GE2025 Kamati ya amani ya mkoa wa Mwanza: Tutaendelea kuwahamasisha Watanzania wakapige kura na kudumisha Amani

GE2025 Kamati ya amani ya mkoa wa Mwanza: Tutaendelea kuwahamasisha Watanzania wakapige kura na kudumisha Amani

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
844
Reaction score
1,606
Kamati ya amani ya mkoa wa Mwanza imesema, kwa kushirikiana na serikali pamoja na viongozi wa dini zote nchini, itaendelea kutoa hamasa kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa uhuru na haki tarehe 29 Oktoba 2025, huku ikiwahimiza wananchi kutumia haki yao ya msingi kwenda kuchagua viongozi wanaowataka katika ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani.

Kamati hiyo imeeleza hayo katika tamko la pamoja lililotolewa leo Oktoba 20, 2025, baada ya kukamilika kwa kongamano la amani la viongozi wa dini mbalimbali lililofanyika mkoani Mwanza. “Tutaendelea kuhamasisha wananchi wa mkoa wa Mwanza na nchi nzima kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa uhuru na haki siku ya tarehe 29, Oktoba 2025.”

Imeeleza kamati hiyo. Kamati hiyo imewasisitiza wananchi kuwa baada ya zoezi la kupiga kura warudi katika makazi yao kwa utulivu, bila vurugu na maneno ya chuki, ili kudumisha taswira njema ya taifa.

Aidha, imebainisha kwamba itaendelea kuhakikisha inasimamia maombi katika kipindi chote cha uchaguzi, ikisisitiza kwamba jamii itambue kuwa amani ndiyo nguzo pekee ya maendeleo katika taifa.

 
Hizi kamati mbona ziko kisiasa sana sana? Tena siasa za upande mmoja. Hizi kamati zingebaki neutra tu kwa kuwa kuna kundi kubwa la wananchi nao wana madai ya msingi wakitaka haki itendeke ndio watashiriki uchaguzi. Wamekataa kushiriki bila reforms na wana haki zao za msingi
 
Hizi kamati mbona ziko kisiasa sana sana? Tena siasa za upande mmoja. Hizi kamati zingebaki neutra tu kwa kuwa kuna kundi kubwa la wananchi nao wana madai ya msingi wakitaka haki itendeke ndio watashiriki uchaguzi. Wamekataa kushiriki bila reforms na wana haki zao za msingi
 
Tanzania ni kisima cha Amani,kisicho na Haki
 
Kamati ya amani ya mkoa wa Mwanza imesema, kwa kushirikiana na serikali pamoja na viongozi wa dini zote nchini, itaendelea kutoa hamasa kwa Watanzania kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa uhuru na haki tarehe 29 Oktoba 2025, huku ikiwahimiza wananchi kutumia haki yao ya msingi kwenda kuchagua viongozi wanaowataka katika ngazi ya Urais, Ubunge na Udiwani.

Kamati hiyo imeeleza hayo katika tamko la pamoja lililotolewa leo Oktoba 20, 2025, baada ya kukamilika kwa kongamano la amani la viongozi wa dini mbalimbali lililofanyika mkoani Mwanza. “Tutaendelea kuhamasisha wananchi wa mkoa wa Mwanza na nchi nzima kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa uhuru na haki siku ya tarehe 29, Oktoba 2025.”

Imeeleza kamati hiyo. Kamati hiyo imewasisitiza wananchi kuwa baada ya zoezi la kupiga kura warudi katika makazi yao kwa utulivu, bila vurugu na maneno ya chuki, ili kudumisha taswira njema ya taifa.

Aidha, imebainisha kwamba itaendelea kuhakikisha inasimamia maombi katika kipindi chote cha uchaguzi, ikisisitiza kwamba jamii itambue kuwa amani ndiyo nguzo pekee ya maendeleo katika taifa.

Mlishindwa kuhamasisha haki sasa mnahamasisha amani?
 
Back
Top Bottom