Kampeni za manyanga, nesema zinanikera
Wenyewe munazipanga, nasisi tunawachora!
Mfano wenu wajinga, mwaonekana uchwara!
Nasema munanikera, kwa vyenu vyote vimbwenga!
Nasubiria novemba, ambapo zitapotea
Mujitangaze umwamba, na suti kujivalia
Kwa sasa mwaficha pamba, suti zenu asilia
Najua zitapotea, batiki na vyo vilemba
Kwa sasa zimefichika, nizisemazo ni suti
Na nyote mwacheka cheka, mwaogopa kula buti
Vigoda pia mikeka, mwakalia hati hati
Imeshakuwa shuruti, kila kona mwaoneka!
Novemba twasubiria, mje ingia mitini
Muanze kutukimbia, kujificha ofisini
Ni kura mwapalilia, ujanja wakizamani
Utadhaninia watani, kwa kura mkililia
Nasema mushatuchosha, twawajua miyeyusho
Kwa dhati ninawapasha, wengi wenu ni michosho
Uthadhani washawasha, wakati mwataka posho
Roho zenu za korosho, na mimi nawajuslisha!
Wenyewe munazipanga, nasisi tunawachora!
Mfano wenu wajinga, mwaonekana uchwara!
Nasema munanikera, kwa vyenu vyote vimbwenga!
Nasubiria novemba, ambapo zitapotea
Mujitangaze umwamba, na suti kujivalia
Kwa sasa mwaficha pamba, suti zenu asilia
Najua zitapotea, batiki na vyo vilemba
Kwa sasa zimefichika, nizisemazo ni suti
Na nyote mwacheka cheka, mwaogopa kula buti
Vigoda pia mikeka, mwakalia hati hati
Imeshakuwa shuruti, kila kona mwaoneka!
Novemba twasubiria, mje ingia mitini
Muanze kutukimbia, kujificha ofisini
Ni kura mwapalilia, ujanja wakizamani
Utadhaninia watani, kwa kura mkililia
Nasema mushatuchosha, twawajua miyeyusho
Kwa dhati ninawapasha, wengi wenu ni michosho
Uthadhani washawasha, wakati mwataka posho
Roho zenu za korosho, na mimi nawajuslisha!