Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Karudi baba fulani, toka safari ya nje
Kavimba yote maini, na kucheua punje
Wanae wakaleta ubani, ili kuepua njenje
Wakataka na madini, yawafae nje nje
Akatamka mtumbua, nimevimbiwa kwelikweli
Hata mkinitumbua, sitatapika nje nje mali
Roho yaniumbua, uhai waniacha dhalili
Kama mnataka vitumbua, mjiunge na serikali
Wakazidi kumdodosa, baba alopoteza imani
Baba yetu mwanasiasa, mbona unatupa deni
Akili zetu za kudesa, hazijajua yaliyo sirini
Kama tunataka pesa, tutapataje chamani?
======
NB: Vina na Mizani vitapangwa baadaye...
Kavimba yote maini, na kucheua punje
Wanae wakaleta ubani, ili kuepua njenje
Wakataka na madini, yawafae nje nje
Akatamka mtumbua, nimevimbiwa kwelikweli
Hata mkinitumbua, sitatapika nje nje mali
Roho yaniumbua, uhai waniacha dhalili
Kama mnataka vitumbua, mjiunge na serikali
Wakazidi kumdodosa, baba alopoteza imani
Baba yetu mwanasiasa, mbona unatupa deni
Akili zetu za kudesa, hazijajua yaliyo sirini
Kama tunataka pesa, tutapataje chamani?
======
NB: Vina na Mizani vitapangwa baadaye...
Ahsante kwa madongo!, na kwao kuwafikia!
Umewapinga vigongo, na sisi twashangilia
Wanatuvunja migongo, na wao wajinonea
Mfano wao vibwengo, na damu watunyonyea!
Wanajiita vigogo, ugogo wa kudokoa
Wanatugea vichogo, wakati wajishibia
Wala kidogo kidogo, na buyu wamalizia
Mfano wao vibwengo, jasho letu washibia
Watavifunga virago, na hilo naashiria
Watuwachia mihogo, maharage na bamia
Wajifanya kama mbogo, kwa wao uharamia
Mfano wao vibwengo, watoto watuulia!