Kama wewe sio mwigulu basi utakua mke wake au mpenzi wake au king'asti wake
Hapana mi sipo katika hao unaowataja na wala sio fans wake pia,ila ni bora kuwekana sawa kuna faida gani kukurupuka na kuanzisha uzi kwa yale unayoyawaza tu ambayo hujafanya uchunguzi wowote wa kina hii tabia tukiiendekeza haitaijenga JF.
Kumbuka uwepo wa JF ni mwiba kwa watendaji wengi ambao hawapo sawa katika mambo yao au nyadhifa zao.Hatuna haja ya kuiweka rehani na kuwapa sababu ya kuiondoa au kuanzishwa kwa sheria ngumu zitakazotufanya tushindwe kuwa na uhuru tulionao sasa.
Tusiwe kama madereva wa Tanzania ambao wameshindwa kusoma alama za mwendo kasi mpaka wawekewe matuta ili kupunguza spidi, ustaarabu ni kitu pekee kinachotutofautisha na wanyama.Mwenzio akikosea muelekeze usimpe kichwa kwakuwa athari yake haitaishia kwake tu yaweza kuja hata kwako.