Trainee
JF-Expert Member
- Sep 22, 2018
- 3,026
- 4,036
Habari zenu,
Tumeshuhudia kampuni za mitandao ya simu zikishirikiana (kufanya kazi) kwa namna tofauti tofauti. Mfano mzuri ni hili la juzi la Tigo na Zantel kuungana na kushare karibu huduma zote muhimu za simu.
Juzi nimekutana na jambo la ajabu katika maswala hayo na sijapata majibu mpaka sasa!
Naanza stori,
Jamaa yangu mmoja ana laini yake ya Vodacom ambayo anatumia siku zote hapa kijijini sasa juzi akaenda sehemu (kijiji jirani) katika harakati zake za maisha.
Baada ya muda fulani akakuta laini yake ya Vodacom kwenye screen ya simu inasomeka airtel. Jamaa anasema hakushtuka akajua ni maswala ya minara tu (yaani aliweka halotel na Vodacom lakini sasa ikawa inasomeka/inaonekana ni halotel na airtel.
Kubwa la kushangaza zaidi ni pale aliponunua vocha ya Vodacom na ikakataa kuingia kwenye laini hiyo lakini akajaribu kuweka vocha ya airtel ikakubali akajiunga kifurushi kabisa na kuwasiliana.
Wakati wa kurudi nyumbani alifika sehemu laini ikajirudisha kusoma Vodacom na akaendelea na huduma za kila siku watoazo Vodacom.
Tukio hilo limeniacha njia panda halafu laini yenyewe nilipojaribu kuichunguza nikagundua kuwa siyo ya kawaida sana (kama laini nyingine za voda) kiasi kwamba mtu hawezi kuamini haraka kwamba ni voda akiiangalia.
Nyongeza na hilo,
Kuna jamaa mwingine voda yake akiweka ndani muda mrefu siku akisema aichukue aweke hewani anakuta ofa ya dakika na mb za kutosha! Mpaka jamaa ameshazoea anaitoa laini anaficha ndani hata miezi miwili kisha anaiweka tena hewani (na mchezo umekuwa ni huo kila dakika za bure zinapokata).
Tumeshuhudia kampuni za mitandao ya simu zikishirikiana (kufanya kazi) kwa namna tofauti tofauti. Mfano mzuri ni hili la juzi la Tigo na Zantel kuungana na kushare karibu huduma zote muhimu za simu.
Juzi nimekutana na jambo la ajabu katika maswala hayo na sijapata majibu mpaka sasa!
Naanza stori,
Jamaa yangu mmoja ana laini yake ya Vodacom ambayo anatumia siku zote hapa kijijini sasa juzi akaenda sehemu (kijiji jirani) katika harakati zake za maisha.
Baada ya muda fulani akakuta laini yake ya Vodacom kwenye screen ya simu inasomeka airtel. Jamaa anasema hakushtuka akajua ni maswala ya minara tu (yaani aliweka halotel na Vodacom lakini sasa ikawa inasomeka/inaonekana ni halotel na airtel.
Kubwa la kushangaza zaidi ni pale aliponunua vocha ya Vodacom na ikakataa kuingia kwenye laini hiyo lakini akajaribu kuweka vocha ya airtel ikakubali akajiunga kifurushi kabisa na kuwasiliana.
Wakati wa kurudi nyumbani alifika sehemu laini ikajirudisha kusoma Vodacom na akaendelea na huduma za kila siku watoazo Vodacom.
Tukio hilo limeniacha njia panda halafu laini yenyewe nilipojaribu kuichunguza nikagundua kuwa siyo ya kawaida sana (kama laini nyingine za voda) kiasi kwamba mtu hawezi kuamini haraka kwamba ni voda akiiangalia.
Nyongeza na hilo,
Kuna jamaa mwingine voda yake akiweka ndani muda mrefu siku akisema aichukue aweke hewani anakuta ofa ya dakika na mb za kutosha! Mpaka jamaa ameshazoea anaitoa laini anaficha ndani hata miezi miwili kisha anaiweka tena hewani (na mchezo umekuwa ni huo kila dakika za bure zinapokata).
lain yako ya vodacom itafanya kaz na internet itafanya kaz na itasoma mtandao wa japan