Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Agizo hilo limetolewa Mkoani Morogoro leo Machi 12, 2026 na Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Prof. Joyce Ndalichako, baada ya wajumbe wa Kamati hiyo kukagua na kuridhishwa na maendeleo ya ujenzi huo ambao umefikia asilimia 74 ya utekelezaji.
Ameongeza kuwa Kamati itaendelea kushirikiana na Wizara ya Ujenzi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa ubora unaozingatia masharti ya mkataba.
Awali akiwasilisha taarifa ya maendeleo ya mradi huo mbele ya Kamati, Waziri wa Ujenzi Abdallah Ulega, ameeleza kuwa Wizara imeendelea kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa jengo hilo la ghorofa nne (4) litakalokuwa na ofisi za idara za kitaaluma pamoja na madarasa yatakayoweza kuhudumia wanafunzi takribani 1,000 kwa wakati mmoja ili likamilike na liweze kutoa huduma iliyokusudiwa.
Aidha, Waziri Ulega ameishukuru Kamati hiyo kwa kuibua wazo la ujenzi wa jengo hilo na kwa kuendelea kufuatilia maendeleo ya Taasisi hiyo ili kuhakikisha inatimiza malengo ya kuongeza wataalamu wenye ujuzi katika Sekta ya Ujenzi.
Mradi wa ujenzi wa jengo la taaluma la ICoT unagharimu kiasi cha Shilingi Bilioni 5.978 na kutekelezwa na Mkandarasi Mzawa B.H. Ladwa na kusimamiwa na Mhandisi Mshauri Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).