Mabagala
JF-Expert Member
- Nov 27, 2009
- 1,477
- 325
Nimejichokea zangu narudi kutoka kazini, niko kwenye usafiri wetu wa jumuia. Foleni ilipoanza kunoga basi kamjadala kakaanza mara baada ya kupita kibasi kikiwa na abiria wenye nguo za njano na kijani (sikuelewa ni wana yanga ama wana Chama Cha Matamu). Kama utani vile mjadala ukaanza. Jamaa kadai maisha magumu kwa upande wake yamesababishwa na mama yake. Kama mama yake angekuwa mjanja basi angemdate fisadi mmoja wapo na yeye asingezaliwa katika familia duni! Hoja mbali mbali zilitolewa hadi uchovu wa foleni ukasahaulika. Nilisahau uchovu wa foleni pale jamaa alipodai viongozi wanadai wameongeza ajira kwa kuangalia vijana waokotao vyuma chakavu na machupa ya maji yaliyokwisha tumika. Nimejikuta nimeshafika safari yangu, sijui huko mbele mjadala umeishaje! Ila nina hakika mijadala ya kwenye usafiri wa daladala huwa haina hitimisho. Wale mlio na usafiri binafsi mnakosa mijadala kama hii!
Mungu irehemu nchi yetu
Mungu irehemu nchi yetu