The Boss
JF-Expert Member
- Aug 18, 2009
- 49,320
- 117,613
Ukiwasikiliza watu wanaomsifia Mwalimu Nyerere kwa uongozi mzuri most of times wengi wao huwa 'wanambambikia' Rashidi Kawawa, mapungufu na makosa yote ya utawala wa Nyerere. Ni kama vile Kawawa ndo anestahili kubebeshwa kila baya la utawala wa Nyerere na mazuri yote ni ya Nyerere, licha ya Nyerere mwenyewe kusema mara kwa mara Hakuna 'mtu mwaminifu' aliewahi kukutana nae kama Kawawa, na mara zote mahusiano yao yalikuwa kama ya Mwalimu na mwanafunzi.
Kawawa alipewa tu maagizo na kuyatekeleza kwa uaminifu mkubwa. Kawawa aliwahi hata kuachiwa nchi, akawa Waziri mkuu wa Tanganyika huru na bado 'akamrudishia' Nyerere madaraka ya ukuu wa nchi. Lakini hata kwa waasisi ni nadra kutajwa...Utasikia Nyerere na Karume. kila lilioenda kombo wakati wa Nyerere lawama alipewa Kawawa.
Rais mpya Magufuli keshajipatia 'mashabiki' wenye jazba na wasiotaka hata akosolewe, ni kama wengine ni kama washaanza mchakato wa kumfanya Magufuli awe 'mtakatifu' mpya baada ya Nyerere, wakati ana siku 20 tu ofisini na wengine wameshaanza lawama kwa Kassim Majaliwa wakimtaka aende na kasi ya Rais.
Maswali yapo mengi ya kujiuliza.
Je Majaliwa ana sauti kiasi gani kwa Rais? je ataweza hata kumkosoa bossi wake? au kupendekeza watu kwenye baraza la mawaziri? au itakuwa kama Nyerere na Kawawa? Mwalimu na mwanafunzi? na je mapungufu na makosa yakijitokeza. Majaliwa hatageuzwa 'Kawawa mwingine'?
Je kama maamuzi yote yatatoka kwa Rais, Majaliwa atatendewa haki? au ndo tutarudi kule kule?
Sifa ni za Magufuli, na makosa ni ya Majaliwa?
Kawawa alipewa tu maagizo na kuyatekeleza kwa uaminifu mkubwa. Kawawa aliwahi hata kuachiwa nchi, akawa Waziri mkuu wa Tanganyika huru na bado 'akamrudishia' Nyerere madaraka ya ukuu wa nchi. Lakini hata kwa waasisi ni nadra kutajwa...Utasikia Nyerere na Karume. kila lilioenda kombo wakati wa Nyerere lawama alipewa Kawawa.
Rais mpya Magufuli keshajipatia 'mashabiki' wenye jazba na wasiotaka hata akosolewe, ni kama wengine ni kama washaanza mchakato wa kumfanya Magufuli awe 'mtakatifu' mpya baada ya Nyerere, wakati ana siku 20 tu ofisini na wengine wameshaanza lawama kwa Kassim Majaliwa wakimtaka aende na kasi ya Rais.
Maswali yapo mengi ya kujiuliza.
Je Majaliwa ana sauti kiasi gani kwa Rais? je ataweza hata kumkosoa bossi wake? au kupendekeza watu kwenye baraza la mawaziri? au itakuwa kama Nyerere na Kawawa? Mwalimu na mwanafunzi? na je mapungufu na makosa yakijitokeza. Majaliwa hatageuzwa 'Kawawa mwingine'?
Je kama maamuzi yote yatatoka kwa Rais, Majaliwa atatendewa haki? au ndo tutarudi kule kule?
Sifa ni za Magufuli, na makosa ni ya Majaliwa?