Katiba imekaa vizuri sana

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,951
Nimeipitia katiba kipengere kwa kipengere.
Hakika imekaa vizuri sana. nimekuwa nikijiuliza wale wanaoipinga wanapinga kwa hoja zipi!!?
Ailimia kubwa mambo yaliyopendekezwa na tume ya Warioba yamo.
Eti kwa sababu tu kwamba serikali tatu haipo.
Asilimia kubwa ya watu wanaisoma kwa mrengo wa kuipinga. Hawako na free mind.

Kuna mambo mazuri sana mengi. Mfano:


Na kuna mambo mengi sana nitaendelea kuya toa.
 
Raisi kapewa mamlaka makubwa yakuteua mpaka kuku sasa ndo kukaa vzur uko? Tume huru ya uchaguzi haiwez kuteuliwa na raisi isome tena vzur
 
SURA YA TANO
HAKI ZA BINADAMU, WAJIBU WA RAIA, JAMII NA MAMLAKA ZA NCHI

Code:
Hii inazungumzia haki za Binadamu na Wajibu wa raia.

Pia tena inatoa mipaka ya haki za binadamu hebu tujaribu kuisoma vizuri
 

Usilete ushabik kwa mfumo uliopo wa serikali mbili hayo mambo hayawez kutekelezeka labda arudi masia" kwa utitiri wa wabunge 360 na makamu wa raisi watatu kwa budget ipi watz ebu zindukeni kutoka ucngizini hizi sanaa tu
 
Angalia hapa tena.

 
wewe nenda taratibu soma Ibara ya 20 (2) tatizo lenu mnakurupuka sana! hamsomi as a whole!!

Hii katiba haifai kabisa.
 
Usilete ushabik kwa mfumo uliopo wa serikali mbili hayo mambo hayawez kutekelezeka labda arudi masia" kwa utitiri wa wabunge 360 na makamu wa raisi watatu kwa budget ipi watz ebu zindukeni kutoka ucngizini hizi sanaa tu

1. Makamu wa kwanza ndiye mgombea mwenza wa rais
2. Makamu wa pili ni Rais wa Zanzibar
3. Makamu wa tatu ni waziri mkuu.

Unaielewa mantiki yake?
 
wewe nenda taratibu soma Ibara ya 20 (2) tatizo lenu mnakurupuka sana! hamsomi as a whole!!

Hii katiba haifai kabisa.

Nakuomba uisome sura nzima inaongelea nini
SURA YA PILI
MALENGO MUHIMU, MISINGI YA MWELEKEO WA
SHUGHULI ZA SERIKALI NA SERA ZA TAIFA
 
Taifa kuwa na Lengo

 
... Toa Hiyo Toilet Pepa Yenu.! Inanuka
Unatakiwa uisome na utoe comment sio kuleta porojo mimi hapa natoa yaliyomo kwenye katiba wewe unaleta bra bra tu.
 
... Tanzania Kweli Wapumbavu Wengi Sana, Kaz Ipo
 
Unatakiwa uisome na utoe comment sio kuleta porojo mimi hapa natoa yaliyomo kwenye katiba wewe unaleta bra bra tu.

.... Na Wala Hakuna Uzuri Wowote Hapo, Uvundo Tu. Mfano, Ardhi Ni Suala La Muungano? Mbona Lipo Kwnye Katiba Ya Tanzania.
 
sera ya mambo ya nje
 
Hayo ndiyo uliyoaona mazuri. Je,
- Kwako kutomwajibisha mbunge hata asipoonekana jimboni miaka 2 ni sawa?
- Kwako mbunge kutokuwa na kikomo cha ubunge (kama ubunge wa kifalme) ni sawa?
- Kwako mbunge kuwa waziri na kushindwa kutitimiza majukumu ya kibunge ni sawa?
- Kwako spika kuwa mbunge ni sawa?
- Kwako,uwajibikaji,uwazi na uadilifu kuondolewa kama tunu za Taifa ni sawa?
Katiba inayopendekezwa kwa kuondoa haya inapalilia ufisadi na uhujumu wa maliasili ya nchi. Au niambie kwa nini yameondolewa maoni yetu hayo? Kungekuwa na ubaya gani yangebaki kwenye katiba? Jibu lake ni fupi, YANALINDA MAFISADI.

Lazima ujue pia kwamba ardhi siyo suala la muungano,hivyo unapoweka katika katiba ya muungano suala lisilo la muungano,ni nani atakayesimamia utekelezaji wake? Hili ni changa la macho.Unapewa haki katika mkono mmoja wakati mkono mwingine unanyanganya haki hiyo. Hakika sura ya ardhi ni mapambo tu ya kupamba katika mpya.Funguka mwananchi.
 
.... Na Wala Hakuna Uzuri Wowote Hapo, Uvundo Tu. Mfano, Ardhi Ni Suala La Muungano? Mbona Lipo Kwnye Katiba Ya Tanzania.
Hapo ndio unapo shindwa kuelewa mantiki ya katiba hii. Ngoja nikukumbushe kitu kimoja tu.
Zanzibar itajishughulisha na mambo yasiyo ya Muungano yanayo husu zanzibar. Lakini JMT itajihusisha na mambo yote ya Tanzania bara na mambo yote ya Muungano. Get the point?
 
.... Wabunge 380?? Makamu Wa Rais Watatu? Arafu Eti Serikali Za Mitaa Na Zenyewe Zimewekwa Kwny Muungano? Hahahaha, Hii Katiba Ya Ccm Ni Vioja.!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…