Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Habari ndugu zangu wapeendwa, leo sina mengi sana ya kuandika hapa kama ilivyo kawaida yangu. kwa kifupi sana nataka kujadili kuhusu madai ya katiba, si vibaya lakini tunapaswa kujiuliza kwanza ni nini tunachokidai katika katiba hiyo.
Nasema hivyo nikiwa na maana ya kuwa, mabadiliko tunayoyadai ni haki ya watanzania wote lakini ni wangapi leo hii aambao wamewahi kuiona na kuisoma katiba hiyo zaidi ya kuisikia katika midomo ya wanasiasa pekee.
Kwa nini kabla ya kudai mabadiliko hayo nguvu zetu tusizielekeze katika madai ya kuchapishwa katiba hiyo ili iwe wazi kwa watanzania wote waisome ili wachangie mawazo yao katika vipengele ambavyo watakuwa hawajalizika navyo ili mabadiliko hayo yachangiwe na watanzania wote.
Tunajua kuwa katiba hiyo inafichwa na kuwa ni siri kubwa kutokana na mapungufu yake. Lakini imefikia wakati sasaa iwekwe hadharani tena iandikwe kiswahili kila anayejua kusoma aisome na kuielewa ndipo tuanze kudai mabadiliko hayo. Tofauti na hivyo tutakuwa tunadai mabadiliko ya kitu wasichokijua mamilioni ya watanzania.
Nasema hivyo nikiwa na maana ya kuwa, mabadiliko tunayoyadai ni haki ya watanzania wote lakini ni wangapi leo hii aambao wamewahi kuiona na kuisoma katiba hiyo zaidi ya kuisikia katika midomo ya wanasiasa pekee.
Kwa nini kabla ya kudai mabadiliko hayo nguvu zetu tusizielekeze katika madai ya kuchapishwa katiba hiyo ili iwe wazi kwa watanzania wote waisome ili wachangie mawazo yao katika vipengele ambavyo watakuwa hawajalizika navyo ili mabadiliko hayo yachangiwe na watanzania wote.
Tunajua kuwa katiba hiyo inafichwa na kuwa ni siri kubwa kutokana na mapungufu yake. Lakini imefikia wakati sasaa iwekwe hadharani tena iandikwe kiswahili kila anayejua kusoma aisome na kuielewa ndipo tuanze kudai mabadiliko hayo. Tofauti na hivyo tutakuwa tunadai mabadiliko ya kitu wasichokijua mamilioni ya watanzania.