MKEHA
JF-Expert Member
- Jan 26, 2013
- 716
- 1,144
Nikiwa shabiki mkubwa na mnazi wa Arsenal nilikua nikiumia sana kipindi Drogba akiwa kwenye form kwani kila Arsenal ilipokutana na Chelsea tulichezea kichapo na hapo goli la Drogba halikukosa kabisa.
Nakumbuka katika mechi 12 alizocheza against na Arsenal alitufunga magoli 11 toka mguuni mwake.
Nilitokea kumchukia sana lakini baadae nikaujua ukweli kwamba najiumiza bure kwani uwezo wa Drogba ulikua mkubwa sana hivyo sikua na haja ya kuendeleza chuki yangu kwake na baadae nikaanza kumpenda bila kutaka.
Tulianza kuwafunga Chelsea baada ya Morinho na Drogba kuondoka pale daraajani. Nimetoa kisa hiki kujenga hoja juu ya uwezo wa Lowassa na Pinda. Lowassa alilazimika kujiudhuru uwaziri mkuu kwa shindikizo la bunge baada ya kuonekana kwamba mawaziri waliokua chini yake hawakuwajibika kisawa sawa mpaka kupelekea taifa kupata hasara.
Japo ripoti ile ya Mwakiembe haikumutia hatiani moja kwa moja Lowasa kama mhusika mkuu lakini walimpa option ya kupima mwenyewe kama anafaa kuendelea kuwa kwenye ofisi ile na mwisho wake kweli aka step down.
Naendelea kumshangaa Pinda kana kwamba haoni mood ya Watanzania anaendelea kung'ang'ania ofisi kana kwamba hakuna lililotokea kabisa.
Hili linachangiwa zaidi na watu wanao muunga mkono Pinda kwenye mbio zao za urais wakisema kwamba kuna mkono wa Lowassa kwenye ripoti ya ESCROW ili Pinda aadabishwe na Lowassa apite kiulaini.
Huku ni kutokujua na kujifanya hawajui ukweli wa mambo jisi yanavyoenda hapa nchini. Lowassa jamani ana nguvu za ajabu kama kimbunga hata utafiti wa TWAWEZA umebainisha hilo.
Kuna watu wanaweza wakawa hawampendi Lowassa kwa sababu tu anawakosesha raha kwenye timu zao za urais kama ambavyo Drogba alivyonifanya kipindi kile lakini kutompenda kwangu hakukuisaidia Arsenal kuishinda Chelsea kwa roho mbaya yangu kwake mwishoni ilibidi nianze kumpenda kwa kujilazimisha kwa sababu ya uwezo wake.
Hivyo hivyo kwa wasiompenda Lowassa waanze kumpenda kwa kujilazimisha maana aweza kuwa rais wetu ajaye hata kama hatutaki.
Ni mtazamo wangu tu jamani nikiwa huku kijijini kwetu Muyama Buhigwe
Nakumbuka katika mechi 12 alizocheza against na Arsenal alitufunga magoli 11 toka mguuni mwake.
Nilitokea kumchukia sana lakini baadae nikaujua ukweli kwamba najiumiza bure kwani uwezo wa Drogba ulikua mkubwa sana hivyo sikua na haja ya kuendeleza chuki yangu kwake na baadae nikaanza kumpenda bila kutaka.
Tulianza kuwafunga Chelsea baada ya Morinho na Drogba kuondoka pale daraajani. Nimetoa kisa hiki kujenga hoja juu ya uwezo wa Lowassa na Pinda. Lowassa alilazimika kujiudhuru uwaziri mkuu kwa shindikizo la bunge baada ya kuonekana kwamba mawaziri waliokua chini yake hawakuwajibika kisawa sawa mpaka kupelekea taifa kupata hasara.
Japo ripoti ile ya Mwakiembe haikumutia hatiani moja kwa moja Lowasa kama mhusika mkuu lakini walimpa option ya kupima mwenyewe kama anafaa kuendelea kuwa kwenye ofisi ile na mwisho wake kweli aka step down.
Naendelea kumshangaa Pinda kana kwamba haoni mood ya Watanzania anaendelea kung'ang'ania ofisi kana kwamba hakuna lililotokea kabisa.
Hili linachangiwa zaidi na watu wanao muunga mkono Pinda kwenye mbio zao za urais wakisema kwamba kuna mkono wa Lowassa kwenye ripoti ya ESCROW ili Pinda aadabishwe na Lowassa apite kiulaini.
Huku ni kutokujua na kujifanya hawajui ukweli wa mambo jisi yanavyoenda hapa nchini. Lowassa jamani ana nguvu za ajabu kama kimbunga hata utafiti wa TWAWEZA umebainisha hilo.
Kuna watu wanaweza wakawa hawampendi Lowassa kwa sababu tu anawakosesha raha kwenye timu zao za urais kama ambavyo Drogba alivyonifanya kipindi kile lakini kutompenda kwangu hakukuisaidia Arsenal kuishinda Chelsea kwa roho mbaya yangu kwake mwishoni ilibidi nianze kumpenda kwa kujilazimisha kwa sababu ya uwezo wake.
Hivyo hivyo kwa wasiompenda Lowassa waanze kumpenda kwa kujilazimisha maana aweza kuwa rais wetu ajaye hata kama hatutaki.
Ni mtazamo wangu tu jamani nikiwa huku kijijini kwetu Muyama Buhigwe