraza ya kutunga sheria, lakini sio katiba!. Wananchi waliwachagua kuwa wawakilishi wao katika mabaraza hayo, kwa kuwatuma kwenda kuwatungia sheria!, nani aliyewatuma kwenda kuwatungia katiba?!, au sasa kutunga sheria ndio sawa na kutunga katiba?!, kiukweli kabisa kiuhalisia, wabunge hao wa Bunge la JMT na wajumbe wa BLW, hawana "peoples mandate" yoyote ya kuwatungia Watanzania katiba!. Uamuzi wa kuwageuza wabunge na wawakilishi kuwa wajumbe wa bunge la katiba, umefanywa kuokoa gharama za kuitisha uchaguzi wa wabunge wa bunge la katiba!, "its a process to save money!, hivyo ni kweli kabisa serikali yetu imeamua kuukubali ule msemo, "if you think education is expensive, try ignorance!", hivyo imeamua "to save money" because democray is expensive!.

Kama process hiyo ingefanyika, kusingelikuwa hata na haja ya wale wateule wa rais amba ni wawakilishi "viini macho" wa wananchi!. Nimewaita "viini macho", kwa sababu logic ya uteuzi wao, toka makundi mbalimbali ya jamii, ni kuhalalisha kuwa "wananchi" wamewakilishwa!, jee ni wananchi gani waliowachagua hata kuwawakilisha?!.

Hoja ya hao wajumbe 201 itatetewa na sheria kuwa "wale wawakilishi wa wananchi, tuliowatuma kwenda kutunga sheria, pia walitunga sheria iliyompa mamlaka rais wa JMT. kuwateulia "wawakilishi" wao kwenda kuwatungia katiba yao, hivyo rais wa JMT amepata hiyo mandate ya kuwachagulia wananchi, wajumbe wa bunge la katiba by proxy iliyotolewa na wawakilishi wao, waliotumwa tuu kutunga sheria na sio katiba, na ni katika utungaji huo wa sheria, wakatunga sheria halali kumuwezesha rais kuwachagulia wawakilishi wao na kutunga katiba ambayo wao hawakutumwa!.

Najua fika hoja yangu hii itakuwa ni ngumu kueleweka na huu uzi utapata wachangia wachache kufuatia si wengi wenye uwezo wa kuzama deep kwenye issues kama hizi!.

Wasalaam.

Pasco.

Ndugu Pasco,

Nakubaliana na wewe kuhusu "Uharamu" wa bunge hili la katiba ambalo pamoja na mbinu za kufukia mambo kufanya ionekane lina uwakilishi wa wananchi. Ni kweli halina mandate ya wananchi wa nchi hii. Pia ni wazi mchakato wa kupatikana wajumbe/wabunge wa bunge hilo la katiba umekuwa na kasoro nyingi, hasa kubwa ikiwa ni bunge la kawaida (la kutunga sheria) kuamua bila ridhaa ya wananchi, kwamba mamlaka ya kuteua wajumbe wa bunge la katiba awe nayo Rais. Rais ambaye on the other hand ni zao la mfumo wa mrengo flani wa siasa. mmoja kati ya pande zenye kutaka kunufaika na katiba itakayoundwa! Kwa busara za kawaida tu kama kweli Wabunge wangejali au kama Rais angejali wote kwa pamoja walitakiwa ku-declare conflict of interest na kuliachia hilo jukumu.

Pamoja na kuwa katiba siyo kitu ambacho tunaweza kukitengeneza kila mwaka, ni wazi hii ya sasa itakuwa na kasoro na itawalazimu Wananchi kudai katiba nyingine hata kabla ya miaka mitano kwisha. Kwa hiyo kama tungekubaliana mi nadhani mchakato huu ni batili kikatiba, kisheria na kidemokrasia. Hivyo unapaswa kusitishwa kabla haujaleta hasara zisizo za msingi kwa lengo ambalo halitatimia.

Vinginevyo tutalazimika kufungua shauri mahakamani, hapo baadaye, kupinga uhalali wa katiba, based on kasoro ya utaratibu uliozalisha katiba hiyo na walioijadili na kuipa baraka(kwa maana ya wajumbe wa bunge la katiba na mandate yao)

CC: John Mnyika
user-offline.png
 
Ndugu Pasco,

Nakubaliana na wewe kuhusu "Uharamu" wa bunge hili la katiba ambalo pamoja na mbinu za kufukia mambo kufanya ionekane lina uwakilishi wa wananchi ni kweli halina mandate ya wananchi wa nchi hii. Pia ni wazi mchakato wa kupatikana wajumbe/wabunge wa bunge hilo la katiba umekuwa na kasoro nyingi, hasa kubwa ikiwa ni bunge la kawaida (la kutunga sheria) kuamua bila ridhaa ya wananchi, kwamba mamlaka ya kuteua wajumbe wa bunge la katiba awe nayo Rais. Rais ambaye on the other hand ni zao la mfumo wa mrengo flani wa siasa. mmoja kati ya pande zenye kutaka kunufaika na katiba itakayoundwa! Kwa busara za kawaida tu kama kweli Wabunge wangejali au kama Rais angejali wote kwa pamoja walitakiwa ku-declare conflict of interest na kuliachia hilo jukumu.

Pamoja na kuwa katiba siyo kitu amabcho tunaweza kukitengeneza kila mwaka, ni wazi hii ya sasa itakuwa na kasoro na itawalazimu Wananchi kudai katiba nyingine hata kabla ya miaka mitano kwisha. Kwa hiyo kama tungekubaliana mi nadhani mchakato huu ni batili kikatiba, kisheria na kidemokrasia. Hivyo unapaswa kusitishwa kabla haujaleta hasara zisizo za msingi kwa lengo ambalo halitatimia.

Vinginevyo tutalazimika kufungua shauri mahakamani, hapo baadaye, kupinga uhalali wa katiba, based on kasoro ya utaratibu uliozalisha katiba hiyo na walioijadili na kuipa baraka(kwa maana ya wajumbe wa bunge la katiba na mandate yao)

CC: John Mnyika
user-offline.png

Mtikila alishasema atafanya hivyo, sijui asasi zingine zina maoni gani; nadhani anasoma tu mchezo na kuaandaa ushahidi usio na shaka. Tutasikia mengi kupitia huu mchakato.
 
Kama sikosei mleta MADA anataka kuona uwepo wa Bunge la Wananchi,Hiyo ni nzuri sana na inastahili kuungwa mkono.Hii Katiba inayotengenezwa ni Wananchi hivyo iliku vyema Wananchi tupewe kipaumbele katika hatua zote za ujenzi wa Katiba mpya.Sisi ndiyo WAAJIRI na Serikali ni WAAJIRIWA ni KATIBA mpya ni MKATABA mpya tunaotaka kuutengeneza upya ambapo hawa WAAJIRIWA wetu yaani Serikali wanapaswa kula kiapo cha kutii yote yaliyomo ndani ya hiyo Katiba.Sasa inashangaza kuwaona hawa WAAJIRIWA wakitaka kuweka mawazo yao kwenye huu MKATABA ambao kimsingi ni wa Wananchi.Naungana na Pasco kuwa Bunge la Katiba linapaswa kuwa mwonekano wa kiuwakilishi wa Wananchi.Ila nina mashaka na SINCERITY ya Bw. Pasco kuhusu namna tulivyofika hapa kwenye mchakato huu.Ni Katiba mbovu ya zamani ndiyo inayotumika kama mwongozo wa kuelekea kuipata Katiba mpya.Katiba ya zamani imempa Rais wa nchi madaraka makubwa juu ya kila kitu na JK ndiyo anautumia mwanya huo sasa kutengeneza Katiba itakayolinda maslahi ya Chama chake kisiasa.
 
Kama sikosei mleta MADA anataka kuona uwepo wa Bunge la Wananchi,Hiyo ni nzuri sana na inastahili kuungwa mkono.Hii Katiba inayotengenezwa ni Wananchi hivyo iliku vyema Wananchi tupewe kipaumbele katika hatua zote za ujenzi wa Katiba mpya.Sisi ndiyo WAAJIRI na Serikali ni WAAJIRIWA ni KATIBA mpya ni MKATABA mpya tunaotaka kuutengeneza upya ambapo hawa WAAJIRIWA wetu yaani Serikali wanapaswa kula kiapo cha kutii yote yaliyomo ndani ya hiyo Katiba.Sasa inashangaza kuwaona hawa WAAJIRIWA wakitaka kuweka mawazo yao kwenye huu MKATABA ambao kimsingi ni wa Wananchi.Naungana na Pasco kuwa Bunge la Katiba linapaswa kuwa mwonekano wa kiuwakilishi wa Wananchi.Ila nina mashaka na SINCERITY ya Bw. Pasco kuhusu namna tulivyofika hapa kwenye mchakato huu.Ni Katiba mbovu ya zamani ndiyo inayotumika kama mwongozo wa kuelekea kuipata Katiba mpya.Katiba ya zamani imempa Rais wa nchi madaraka makubwa juu ya kila kitu na JK ndiyo anautumia mwanya huo sasa kutengeneza Katiba itakayolinda maslahi ya Chama chake kisiasa.

kwa nini unafikiri serikali moja sio nzuri kwa tanzania
 
walio chaguliwa na raisi mliwapeleka wenyewe, sasa hivi mnalilia

Kababu bana!,

It was very wrong kwa waliochaguliwa kupelekwa kwa rais. Katika nchi inayojali demokrasia haikuwa kazi ya rais kupendekeza nani anatakiwa na nani asiwepo kwenye bunge la katiba. ilikuwa ni kazi ya wananchi kujichagulia wawakilishi wao moja kwa moja na wasiulizwe kwa nini.

Pia imekuwa kawaida hapa nchini, hasa kutokana na ukosefu wa elimu ya uraia kwa wananchi na hata viongozi wao, wananchi wamekuwa wakiburuzwa tu. Kwa sababu viongozi wanadhani wana haki ya kuwaamulia wananchi hatma yao au labda nchi hii ni yao hivyo wao wantakiwa kuwasemea wananchi kila kitu.

Sasa kwa kuwa wale jamaa walichaguliwa na wananchi, kisha wakapelekwa kwa rais (of which siyo sahihi kabisa) haimaanishi wananchi wasilalamike hata baada ya kuona athari za uchaguzi walioufanya! Siyo dhambi mtu kukiri "I was wrong then and I want it right now" Naamini ni walioamka na wanaojitambua ndiyo wanaopiga kelele sasa. Sitaki kujua kwa nini hawakuamka jana. nnachojua ni kuwa jana walikuwa usingizini lakini leo wameamka na wanataka kurekebisha.And that, my dear, is what people who wants to develop do always do.
 
[Pasco] Na mimi nitupie like, naona kila anayechangia unamtupia, na mm bect.
Wee Bei, baada tuu ya kusoma hii posti yako, nikarudi nyuma kutafuta mahali kwa mcvhangiaji ambaye nilisahau kumgomgea!, nilichoona nikachoka!, ikanibidi nirudi hapa nikupe thanks!.
Pasco
 
Mkuu Pasco ninaunga mkono hii hoja yako kwa asilimia 100.. Toka ccm walipopora ajenda ya katiba mpya (ambayo haikuwapo kwenye ilani yao) nilishajiaminisha kwamba hakutakuwa na katiba mpya itakayotokana na wananchi... Bahati mbaya kabisa suala hilo likawa ni la wanasiasa na mivutano yote ikawa ni ya kisiasa.. Mchakato wa utengenezaji wa katiba ya wananchi unapaswa kuchukua sio chini ya miaka mitano mpaka kupata katiba ilioridhiwa na wananchi wengi..
 
Last edited by a moderator:
Tulipokwenda kupambana Idd Amini Dadaa, Taifa lilisimamia katika kauli hii.".....Nia tunayo, uwezo tunaona, sababu tunayo..." hivyo tulisonga mbele na kushinda vita...(Umoja ulitawala fikra, matendo na mipango stahiki)

Siyo sababu yangu kuwakumbusha vita vya Kagera lah hasha, bali nataka kujenga hoja moja ndogo katika hili suala la katiba.
  1. Najiuliza...! Hivi nia ya dhati juu ya matakwa ya katiba mpya tulikuwa nayo?
    • Hapa kwenye nia ndipo ninapopatilia mashaka. Kuhusu sababu na uwezo sina shida navyo maana najua sababu za kutaka Katiba mpya tunazo, uwezo wa kuendesha zoezi tunaoa, bali nia ya dhati.....!??? Sina uhakika

Katika hili, nawiwa kuamini kwamba, kukosekana kwa nia ya dhati katika kutengeneza katiba mpya ndiko huko kuliko tufikisha hapa tulipo na ndiko hukohuko kutakapo tupatia mwisho mbaya pengine mwisho tusiopenda utokee.

Naomba niwakumbushe jambo moja la msingi



  1. [*=1]Kwa nini tume ya katiba iliamua kutumia Qualitative method na si Quantitaive method, right at the biggining? Je, hakukuwa na wapi waliopinga hili?
    [*=1]Maoni yaliyopo kwenye rasimu mpya ya katika kweli ndiyo maoni na matakwa ya wananchi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania?
    [*=1]Sasa wamepatikana wajumbe wa Bunge la katiba, Je ni wawakilishi wa watu gani kuhusia na mtazania yule kwa kule tambuka reli?
    [*=1]Political frames (ideologies, stands, willingness, Propaganda etc) zina nguvu kiasi gani ukilinganisha na wawakilishi binafsi au wanaharakati katika hili bunge la katiba?
Haya ni baadhi tu ya mambo ambayo hatakiwi mtu kutumia nguvu kuya-adress. Ni dhahiri kuwa tulishakosea toka mwanzoni. Now more are still on the way to come nani alaumiwe?
 
Well said Pasco,
Kwenye forum ya Katiba mpya mwaka Jana niliweka Uzi wenye kichwa cha habari KATIBA MPYA ISIPOPATIKANA 2014 NINI KIFANYIKE?. Namshukuru Mungu kuona Watanzania wengi sasa wameona 'Uharamu' wa mchakato huu. Nakumbuka wakati wa CSO's kujadili sheria ya mabadiliko ya katiba kule bungeni dodoma tulipigwa mabomu tukidaiwa kuwa tulikwenda wengi wakati waliokuwa wameingia ndani walikuwa saba tu tena wasiojulikana na Jukwaa la Katiba Tanzania hadi pale Katibu wa bunge alipoingilia kati japokuwa baadhi ya wanafunzi wa UDOM walizuiwa kuingia.

Kimsingi mchakato huu hauna Public legitimacy.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom