Katazo la mashabiki kutovaa jezi za Al Ahly na Mamelodi haliwezi kufaulu

Kambi ya Fisi

JF-Expert Member
Feb 3, 2018
13,520
22,015
Wekundu.PNG

Kuna jambo ninaliona hapa kuhusu marufuku ya waziri Ndumbaro itakavyoshindwa kufaulu ni hivi.

Ikiwa watakao kagua passport za mashabiki wenye jezi sio askari wa uhamiaji bali ni FFU wale wanaoendaga uwanjani kutazama mechi na si kuzuia fujo hawataweza kuwabaini wazee wa passport feki, watadanganywa kirahisi mno kwa kuoneshwa passport feki zilizotengenezwa na Wataalam wa passport feki, hapo mashabiki wa bongo wataingia kiulaini tu Kwa kutumia hizo passport feki huku wakiwa na jezi pendwa kwao.

Hakuna ofisi ya uhamiaji pale kwa Mkapa hivyo tutegemee jangu wetu wakichukua jukumu lisilo lao la kukagua passport na hapo ndipo wataaibika katika kuhojiana na mashabiki maana njagu wetu wengi wao ung'eng'e haupandi.

Ni wazi waziri hawezi kushindana ama kuzimisha morari ya mashabiki Kwa kuwapangia cha kuvaa pale kwa Mkapa.

Ni heri aachane hiyo marufuku kabla hajaaibika kitaifa na kimataifa.
 
Mi naona Wana SIASA wangekaa mbali na mpira mbona kama ni misifa ya kijinga wanapewa na wasanii wao kila siku???
Watu tuliamua kushabikia soka ili angalia tupate furaha tena wameleta huku UPUMBAVU wao....

Mi furaha yangu n kuitania Simba na Simba furaha yake n kunitania ndo mpira huo... Tukiwa kitu kimoja hakutakua na ushabiki tena ..

Mi naona wangekuatana huko wasiafiane ujinga wao Ila kwenye mpira wake mbali
 
Wabaki na siasa zao watuachie mpira wetu,, baba watatu kashanunua jezi yake na yangu hivi huyu ndumbaro anaweza kunilelea timu ya nyumbani kwangu? Au analopokwoka kwa kushiba posho. Mama samia nae amtengue liwe somo kwa wengine sie hawatufatillii watuache kama tulivyowaaacha.
 
Cha ajabu nimemsikia anajisifu ana kadi ya uanachama ya timu ya Liverpool. Nchi hii tuna viongozi wa ajabu sana aisee.
 
Halafu mpaka dakika hii mamlaka zilizomteua huyo waziri hazijaona haja ya kufuta hiyo kauli.

Leo itaanza kwenye jezi kesho itahamia katika nguo zote kwa ujumla.

Michezo na kiki za kisiasa na vitu viwili tofauti. Waziri anataka political mileage kwa vitu vya kipumbavu kabisa.

Uzalendo haulazimishwi.
 
Simba na yanga sio timu za taifa hata aina ya wachezaji wanaocheza wengi wao ni wahaini. Mfano mchezaji wa kitanzania angekuwa anachezea mamelody au ah ahly asingeruhusiwa kucheza?
 
Kama ni kweli katoa hiyo kauli basi huyo waziri ni majawapo ya watawala wajinga tulionao madarakani
 
Back
Top Bottom