Katiba Mpya: Clouds FM Wachochezi!


Waandae tu disco zao haya mambo ya siasa hawayawezi, wamwulize mwenzao yule wa kasha sasa hivi anahenyeka na ICC
 

Waandae tu disco zao haya mambo ya siasa hawayawezi, wamwulize mwenzao yule wa kenya sasa hivi anahenyeka na ICC
 
Kwa kusema hivyo tayari anatakiwa kua mtuhumiwa namba moja.

Tatizo hivi vyeo vya ukuu wa wilaya na mikoa unawapumbaza sana wanahabari walio wengi hadi kusababisha msamiati wa ukanjanja uzidi kushamili bila kusahau bahasha za kaki.
 
Huyo pj, akae akijua kuwa the hague hakuna upendeleo na tutamsikia analialia oo mie sikusema! Amuulize Arap Sang wa kenya mwanahabari kama yeye leo anashinda huko badala ya kukaa na familia yake.tumewachoka hao mizoga
 
Amuulize Arap Sang wa kenya mwanahabari kama yeye leo anashinda huko badala ya kukaa na familia yake.
Una maanisha anashinda mamtoni, anakwea pipa kama anapanda daladala za mwenge posta vile.
 

Ni kweli mkuu, Lakini PJ anapata nguvu zaidi kutokana misimamo ya uongozi wa Clouds ambao wameamua kukamata fursa kupitia CCM.Hizi network zitakufa very soon na tutabaki na majeruhi wengi watakaokosa hata pa kuficha nyuso zao.
 
Kuna watu hawana haibu hapa duniani na miongoni mwao ni wale wanaojiita 'ccm damu' ambao hii radio nayo ni kitengo chao cha propaganda.
Nia yao ni kuwa kuliko mawazo ya wananchi walio wengi kutekelezwa ni bora sote tukose, na kinara wao keshasema kuwa hii kitu haitawezekana labda mpaka aondoke madarakani! Tambua hili
 
Nilishangaa , halafu hata hawajamuhoji Lipumba akasema sababu za kujitoa wao wanamnaga tu . hawa jamaa ni Mungiki kabisa
 
Kumbe amewahi kujitosa kugombea ubunge....!!
Basi ndio maana huwa anaongea vile redioni.....!
 
Una maanisha anashinda mamtoni, anakwea pipa kama anapanda daladala za mwenge posta vile.

Ee si unasikia kaka kesi ikisikilizwa leo wanaambiwa baada ya siku 7 mwenzake anarudi yeye anabaki kule.
 
Naamin kama TCRA wapo makin watawahoji,moja ya mistari ya PJ ile inayosema kuna njama za kuifanya tanzania isitawalike baada ya kuvuruga mchakato wa katiba,,,,kumepangwa kufanyika machafuko pande zote za nchi hii,binafsi nilishtuka

Hao achaneni nao bali muda muafaka ukifika watakuwa Historia na kuwajibika kwa matendo yao binafsi na sio Radio Clouds
 
Ni sera ya hii Radio kupumbaza watanzania na si ajabu kusikia habari zisizo na weledi ili mradi tu ziwe upande wa magamba!Hata mimi naamini iko siku watalazimika kuwajibika kwa maneno yao!

Sent from my BlackBerry 9220 using JamiiForums
 
Watafanya nn jamani na wanataka kuishi vizuri mjin? Yani hao jamaa kila kitu wanajua wao na wanacho amini wao ndo wanataka watu wote tukikubali, kwao wao jd ni mbaya basi na ss wote tukubali hvyo
 
 
Jifunzeni kusikia hoja mbadala wa zile mnazopenda kusikia. Sio kila mtu aliye na mawazo tofauti na yale mnayoyapenda, hana akili.
Hoja ipi inayopingwa hapa. Watu wanajadili usahihi wa taarifa na jinsi ilivyowasilishwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…