Kama ungekuwa Rais ungebadilisha kitu gani?

Boss Man

JF-Expert Member
Feb 10, 2022
458
991
Wakubwa ebu leo tujichallange kidogo, tusiishie kukosoa tu huku tukiwa benchi ebu Leo tujipe madaraka ya Urais na kila mtu aseme kwa nafasi yake kama ungekuwa Rais ungefanya Nini? au ungeboresha kitu gani? pengine baadhi ya maoni yanaweza kuchukuliwa hapa na kufanyiwa kazi


Binafsi kama Mimi ndio namba One, ningeboresha kwenye swala la usafiri wa umma na ningepiga marufuku matumizi ya magari binafsi siku za kazi (weekdays) na ningeyaruhusu siku za weekends tu, hata wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za serikali wangekuwa na mabasi yao pamoja na wabunge, mambo ya V8 kuendea jimboni kwako tu

Kwanza kabisa hii ingesaidia kupunguza foleni na kufika kazini kwa wakati, na mafuta yangekuwa bei rahisi, matabaka yangepungua kwa kiasi kikubwa, pia ingesaidia kupunguza ulimbukeni wa vijana kukimbilia kumiliki magari bila sababu za msingi

Kitu kingine ningechukua vijana wote waliokosa kazi na kuwapeleka semina za kilimo baada ya nawaimgiza maporini huko kwenye mashamba pembejeo Kila kitu Bure, ukishavuna serikali inakula asilimia 60% ya mavuno kwa misimu 3 mfululizo baada ya hapo unaachwa undelee mwenyewe, na uamuzi ni wako kuendelea na kilimo au kufanya Biashara nyingine

Hii itasaidia nchi kuwa na chakula Cha kutosha, hvyo hata bei za vyakula masokoni itakuwa ni rafiki kwa mwananchi wa kawaida na pia tutakuwa tumepunguza vijana wengi wasio na Kazi na kujipatia mitaji kwa style hiyo

Hayo ni machache kati ya mengi ambayo ningeyafanya au natamani serikali ingeyafanya, siwezi kueleza yote nimewaachia na nyie Uwanja

NB: Ni ruksa kukosoa mawazo ya mtu ila kwa hoja, hata Mimi unaweza kunikosoa hayo mawazo yangu kwa hoja


Je wewe ungefanya/boresha nini?
Screenshot_20220630-143812.jpg
 
1. Kitu cha kwanza ni kuinasua nchi itoke kwenye makucha na mitego michafu na hatari ya London & Washington. Tanzania haiendelei vilivyo kwa sababu imekabwa koromeo na mabepari manyang'au chini ya hisani na baraka za viongozi vipofu.

2. Ondoa matumizi yasiyo ya lazima (hii ni muhimu sana!)

3. Wekeza katika miradi ya maendeleo himilivu.

4. Punguza kuendekeza mikopo.

5. Wajengee uwezo wananchi WOTE (mtu mmoja-mmoja)--elimu, afya, mapato.
 
Ningesema idea zangu ila tatizo washenzi katika hii nchi ni 90% huku ambao tunajali uzalendo ni 10% watakuja kuniua bure tu ili waendelee kulamba asali.

Tip: Ni ku reform CCM. Nafukuza wanachama wote naanzisha chama upya with new spirits. Nasajili viongozi wa madrasa na wana Ukwata tu 😂😂😂 pamoja na masheikh na maaskofu.
Wahuni wote napiga chini.
 
Ningesema idea zangu ila tatizo washenzi katika hii nchi ni 90% huku ambao tunajali uzalendo ni 10% watakuja kuniua bure tu ili waendelee kulamba asali.

Tip: Ni ku reform CCM. Nafukuza wanachama wote naanzisha chama upya with new spirits. Nasajili viongozi wa madrasa na wana Ukwata tu pamoja na masheikh na maaskofu.
Wahuni wote napiga chini.
Ila angalia tu hao ukatao waweka
Wasije wakajifunza uhuni

Ova
 
1. Kitu cha kwanza ni kuinasua nchi itoke kwenye makucha na mitego michafu na hatari ya London & Washington. Tanzania haiendelei vilivyo kwa sababu imekabwa koromeo na mabepari manyang'au chini ya hisani na baraka za viongozi vipofu.

2. Ondoa matumizi yasiyo ya lazima (hii ni muhimu sana!)

3. Wekeza katika miradi ya maendeleo himilivu.

4. Punguza kuendekeza mikopo.

5. Wajengee uwezo wananchi WOTE (mtu mmoja-mmoja)--elimu, afya, mapato.
Hiyo namba 1 inabidi uwe Putin haswa
 
Kwa kweli mimi ningekuwa rais ningepambana kwanza haki iwe inatendeka kila mahali hasa kwenye taasisi kama mahakama na ofisi mbalimbali, hii nchi connection zimezidi.

Ningefumua baadhi ya mifumo iliyoundwa wakati wa chama kimoja ikiwa ni pamoja na kurudisha viwanja vya ccm kwa serikali, ningebalance kipato kwa kila ngazi tofauti na sasa wanasiasa wanaishi km wako edeni huku wananchi wakiishi km wako jehanum.
Ningerudisha viwanda vyetu vilivyotaifishwa au kuuliwa kihuni km General tyre Arusha na Karatasi Mgololo Iringa, huwa naumia sana kwa hivi viwanda

Ningetengeandaa katiba mpya ambayo ingepunguza mamlaka ya rais na kuyarudisha kwa wananchi, pia suala la muungano tungelijadili na kuboresha kulingana na mahitaji ya wananchi.

Ningefuta vyeo vya wakuu wa mikoa na wilaya maana hawana tija ni kuongeza tu mizigo kwa serikali, wakurugenzi wanatosha kabisa kusimamia mambo wakiwa na makatibu tawala.

Ningefanya mengi nyie acheni tu!
 
1.boresha kilimo
2.elimu
3.ajira za uhakika
4.afya
5.miundo mbinu bora achana na mindege
 
Ningesema idea zangu ila tatizo washenzi katika hii nchi ni 90% huku ambao tunajali uzalendo ni 10% watakuja kuniua bure tu ili waendelee kulamba asali.

Tip: Ni ku reform CCM. Nafukuza wanachama wote naanzisha chama upya with new spirits. Nasajili viongozi wa madrasa na wana Ukwata tu pamoja na masheikh na maaskofu.
Wahuni wote napiga chini.
Sasa huku kwenye Dini tutaongozwa na nani? na utasababisha ma-Sheikh na maaskofu kuwa viongozi wa Dini kwa lengo la kuingia katika siasa hapo badae, maana next term watahitajika wengine.... hapo uhuni ndipo unapoanzia Sasa

Yani kwa kifupi utakuwa umeleta uhuni hadi kwenye Dini Sasa...
 
Kwanza katiba mpya yenye kuipa kila mhimili nguvu kubwa bila kutegemea mwingine na adhabu iwe ni kifo risasi hadharani kwa wezi wa mali za umma au wanaosign mikataba mibongo ya kuigharimu nchi, mikataba yote iwe wazi na ijadiliwe bungeni...

Kuwa waziri lazima kufanyike vetting sio kuteua tuu, Nchi ingegawanywa kwa kanda yenye serikali ndogo ndani yake kwa kila kanda.

Elimu hii mkoloni ingekufa Natura death tuje na elimu inayoendana na mazingira yetu..

Mwisho ningeresign urais baada ya hayo yote kukaa sawa maana siupendi aje mwingine mimi nikaendelee na biashara
 
Wakubwa ebu leo tujichallange kidogo, tusiishie kukosoa tu huku tukiwa benchi ebu Leo tujipe madaraka ya Urais na kila mtu aseme kwa nafasi yake kama ungekuwa Rais ungefanya Nini? au ungeboresha kitu gani? pengine baadhi ya maoni yanaweza kuchukuliwa hapa na kufanyiwa kazi


Binafsi kama Mimi ndio namba One, ningeboresha kwenye swala la usafiri wa umma na ningepiga marufuku matumizi ya magari binafsi siku za kazi (weekdays) na ningeyaruhusu siku za weekends tu, hata wafanyakazi wa taasisi mbalimbali za serikali wangekuwa na mabasi yao pamoja na wabunge, mambo ya V8 kuendea jimboni kwako tu

Kwanza kabisa hii ingesaidia kupunguza foleni na kufika kazini kwa wakati, na mafuta yangekuwa bei rahisi, matabaka yangepungua kwa kiasi kikubwa, pia ingesaidia kupunguza ulimbukeni wa vijana kukimbilia kumiliki magari bila sababu za msingi

Kitu kingine ningechukua vijana wote waliokosa kazi na kuwapeleka semina za kilimo baada ya nawaimgiza maporini huko kwenye mashamba pembejeo Kila kitu Bure, ukishavuna serikali inakula asilimia 60% ya mavuno kwa misimu 3 mfululizo baada ya hapo unaachwa undelee mwenyewe, na uamuzi ni wako kuendelea na kilimo au kufanya Biashara nyingine

Hii itasaidia nchi kuwa na chakula Cha kutosha, hvyo hata bei za vyakula masokoni itakuwa ni rafiki kwa mwananchi wa kawaida na pia tutakuwa tumepunguza vijana wengi wasio na Kazi na kujipatia mitaji kwa style hiyo

Hayo ni machache kati ya mengi ambayo ningeyafanya au natamani serikali ingeyafanya, siwezi kueleza yote nimewaachia na nyie Uwanja

NB: Ni ruksa kukosoa mawazo ya mtu ila kwa hoja, hata Mimi unaweza kunikosoa hayo mawazo yangu kwa hoja


Je wewe ungefanya/boresha nini?View attachment 2277496
Ningeunda bunge na taasisi zote za usalama ningezofanya kuwa za ma genius. Hupati cheo kwa kujikomba nakusema mtukufu rais Brain ndio itakubeba kilaza kaa pembeni. Naninaposema kilaza sio wadarasani tu maana kuna watu ni prof ila nivilaza. Yani umefanya nini kwa taifa lako hilo ndio swali lakwaza kujiuliza nakupanda daraja. Kiongoz asie wajibika kwa wananchi hatufai yani taifa hili la Tz lingepaa kama ndege. Rais sio Mungu ningetaka watu wawe Uhuru kukosoa na sheria iwalinde. Vijana na wazee wangefurahi sana Japo wazembe na majizi wangepata tabu sana japo ukiiba kwa akili tunakupa kaz maalumu. End
 
Hahaa.. yani nimesoma naishia kucheka tu.

Hivi wakuu nyie mnadhani hao waliopo madarakani hawayaoni hayo mnayoyaandika hapa. Siasa ni game na kila game ina sheria zake so kinachoendelea wao wenyewe wanafuata sheria za game. Wanasema don't hate the player hate the game

Mi naendelea kusoma COMMENTS
 
Back
Top Bottom