Bado Kidogo 2015
JF-Expert Member
- May 24, 2012
- 207
- 78
Wanabodi,
Katika mkutano ulimalizika majuzi hapa mjini Dodoma - Kizota serikali ya CCM imewataka wanaCCM kutembea kifua mbele na kuepuka tambo za wapinzani kuwa hawajafanya kitu!!!!! Kauli hiyo na nyingine nyingi za matambo zilizotoka zilikuwa na lengo la kuwaaonyesha wananchi na wanaCCM kwa ujumla kuwa chama chao kimefanya na kinafanya kazi kubwa mpaka hapo kilipofikia!!!!!
Ok, tukiachana na hilo ipi ni hali halisi??? Kiukweli namkubuka babu yangu aliyesema "ukiona mtu anajitamba sana jua hana kitu" Nami kauli hiyo naona ina ukweli kwa 75%.
1. Huwezi ukawa unashindwa kutekeleza majukumu yako ya ndani kisha ukajisifu kwa kujenga nyumba. Nyumbani watoto wanalala na njaa lakini wewe nje unasema nina nyumba nne. Kitendo cha serikali ya CCM kushindwa hata kutekeleza mahitaji ya serikali yake yenyewe ni hatari sana. Mpaka sasa karibu nusu ya mwaka wa fedha unataka kukatika lakini serikali imeshindwa kuleta hata nusu ya bajeti ya kila wizara iliyopitishwa na bunge ni aibu kubwa. Kama kuna mtu anabisha achukue bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012 alinganishe na 2012/2013 kwa mtiririko wa mafungu au utekelezaji.
Wizara nyingi za serikali zinalia njaa, wanashindwa kutengeneza magari, mafuta hawana, vitendea kazi ofisini hakuna, na mbaya zaidi saizi kumezuka mtindo wa kuchelewesha hata haki zao yaani mishahara!!! Ni mjinga gani atayefurahia kutengenezwa kwa barabara huku akijua fedha nyingi ya mabarabara hayo ni mikopo???
2. Nikiachana na watumishi wa serikali wao wanajuana na mwajiri wao, vipi hali halisi ilivyo mtaani. Karibu watu wengi saa hizi wanalia hali kuwa ngumu kuliko ilivyokuwa miaka ya nyuma. Kwa kuwa wananchi wengi wa Tanzania hatuhoji hali hii imekuaje??? Ukweli ni kwamba SERIKALI IMEPUNGUZA MATUMIZI YAKE na kusababisha mzunguko wa fedha kuwa mdogo.
Wapo wanaweza kubisha, lakini wafanya biashara wengi wanaofanya biashaara na serikali wapo njiani kugoma kutokana na kutolipwa. Hali hii ingekuwa ina uafadhali kama basi serikali ingejitahiti hata kukidhi mahitaji ya kiuendeshaji ya serikali yenyewe!!!!
Kwa mantiki hiyo basi, kama mkulima analia, mfanyakazi analia na hata hao wafanyabiashara wengi wanakiri hali ya kipato chao siyo nzuri kutokana na wengi kutokuwa na fedha LIPI WANALOJIVUNIA SERIKALI YA CCM mapaka kuwafanya watembee kifua mbele????
Naamini chama chochote kama kingekuwa madarakani kisingeshindwa kufanya haya wanayofanya wanaCCM na kujitamba. Kama vyanzo ni kwenda kukopa hata ukiniweka mimi nitashindwa kukopa nije niwafanyie haya wanayofanya serikali ya CCM????
Kiukweli kama serikali ya CCM inataka wanachama na serikali yake ifanye zaidi ya haya inayoyasema ili tuone tofauti badala ya kujisifia kwa kitu ambacho kila mtu anaweza kukifanya as long as yupo madarakani!
Kwa kuhitimisha, serikali ya sasa iache matambo badala ya kufanya kazi. Hali ni mbaya sana mtaani, wakulima wanalia, wafanyakazi wanalia, ni wafanyabiashara tu angalau kidogo vinginevyo serikali nayo inalia lakini inataka kuwaaminisha wananchi inacheka!!!!
Huo ni kwa kadri ya uelewa wangu wa form 4 ya kata niliyomaliza majuzijuzi. Kama ningefika hata form six, I could dig more for the benefit of others.
Copy, Mzee Mwanakijiji, Mchambuzi PakaJimmy Mungi, Crashwise Ritz zomba Rejao @Naape Jr Preta BADILI TABIA, Mwana Mtoka Pabaya mikaeli p aweda, Tumaini Makene, Money stunna, Bujibuji, maggid; Molemo,
Ruttashobolwa Yericko Nyerere, na wengineo wengi ambao sijwataja.
MoDs naomba usiunganishe na nyuzi ngingine.
Nawasilisha.
Katika mkutano ulimalizika majuzi hapa mjini Dodoma - Kizota serikali ya CCM imewataka wanaCCM kutembea kifua mbele na kuepuka tambo za wapinzani kuwa hawajafanya kitu!!!!! Kauli hiyo na nyingine nyingi za matambo zilizotoka zilikuwa na lengo la kuwaaonyesha wananchi na wanaCCM kwa ujumla kuwa chama chao kimefanya na kinafanya kazi kubwa mpaka hapo kilipofikia!!!!!
Ok, tukiachana na hilo ipi ni hali halisi??? Kiukweli namkubuka babu yangu aliyesema "ukiona mtu anajitamba sana jua hana kitu" Nami kauli hiyo naona ina ukweli kwa 75%.
1. Huwezi ukawa unashindwa kutekeleza majukumu yako ya ndani kisha ukajisifu kwa kujenga nyumba. Nyumbani watoto wanalala na njaa lakini wewe nje unasema nina nyumba nne. Kitendo cha serikali ya CCM kushindwa hata kutekeleza mahitaji ya serikali yake yenyewe ni hatari sana. Mpaka sasa karibu nusu ya mwaka wa fedha unataka kukatika lakini serikali imeshindwa kuleta hata nusu ya bajeti ya kila wizara iliyopitishwa na bunge ni aibu kubwa. Kama kuna mtu anabisha achukue bajeti ya mwaka wa fedha 2011/2012 alinganishe na 2012/2013 kwa mtiririko wa mafungu au utekelezaji.
Wizara nyingi za serikali zinalia njaa, wanashindwa kutengeneza magari, mafuta hawana, vitendea kazi ofisini hakuna, na mbaya zaidi saizi kumezuka mtindo wa kuchelewesha hata haki zao yaani mishahara!!! Ni mjinga gani atayefurahia kutengenezwa kwa barabara huku akijua fedha nyingi ya mabarabara hayo ni mikopo???
2. Nikiachana na watumishi wa serikali wao wanajuana na mwajiri wao, vipi hali halisi ilivyo mtaani. Karibu watu wengi saa hizi wanalia hali kuwa ngumu kuliko ilivyokuwa miaka ya nyuma. Kwa kuwa wananchi wengi wa Tanzania hatuhoji hali hii imekuaje??? Ukweli ni kwamba SERIKALI IMEPUNGUZA MATUMIZI YAKE na kusababisha mzunguko wa fedha kuwa mdogo.
Wapo wanaweza kubisha, lakini wafanya biashara wengi wanaofanya biashaara na serikali wapo njiani kugoma kutokana na kutolipwa. Hali hii ingekuwa ina uafadhali kama basi serikali ingejitahiti hata kukidhi mahitaji ya kiuendeshaji ya serikali yenyewe!!!!
Kwa mantiki hiyo basi, kama mkulima analia, mfanyakazi analia na hata hao wafanyabiashara wengi wanakiri hali ya kipato chao siyo nzuri kutokana na wengi kutokuwa na fedha LIPI WANALOJIVUNIA SERIKALI YA CCM mapaka kuwafanya watembee kifua mbele????
Naamini chama chochote kama kingekuwa madarakani kisingeshindwa kufanya haya wanayofanya wanaCCM na kujitamba. Kama vyanzo ni kwenda kukopa hata ukiniweka mimi nitashindwa kukopa nije niwafanyie haya wanayofanya serikali ya CCM????
Kiukweli kama serikali ya CCM inataka wanachama na serikali yake ifanye zaidi ya haya inayoyasema ili tuone tofauti badala ya kujisifia kwa kitu ambacho kila mtu anaweza kukifanya as long as yupo madarakani!
Kwa kuhitimisha, serikali ya sasa iache matambo badala ya kufanya kazi. Hali ni mbaya sana mtaani, wakulima wanalia, wafanyakazi wanalia, ni wafanyabiashara tu angalau kidogo vinginevyo serikali nayo inalia lakini inataka kuwaaminisha wananchi inacheka!!!!
Huo ni kwa kadri ya uelewa wangu wa form 4 ya kata niliyomaliza majuzijuzi. Kama ningefika hata form six, I could dig more for the benefit of others.
Copy, Mzee Mwanakijiji, Mchambuzi PakaJimmy Mungi, Crashwise Ritz zomba Rejao @Naape Jr Preta BADILI TABIA, Mwana Mtoka Pabaya mikaeli p aweda, Tumaini Makene, Money stunna, Bujibuji, maggid; Molemo,
Ruttashobolwa Yericko Nyerere, na wengineo wengi ambao sijwataja.
MoDs naomba usiunganishe na nyuzi ngingine.
Nawasilisha.