Kanisa likiionya Serikali hapo linaingilia Siasa, likiisifia wako kimya

Kanisa likiionya Serikali hapo linaingilia Siasa, likiisifia wako kimya

Return Of Undertaker

JF-Expert Member
Joined
Jun 12, 2012
Posts
4,572
Reaction score
26,892
Hapa nazidi kushangaa na kuprove kuwa binadamu mapungufu ni mengi na hatujakamilika kiukweli kweli.

Ukimsikia askofu Munga wa KKKT, Pia askofu wa Morovian, na wengine wachache unapata faraja kuwa wako na watu hao wanaonekana wachache na wanyonge katika kutetea haki za raia wasio na sauti na wakiwasemea.

Lakini jana nimeshangaa kanisa kongwe kuungana na serikali kikandamiza haki za watanzania.

Hawa viongozi wa dini na sio wa kiroho walichokishuhudia kwenye chaguzi za mitaa wakati wa zoezi la uandikishaji, uchukuaji na urejeshaji wa fomu walitaka vyama vya upinzani wafanye nini ikiwa 96% ya wagombea walienguliwa? Wakae meza moja meza ipi?

Dini ipo kwa kisudi la haki. Je kuna haki katika mchakato huu?

Hivi mnafikiri waumini wenu wasipoipata haki huko makanisani watakuja kufanya nini? Mnaongoza watu kiroho au kimaslahi ya kiserikali.

Mbona kipindi cha Kikwete mlikuwa huru na wazi kukosoa kwa Magufuli mna hofu ya ukatoliki wake?

Na kwa kauli ya jana mbona sijasikia ule msemo pendwa ya Kaisari mwachieni Kaisari na ya Mungu aachiwe Mungu.

Msemo huu huja pindi tu serikali imeonywa na kauli mbiu vueni majoho wapande kwenye majukwaa.

Ila kwa kauli hii safi kabisa.

Nilikumbushe kanisa toka mwanzo na historia ya dini iko wazi hakuna mtakatifu wala mtume anayejulikana kwa kuwa pamoja na serikali kwa sababu watu hao walitaka haki toka kwa watawala na neno la Mungu ni mwanga wa haki ambayo binadamu huinyima na kujimilikisha
 
Well said, nimeshangaa sana sana kwa Kanisa hili kutoa tamko kama lile, I think wangekaa kimya tu ili kulinda reputation yao! Tunapita kwenye kipindi kigumu sana
IMG_20170213_124601.jpeg
 
Kauli ya Kanisa Katoliki ina nguvu sana kuliko sauti za madhehebu na dini zote zilizobakia ukizijumlisha pamoja!
 
Huyo ni askofu, katoa maoni yake binafsi, na uhuru huo anao. Ingekuwa ni msimamo wa kanisa katoliki, basi wangetoa waraka ambao ungeelekezwa kwa waumini kupitia ngazi za majimbo, parokia, na hata vigango.

Tathmini ya haraka haraka inaonyesha makanisa na hata misikiti imejitenga na kuongea chochote minachohusu huu uchaguzi. Mmeambiwa "mwenye macho na atazame aamue mwenyewe". Huo ndiyo ninaoweza kuuona kama msimamo rasmi wa kanisa katoliki na hata madhehebu mengine.
 
.... viongozi wa kanisa katoliki ni vyema mkajua sisi waumini wenu sio watoto wadogo, kuja kwetu kanisani na kukaa kimya mpaka ibada inaisha, haina maana sisi waumini wenu ni makondoo ( kama tunavyoitwa sisi ni kondoo wenu) tuna akili zetu timamu vizuri sana tu.

#tuheshimiane.
 
.... viongozi wa kanisa katoliki ni vyema mkajua sisi waumini wenu sio watoto wadogo, kuja kwetu kanisani na kukaa kimya mpaka ibada inaisha, haina maana sisi waumini wenu ni makondoo ( kama tunavyoitwa sisi ni kondoo wenu) tuna akili zetu timamu vizuri sana tu.

#tuheshimiane.
Kwani wewe ni kondoo?
 
.... viongozi wa kanisa katoliki ni vyema mkajua sisi waumini wenu sio watoto wadogo, kuja kwetu kanisani na kukaa kimya mpaka ibada inaisha, haina maana sisi waumini wenu ni makondoo ( kama tunavyoitwa sisi ni kondoo wenu) tuna akili zetu timamu vizuri sana tu.

#tuheshimiane.
Ninachoshangazwa, badala ya kumlaumu na kumshauri ALIYEMPIGA KIBAO MWENZIE, wao wanamlalamikia ANAYELIA, BAADA YA KUPIGWA KIBAO!
 
Moja kati ya karata nzuri ya jiwe msimu huu ni RC..anaelewa kupitia viongozi wa RC nyumbu wengi wataendelea kuwa na imani naye...
 
Kila mtu anavutia kamba upande wake;

Kanisa likionya kwa mambo ambayo yanafurahisha watu fulani ( Utasikia wahusika wakisema, limetimiza wajibu wake) lisipoonya kwa mambo yanayofurahisha upande fulani ( Utasikia wahusika wakisema, linatumika)
 
Dini ipo kwa kisudi la haki. Je kuna haki katika mchakato huu?

Hivi mnafikiri waumini wenu wasipoipata haki huko makanisani watakuja kufanya nini? Mnaongoza watu kiroho au kimaslahi ya kiserikali.
Kanisa lipo kututayarisha kwa maisha ya baadae-huko tunaita /tumeambiwa mbinguni. Hapa ndio "kumpenda Mungu" na "Jirani yako" vinahusika.

Tukiwa hapa duniani Kanisa linatakiwa kuhakikisha tunaishi kwa haki na tunatawaliwa/kuongozwa kwa kutumia mbinu za utawala bora nasi tuna mpa Siza ya ya Siza kama kulipa kodi na kutii mamlaka zilizowekwa na Mungu.
Tatizo linakuja pale hizo mamlaka zinapotaka utii bila kutimiza vizuri wajibu wake.

Hivyo basi bila haki na utawala bora tuna haki ya kupiga kelele na kuchukua hatua zitakazo rekebisha mambo. Kanisa au Dini yeyote wakituunga mkono tunapata nguvu vininevyo tunadhoofika lakini wajibu ni wetu kuhakikisha tunaishi maisha yenye haki na utawala bora.

Kuna wanaopenda kuongelea KUFUATA SHERIA hasa serikali na wapambe wake, lakini ni ukweli usio fichika kuna sheria zinazonyima raia haki za msingi hizi nazo ni za kupigwa vita.
 
Hahahaha nilikua nafukunyua mafaili yangu nikazikuta hizo picha! Ilikua safari moja amazing sana sana! Tulitoka Kigoma tukapita kote huko tukalala Biharamulo kesho tukaibukia Bukoba then jioni tukalala Mwanza, ilikua siku ya Mtatifu Valentino... Acha siku zipite.
Mzee hii picha imenikumbusha mbali sana
Acha maisha yaendelee
 
Askofu Nyaisonga ni Askofu wa Jimbo la Mbeya na sio msemaji wa kanisa katoliki Tanzania. Ingekua ni kauli ya kanisa nzima la Tanzania kauli hiyo ingetolewa kipitia waraka na sio Kama alivyofanya. Inawezekana yakawa maoni yake binafsi.
Hata hivyo asingepaswa kuongea lolote kutokana na uongo wa siasa za Tanzania ulivyo, wanasiasa hawana utu, hawana ukomavu, hawana adabu, ni waongo na wezi angewaacha waendelee na uhuni wao
 
Kila mtu anavutia kamba upande wake;

Kanisa likionya kwa mambo ambayo yanafurahisha watu fulani ( Utasikia wahusika wakisema, limetimiza wajibu wake) lisipoonya kwa mambo yanayofurahisha upande fulani ( Utasikia wahusika wakisema, linatumika)
Wewe,unashauri nini kifanyike???
 
Back
Top Bottom