MTAZAMO
JF-Expert Member
- Feb 8, 2011
- 19,643
- 33,439
Hapana Jeshi la Polisi na familia ya dogo wafatilie kuna jambo halipo sawa. Tunao makachero wabobezi ambao watafungua hilo box la siri. Ule ujumbe hau make sense kufanya mtu ajiue! Impossible ...
Hizi stori za mtu kumpenda mke wa mtu mpaka kuamua kujiua kwaajili yake sioni zikiniingia akilini.
Kama ni kweli hili jambo limetokea, ni muhimu jeshi la Polisi likafanya uchunguzi wa kina.
Pengine hili sokomoko la sms za mke wa mtu limetumika kuficha kitu.
Binafsi sijawahi kusikia mtu akimpenda mke wa mtu hadi kujitoa uhai kwasababu yake huku akijua kabisa ni kosa la kimaadili, tena mke wa mchungaji na yeye alikuwa akitumika kwa kazi ya Mungu.
Kama ingelikuwa amejiua kisa mchungaji kutembea na mke wake hapo ningeweza kuelewa japo kidogo kwamba amejiua kukimbia aibu.
Hizo sms ukizisoma wala hazionyeshi kama kuna uzito wa kupelekea yeye kujiua, wala hazioneshi labda Mwenye mke wake amejua kwamba anatembea na mkewe.
Au niambieni nyie ndugu zangu kama hii inawaingia akilini.