Kama huu ni udikteta uchwara, tuendelee nao

mabuba

Senior Member
Dec 5, 2006
133
90
Kudhibiti wakwepa kodi ni lazima,

Walifanya yao nchi pasi huruma,

Walikula na kukomba kwa kukomoaa

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wafanyakazi hewa hatukuwataka,

Sasa arobaini imefika, wajifanya hasira,

Waondolewe kwa mbwembwe

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Madawati yanaundwa kwa hara,

Watoto wapate jisitiri,

Hili nalo nongwa, aibu,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wabunge wasionidhamu.

Chamoto wanakiona,

Wamefurushwa bungeni,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wengine wanadanya, kule mjengoni,

Tulia amewatuliza, wauita uchwara,

Koma yenu imefika, ukweli uwe wazi

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Miungu kwenye utumishi, zao zinahesabika,

Wabanangaji kwenye kazi, muda umetimu,

Weledi na mahiri, nyuso zenye tabasamu,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Mafisadi wanahaha, kificho kukiingia,

Wanaona kihama, chao kimefika,

Wanatumia kila mbinu, kuficha zao kucha,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Walimuona dhaifu, Jakaya Muungwana,

Sasa kaja wakuwasimamia, waanza lalama,

Aliwaacha wajifunze, matusi yawatoka,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.
 
MTOA THREAD NIMEKUSHITUKIA UNATAKA TUTOE MAONI ILI TUFIKISHWE KULEEEEEEEE KWA PILATO
 
Kudhibiti wakwepa kodi ni lazima,

Walifanya yao nchi pasi huruma,

Walikula na kukomba kwa kukomoaa

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wafanyakazi hewa hatukuwataka,

Sasa arobaini imefika, wajifanya hasira,

Waondolewe kwa mbwembwe

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Madawati yanaundwa kwa hara,

Watoto wapate jisitiri,

Hili nalo nongwa, aibu,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wabunge wasionidhamu.

Chamoto wanakiona,

Wamefurushwa bungeni,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Wengine wanadanya, kule mjengoni,

Tulia amewatuliza, wauita uchwara,

Koma yenu imefika, ukweli uwe wazi

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Miungu kwenye utumishi, zao zinahesabika,

Wabanangaji kwenye kazi, muda umetimu,

Weledi na mahiri, nyuso zenye tabasamu,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Mafisadi wanahaha, kificho kukiingia,

Wanaona kihama, chao kimefika,

Wanatumia kila mbinu, kuficha zao kucha,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.



Walimuona dhaifu, Jakaya Muungwana,

Sasa kaja wakuwasimamia, waanza lalama,

Aliwaacha wajifunze, matusi yawatoka,

Ni udikteta uchwara, basi mimi nautaka.


Mdau nakuelewa, hayo unayotamka,

Maadili zingatia, katufikisha hakika,

Na kama ndo maana, wengi tumefarijika,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Sisi waakina mama, k’jifungua sakafuni,

Ndani miezi miwili, twajimwaga vitandani,

Kama hi si miujiza, sikubali abadani,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Miongo imeyoyoma, wanafunzi mavumbini,

Mwaka bado hujatima, sasa wa madawatini,

Tunajidai lawama, kuvaa mbao miwani,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Ofisini Mungu watu, Njoo kesho Njoo kesho,

Hili analidhibiti, nidhamu inarejea,

Ufanisi kujongea, nani hajalitambua?

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Kodi anazidhibiti, Nuer haoni ndani,

Viwanda viko mbioni, wasubiri wananchi,

Kudumisha hapa kazi, Maisha kuyaborehsa,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Ufisadi kwake mwiko, mahakama i mbioni,

Katu mali kwa mkato, Bali mali ni kwa jasho,

Na tumuunge mkono, Rais wetu makini.

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’



Mengi nengeyaeleza, Lakini hapa ni Kazi tu,

Nahudumia wateja, Risiti nawapatia,

Bado ninasisitiza, endapo ndiyo maana,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’
 
Asante sana Mdau
Mdau nakuelewa, hayo unayotamka,

Maadili zingatia, katufikisha hakika,

Na kama ndo maana, wengi tumefarijika,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Sisi waakina mama, k’jifungua sakafuni,

Ndani miezi miwili, twajimwaga vitandani,

Kama hi si miujiza, sikubali abadani,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Miongo imeyoyoma, wanafunzi mavumbini,

Mwaka bado hujatima, sasa wa madawatini,

Tunajidai lawama, kuvaa mbao miwani,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Ofisini Mungu watu, Njoo kesho Njoo kesho,

Hili analidhibiti, nidhamu inarejea,

Ufanisi kujongea, nani hajalitambua?

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Kodi anazidhibiti, Nuer haoni ndani,

Viwanda viko mbioni, wasubiri wananchi,

Kudumisha hapa kazi, Maisha kuyaborehsa,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’


Ufisadi kwake mwiko, mahakama i mbioni,

Katu mali kwa mkato, Bali mali ni kwa jasho,

Na tumuunge mkono, Rais wetu makini.

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’



Mengi nengeyaeleza, Lakini hapa ni Kazi tu,

Nahudumia wateja, Risiti nawapatia,

Bado ninasisitiza, endapo ndiyo maana,

Nami pia nautaka, ‘udikteta Uchwara’
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom