Kati ya hawa yupi sahihi kumuoa

Kati ya hawa yupi sahihi kumuoa

Nduka Original

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2010
Posts
1,012
Reaction score
817
Kati ya mwanamke msomi na asiye msomi yupi sahihi kumuoa.

Kwakweli mimi naona ni heri mwanamke asiyesoma hawa waliosoma ni wasumbufu sana na wanajifanya wanajuwa kila kitu na ndio maana hata ndoa zao hazidumu
 
Kila binadamu na mawazo yake, wengine tunapenda wanawake walio soma.
 
wote ni wanawake na wate wanahiji kuwa na waume zao hakuna aliye bora zaidi ya mwingine
 
inategemea na moyo wako umeangukia wapi nadhani,ukimwangukia msomi oa na ukimwangukia asiyesoma oa huyo huyo pia,coz ndoa au kuoa na kuolewa is all about love na sio usomi na mengineyo.
 
^^
Sasa!! Tayari umechagua upande wako..kuna haja ya ushauri kweli?
^^
 
kuoa hakuangalii elimu au kutokuwa na elimu bali maelewano kati yenu mlio amua kuoana. unaweza oa alie na elimu akawa unavyosema msumbufu na pasua kichwa lakini ukaoa aliesoma mambo yakanyooka sana tu. ila ukaoa ambaye hajasoma likawa janga au ikawa neema hadi wewe mwenyewe ukashangaaa . kiujumla mwanamke wa kuoa ni yule mnayesikilizana mnaweza panga kitu kikatokea vinginevo you are finished.
 
Kua ni sawa nakutia mkono gizani,huyo ulomtaka wewe asie soma anaweza akawa na majanga na akakukondesha,
na ukampa alie soma ukasema najuta kuchukua yule asiesoma,chamsingi nikuomba mungu akupe mke mwenye kheir na wewe na mue na masikizano lakini usimsemehe alosoma wala asiesoma.........
 
Kati ya mwanamke msomi na asiye msomi yupi sahihi kumuoa.

Kwakweli mimi naona ni heri mwanamke asiyesoma hawa waliosoma ni wasumbufu sana na wanajifanya wanajuwa kila kitu na ndio maana hata ndoa zao hazidumu

kaoe ao wasio na elimu sisi sio levo yako.
 
Hili swali kamuulize member mwenzetu wa JF anaitwa Da sophy
hahahaaaa hii kali.Huyu si ndo yule aloleta mada kwamba alosoma na sosoma chumvini sawa!
Kwa faida ya mleta mada unaweza ukaoa kwa muda ukatoa probation period of 6 months anza na asiyesoma umalizie aliyesoma then u can conclude yupi bora.
 
kila kitu na wakati wake hivyo msomi na asiye msomi inategemea na umuhimu wake unavyouchukulia wewe... japo kwangu elimu si kigezo sana cha hukumu katika ndoa
 
Kati ya mwanamke msomi na asiye msomi yupi sahihi kumuoa.

Kwakweli mimi naona ni heri mwanamke asiyesoma hawa waliosoma ni wasumbufu sana na wanajifanya wanajuwa kila kitu na ndio maana hata ndoa zao hazidumu

Wewe mwenyewe umesoma? nafikiri hapo utajua uende wapi na wapi usiende.
 
Kati ya mwanamke msomi na asiye msomi yupi sahihi kumuoa.

Kwakweli mimi naona ni heri mwanamke asiyesoma hawa waliosoma ni wasumbufu sana na wanajifanya wanajuwa kila kitu na ndio maana hata ndoa zao hazidumu

baba hajasoma mama hajasoma watoto watasoma kweli????? jamani mnapofikiria maisha yenu jaribu kufikiria na watoto wenu. kama wewe hujasoma jaribu kutafuta aliyesoma angalau kuwe na mawazo tofauti ndani ya nyumba
 
Back
Top Bottom