Ndugu watanzania wanaofuatilia utoaji wa haki kwa raia watakubuka jinsi ndugu zetu wa Mbalali waliotaka kumshtaki mbunge wao Kwa ubadhiirifu wa hela zao walidhokwama kwa sababu serikali haikutaka kuendesha hiyo kesi ili kumlinda mbunge wa wakati huo. walijaribu kumtumia private prosecutor wakakjwama kwa sababu katiba hailruhusu. Ni watu wengi sana wanapoteza haki zao kwa sababu ya utaratibu uliopo wa kumfungulia mashtaka mkosaji anayelindwa na serikali. Hivyo napendekeza tusimame kidete kuhakikisha anakuwepo private prosecutor. Pia lazima kiwepo chombo kingine kinachojitegemea kuchunguza makosa yanayofanya na polisi na majeshi mengine. Jeshi la aina yoyote ile lazima lishtakiwe kama likikosea ndipo demokrasia ya kweli itakuwepo. Nawasilisha kwa majadiliano.