Kama unapenda kudumu katika ndoa yako fanya mambo haya

Bernard bakari

JF-Expert Member
Mar 30, 2016
407
781
Ndoa ni Tamu sana tena Tamu kuliko kitu chochote ndani ya hii Dunia. Utamu wa ndoa utaushuhudia na kuuona pale tu ambapo wana ndoa watakuwa wamoja, wenye furaha na Amani. Kuwepo kwa migogoro kwa wana ndoa huweza kufanya ndoa kuwa chungu zaidi ya pilipili.

Katika vitu vinavyofanya ndoa iwe chungu, iwe na migogoro ya mara kwa mara ni USALITI. Usaliti ukianza kwa mmoja wa wanandoa kunafanya ndoa iwe chungu sana iwe mwenza kagundua au hajagundua kama anasalitiwa Na mpenzi wake.

Ukisaliti ndoa huko unakoenda unaweza pata vitu 2 kwanza unaweza kutana na mambo matamu kuliko ya mwenza wako au ukakutana na mambo mabaya yasikufurahishe kabisa. Ukikutana na mambo mabaya ndo pona yako lakini ukikutana na mambo mazuri na matamu utamsahau mwenza wako na kumwona si kitu, hana chochote, Anakera , Anaboa, Hukuchagua chaguo sahihi na mambo mengine kibao.

Mapenzi ni sanaa, kila mtu anastyle yake, ufundi wake na ujuzi wake wa kuishi na mpenzi wake. Hivyo mmoja wenu akijiingiza kwenye usaliti basi ombea akutane na mambo mabaya akikutana na tamtam ndoa itayumba kila siku.

Ili ndo iwe ya Aman, Upendo na Furaha jambo kumwa la kufanya ni kuepuka kujihusiaha na michepuko, hiyo ndiyo nguzo kubwa na silaha kubwa kwa wanandoa mtakuta ndoa yenu kila siku ina furaha na Amani. Jitahidini kumfanya mwenzako asiwe na wazo la kusaliti ndoa kwa kumwonesha mapenzi ya kweli na kumfanya mda wote afurahie penzi lako. NDOA BILA MICHEPUKO INAWEZEKANA.
 
Mme au Mke kushindwa kumjali mwenzake kuna chochea au kunapelekea usaliti kwa wana ndoa
 
Usaliti ni maamuzi ya mtu... Siyo lazima kila atakayekuchekea mpaka uumlee... Usaliti ni tamaa... Usaliti na akili ndogo... Usaliti ni tabia ambayo ni mbaya...



Cc: mahondaw
 
Mtoa mada umeongelea tabia ambazo kimsingi ni matokeo. Kuchepuka au usaliti ni matokeo. Ulitakiwa upanue wigo wa kujifunza zaidi. Mfano ungeongelea kukosa maarifa kama moja ya sababu yenye kuua ndoa. Leo watu wanaingia kwenye ndoa hawana maarifa yyt kuhusu ndoa mahusiano and all about sexuality. ndo maana ukichunguza utaona vinavyoua ndoa ni vitu vdg vdg ambavyo hata wazee wetu walikumbana navyo ila walihimili bse jando na unyago viliwapa maarifa ya kutosha. Leo hii hizo mila zimekufa zilizojitahidi kubaki ni ngoma tu zisizo na lolote. Vijana wenyewe leo hatuna bidii kujifunza kusoma vitabu kutafuta maarifa. Matokeo ndo ndoa kufa. Usaliti sio tatizo kama watu wanavyodhani bali ni MATOKEO ya kukosa maarifa.
 
Kwa uzoefu wangu matatizo katika ndoa huanza mara baada ya kuzaliwa mtoto wa kwanza.
 
Hongera kwa kufagilia ndoa katika kipindi ambacho ndoa zinapitia changamoto nyingi ikiwemo baadhi kuziogopa, kutodumu kama za miaka iliyopita, michepuko na usiri mkubwa wa baadhi kufanya mambo wakiwa ndani ya ndoa bila kuwataarifu wenzao kwa mfano kuwa na kiwanja au kujenga kwa siri.

Ndoa ni Tamu sana tena Tamu kuliko kitu chochote ndani ya hii Dunia. Utamu wa ndoa utaushuhudia na kuuona pale tu ambapo wana ndoa watakuwa wamoja, wenye furaha na Amani. Kuwepo kwa migogoro kwa wana ndoa huweza kufanya ndoa kuwa chungu zaidi ya pilipili.

Katika vitu vinavyofanya ndoa iwe chungu, iwe na migogoro ya mara kwa mara ni USALITI. Usaliti ukianza kwa mmoja wa wanandoa kunafanya ndoa iwe chungu sana iwe mwenza kagundua au hajagundua kama anasalitiwa Na mpenzi wake.

Ukisaliti ndoa huko unakoenda unaweza pata vitu 2 kwanza unaweza kutana na mambo matamu kuliko ya mwenza wako au ukakutana na mambo mabaya yasikufurahishe kabisa. Ukikutana na mambo mabaya ndo pona yako lakini ukikutana na mambo mazuri na matamu utamsahau mwenza wako na kumwona si kitu, hana chochote, Anakera , Anaboa, Hukuchagua chaguo sahihi na mambo mengine kibao.

Mapenzi ni sanaa, kila mtu anastyle yake, ufundi wake na ujuzi wake wa kuishi na mpenzi wake. Hivyo mmoja wenu akijiingiza kwenye usaliti basi ombea akutane na mambo mabaya akikutana na tamtam ndoa itayumba kila siku.

Ili ndo iwe ya Aman, Upendo na Furaha jambo kumwa la kufanya ni kuepuka kujihusiaha na michepuko, hiyo ndiyo nguzo kubwa na silaha kubwa kwa wanandoa mtakuta ndoa yenu kila siku ina furaha na Amani. Jitahidini kumfanya mwenzako asiwe na wazo la kusaliti ndoa kwa kumwonesha mapenzi ya kweli na kumfanya mda wote afurahie penzi lako. NDOA BILA MICHEPUKO INAWEZEKANA.
 
Kwa uzoefu wangu matatizo katika ndoa huanza mara baada ya kuzaliwa mtoto wa kwanza.
Ngoja niongezee apo apo, Wapenzi wanapopata mtoto mapenzi yanaamishiwa kwa mtoto na kufanya migogoro ya apa na pale
Mama anapeleka mapenzi kwa mtoto, na baba nae anaona kama anasalitiwa anaamishia mapenzi kwa vimada,
Matokeo yake ni ugomvi mkubwa katika family
 
  • Thanks
Reactions: mij
Hilo jambo siyo jipya, watu wamesalitiwa na kusaliti kabla Hata ya mitume na manabii kuja. JIPANGE TU KIJANA
 
Matazamio unayojenga kwenye mahusiano kutoka kwa mtu ulio nae ndio chanzo cha kuchepuka . Kwani ubongo ukishatimiziwa basi unatafuta kingine kikubwa zaidi. Inaendelea kuwa mzunguko usiokwisha, hata siku moja hautakuwa na furaha kwani vitu vinavyokupa furaha ni vya muda tu ambavyo vinaondoka na kukuacha mwenye huzuni kwenye mahusiano. Sura nzuri kama kivutio inabadilika na kuzeeka, stamina ya kufanya mapenzi inapungua na hata inaweza kupotea kabisa . Pesa inaweza kupotea kama ambavyo ilikuja mwanzoni au ikazoeleka kama kitu tu cha kawaida tu .
Kumwambia kuwa mwaminifu kwenye ndoa wakati haujui chanzo nini ni kama kusafisha maji ya mto kwa bidii wakati chanzo cha maji ndio kichafu.
 
Back
Top Bottom