Karibu tufanye biashara ya ajira

Karibu tufanye biashara ya ajira

Existentialist

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
554
Reaction score
377
Poleni na majukumu na uchovu wa safari ndefu ya kuumalizia mwaka ndo kwanza katikati lakini kwa wale wa serikalini hongereni kwa kuumalizia mwaka wa kimahesabu...

Niende kwenye mada, nina post ya Procurement officer awe amehitimu degree ya kwanza au diploma na kama ana CPSP ni added advantage ( Mshahara laki 7 hadi 9 Tshs), ila kwa wanasheria wanaamini hakuna mkataba usiokuwa na consideration ili ukamilike...

Consideration yenyewe ili upate hii nafasi:- Nina mdogo wangu kamaliza diploma ya banking and finance so ukimpatia nafasi kwenye bank yeyote ili mradi ajishikishe kwa muda nami ntakupatia nafasi hii...

NB: Biashara hii ni kwa wale wenye nia ya kusaidia wadogo zao au ndugu sifanyi biashara na mwanafunzi directly.....
 
mm ninayo degree ya procurement na 4 years experience, hyo kazi ni serikalini au ni wapi? nauliza hvyo coz nimeajiriwa serikalini na mshahara ni huohuo. Hapo ningevutiwa na aina ya kampuni na mazingira ya kazi na maslah nje ya mshahara. weka wazi hapa
 
Dah hapo kweli ni pazuri ila kuwa makini
 
...aliyetoa ela katoa ela bandia na aliyepokea ela kauza cheni bandia. waliozea jiji wanasema ngoma droo.
 
..hii ajira ni selikarini ama? nauliza hivi nikiwa na maana...huyo mdg wako lazma afanye bank? kwenye ofice za mikopo hataki?
 
mm ninayo degree ya procurement na 4 years experience, hyo kazi ni serikalini au ni wapi? nauliza hvyo coz nimeajiriwa serikalini na mshahara ni huohuo. Hapo ningevutiwa na aina ya kampuni na mazingira ya kazi na maslah nje ya mshahara. weka wazi hapa

Anahitajika fresh graduate ni NGO siyo serikalini......jamani serikalini apply secretariat ya ajira mimi sina huo uwezo wa kumpa mtu kazi serikalin
 
..hii ajira ni selikarini ama? nauliza hivi nikiwa na maana...huyo mdg wako lazma afanye bank? kwenye ofice za mikopo hataki?

Ajira ni ndani ya a very reputable NGO, ningependa zaidi afanye bank ila hata micro finance institutions siyo mbaya.....mlango uko wazi
 
Back
Top Bottom