Kamati kuu CHADEMA angalieni Huu ushauri

Kamati kuu CHADEMA angalieni Huu ushauri

Dik

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2011
Posts
1,205
Reaction score
416
Kamati kuu CHADEMA angalieni huu ushauri kama utawafaa muuchukue,kama haufai basi muuache!BAADA YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA:
1. Zungukeni maeneo yote mliopaswa na mlikosimamisha wagombea, fanyeni utafiti wa kina mgundue mmeshinda aummeshindwa kwakiwango gani. Hiiitawasaidia kujua ni wapi mmeteleza na ni wapi pakujipanga kwakuongeza nguvu.Kwa walewagombeawalioenguliwamtajua kama wanahaki ya kukatiwarufaa au la na kamawanayo mfanyehivyo.

2. Toeni shukrani zadhati kwawananchi natumieni nafasi hiyokuwapa sera zakukazia maamuziyao waliochukua ili waonehawajakosea,nawalichofanya nisahihi hivyowakidumishe.

3. Toeni semina yauongozi nakiutendaji kwawale wotewalioshinda katikanafasi mbalimbaliili waweze kufiti nakudeliver vizurihuduma kwawananchiwaliowaamini nakuwachagua.Nasema hvi kwasababu kunasehemuwamesimamawagombea waCHADEMA nawameshinda lakinihawana skills zakiuongozi. Kufanyahivyokutawaongezeaufanisi nakuwafanyawakiwakilishechama vizuri.

4. Wekeni mikakati ya mwaka kesho hasakwa yale maeneoambayo mlipatakurakidogo auhamkushinda auhamkusimamishawagombea mpatewagombea wenyesifa kwa maeneoyote kwa ngazi zaudiwani na ubunge.

NAWASILISHA!
 
Ni ushauri mzuri wataufanyia kazi mkuu.
 
Kubwa zaidi katika hizo semina elekezi mtoe maonyo makubwa sana kwa hao viongozi kujiepusha na rushwa ili wananchi waone tofauti yao na wale wa CCM. Wajue wazi kuwa sehemu nyingine sio kuwa Chadema imeshinda kwa kupendwa sana maana wapo walioichagua bado hawaijui vizuri bali rushwa ya wale viongozi wa CCM ilikuwa kero kwao.
Wafamisheni kuwa chama kinayo mamlaka ya kuwafukuza uanachama viongozi watakaobainika kuwa wala rushwa hivyo heshima mbele ya wananchi itakomaa.
 
ushauri huu tutaufanyia kazi kamanda CHADEMA ni chama makini tunasikiliza ushauri makini ..
 
1. Kwa kuongezea muwe karibu na viongozi waliochaguliwa kuwaelimisha zaidi juu ya sera za chama utekelezaji na matumizi ya rasilimali watu fedha kidogo ya eneo iliyopo itumike kwa uadilifu mkubwa ili kujenga ngome imara ya ukawa eneo husika
2: kuwashirikisha wananchi wote bila kujali itikadi zao katika kujiletea maendeleo yao kwa kuwashirikisha kila jambo lolote linalowahusu waliamue wao kwa ajili ya utekelezaji. Ukweli ni kuwa kuna mahali wana ukawa ndio wameingia kwa mara ya kwanza na kama zari wakashinda. Hapo kwa vyovyote vile mgombea wa ukawa atakuwa hajaelewa sera na itikadi za chama kimojawapo cha ukawa kwani huenda wananchi walichagua kwa hasira so magamba yanaweza kutumia mwanya huo kuondosha hasira au kumnunua na kiongozi yule na hatimae kupoteza nafasi hiyo muhimu. Hapa natoa angalizo kwa cdm mwanga kwani alieshinda kijiji cha kighare usangi anazo tabia za kubadilika badilika kwa kifup ana price tag
3. Kujenga upendo na kuhudumu kwa uadilifu mkubwa, kumbukeni maeneo yote wanaukawa walishika yatapata vikwazo vikali vya kichumi kutoka chama dola na dola yenyewe ili kuwakomoa wananchi hao so rasilimali kidogo iliyokuwepo itumike vizuri kwani hili lipo kwenye ilani ya uchaguzi ya chadema2010 ilikuwa na jukumu la kupunguzo michango na gharama za maisha
 
Ushauri mzuri sana. Tafadhali sana viongozi CHADEMA lifanyieni kazi hili. viongozi wote waliochaguliwa wanapaswa kupewa elimu ya ungozi mzuri kwa wananchi na kuepukana na maswala yote ya rushwa. Tafadhari kukitokea malalamiko yoyote kutoka kwa wananchi juu ya kiongozi wao waliyemchagua nashauri aondolewe mapema ili chama kiendelee kuaminiwa na wananchi.
 
Huu ni bonge ya ushauri, kwani uzoefu unaonyesha viongozi wa kiafrika kama tumelogwa na mchawi mmoja. Usishangae leo tunaitoa ccm inaingia cdm ndio inakuwa balaa zaidi. Nashauri wote waliochaguliwa na kuwekewa mapingamizi taarifa zao zifike kwenye vyama husika ili kufanya tathmini ya ushindi na kushindwa na nini ilikuwa sababu. Halafu hao waliochaguliwa lazima wahakikishe wanafanya kazi halali na sio kutegemea cheo kama ndio sehemu ya kutokea kimaisha. Kinyume na hapo tutaona kilekile kinachotokea kwa viongozi wa ccm kwani wengi wao hawana kazi bali wapiga deal za kuuza viwanja na kuwa kero ya kuwa ombaomba kwa wananchi wao. Pale wanapoona wanakwama wasisite kuomba ushauri wa wananchi wao na ngazi za juu za vyama vyao ili ifahamike hatua sahihi za kuchukua. Nasema hivi kwani kuna mambo mengi ya kisheria na kikanuni nina uhakiki wengi hawajui na wakumbuke chama dola ni mabingwa wa hila. Rejeeni mapingamizi mengi yalikuwa ni mambo madogomadogo kama kukosea tu kujaza fomu ikala kwao.
 
Kila kijana ana marafiki zaidi ya kumi na zaidi ahakikishe kila rafiki au jirani yake anajuwa kuwa ccm ni wezi na njia pekee ya kukomboa Tanzania kutoka kwenye watu wenye tamaa kama ccm ni kura kwaiyo sisi vijana tuhamasishane zaidi na zaidi na tujuwane kabla ya kura kuwa kati ya marafiki kumi ni wangapi hawana mtindio wa ubongo kama yule bibi fox
 
Pia chadema msisahau kutoa shukrani kwa mganga wenu ramli yake aliyawapigia imewasaidia sana
 
Naongezea mpaka sasa hivi nguvu ya ccm iko vijijini naomba kwa nguvu kubwa ihamie vjijini ili watu waelimishwe wajitambue maana wameshatishwa sana kuwa wakichagua upinzani kutakuwa na vita hivyo tukiweza kuwatoa hiyo hofu ukombozi U miknoni mwetu iwe kazi rahisi 2015 tukiweza huko ni kazi rahisi itakayobaki ni kumsukuma mlevi,naomba sana hii iwe kazi muhimu naamini tutashinda bila shida.
 
Kuongeza, Ni wakti wa KUWAPENDA ahta MAADUI ZENU hasa CCM, maaana kw akufanya hivyo ndio mtaweza kuwamaliza na kuwafuta kabisa.
 
Ushauri makini, kuna mahali mimi na rafiki zangu tumeanza kutoa elimu ya uongozi kwa viongozi wa CDM kwa gharama zetu. Tumeamua kujitolea.
 
Pia tunaishaur ccm iache kuhangaika kuweka wagombea kwani tayari tushawachokaaaaaa
 
Back
Top Bottom