Kama bajeti mpaka sasa haijatumika (hazina haijatoa) imeenda wapi au nani anaitumia

dosama

JF-Expert Member
Dec 25, 2010
912
957
Wakati bunge limehairishwa Juzi J3 hoja nyingi za wabunge zilionyesha kuwa wizara nyingi hazikapewa fedha kulingana na bajeti ya serikali ya 2011/2012 ya sh. Tril 12.

Kwa mfano wizara ya ujenzi ilipangiwa tril 1.2 na ilikuwa inadaiwa sh Bil 400 na ushehe lakini mpaka mwezi February hazina ilikwisha toa sh bil 300 inamaana zaidi ya bil 900 haIjatoka na tunaelekea bajeti nyingine mwezi wa sita.

Napenda kujua ile ilikuwa bajeti hewa?
Fedha zilikuwepo na zimefanya nn?
Je wizara zote ndo hivi?

Kumbuka uchumi unakuwa kwa 7%

Na TRA imevuka malengo ya ukusanyaji wa kodi
 
Kitu ambacho watz wengi wa kawaida hawajui ni kuwa kinachoitwa bajeti ya serikali huwa ni usanii tu. Bajeti inayopitishwa na bunge huwa ni hewa. Kinachofanyika ni kwamba serikali hupeleka bungeni vyanzo vya mapato na jumla ya mapato inayotegemea kukusanya. Then inasema itagawanya vipi hayo mapato. Fedha halisi zinakua hazipo. Kinachokuja kutokea kama sasa serikali imeshimdwa kukusanya kiasi kile ilichokua inatarajia. Hivyo imegawia mawizara kile kilichopatikana. Fedha nyingine hazijapatikana hivyo hazipo.

Hata wakati wabunge wanapinga kupitisha bajeti ya miundombinu ili iongezwe ilikua usanii tu. Maana hata ile ya awali tu isingepatikana. Wanachofanya ni ku inflate budget na mwisho wa siku hakuna physical output.
 
Hauchi hauchi mwisho wake unakucha...tutafika tu tunapokwenda. Leo si wameshavunja matanga huko msibani? Labda watu watakuwa serious na kazi zao,lol!
 
Wakati bunge limehairishwa Juzi J3 hoja nyingi za wabunge zilionyesha kuwa wizara nyingi hazikapewa fedha kulingana na bajeti ya serikali ya 2011/2012 ya sh. Tril 12.

Kwa mfano wizara ya ujenzi ilipangiwa tril 1.2 na ilikuwa inadaiwa sh Bil 400 na ushehe lakini mpaka mwezi February hazina ilikwisha toa sh bil 300 inamaana zaidi ya bil 900 haIjatoka na tunaelekea bajeti nyingine mwezi wa sita.

Napenda kujua ile ilikuwa bajeti hewa?
Fedha zilikuwepo na zimefanya nn?
Je wizara zote ndo hivi?

Kumbuka uchumi unakuwa kwa 7%

Na TRA imevuka malengo ya ukusanyaji wa kodi

Mkuu,

Mimi nilishaacha kuangalia bunge la bajeti zamani sana. Upuuzi huu wa kupigania kisichokuwapo niliona sio sawa. Angalau katika kila bunge la bajeti kungekuwa na kuwakilisha "yatokanayo" na bajeti ya mwaka uliopita ingekuwa tofauti. Walio serikalini wanasema pesa wanayopata kwa mwaka ni takriban 40% (ukibahatika) ya ile waliyopangiwa kwenye bajeti. Ukiuliza unaambiwa hatukufikia lengo la ukusanyaji! Lakini kila siku tunaelezwa TRA wamevuka lengo na kujipa bonus kubwa kubwa tu.

Sasa kwa nini Waziri wa fedha asichukuliwe hatua kwa kilidanganya taifa mwaka nenda, mwaka rudi?? Siri ya mtungi aijuaye ni kata!
 
Bajeti ni mpango unaoelezea matumizi katika miradi na shughuli zilizoainishwa...pia huelezea matarajio na vyanzo vya fedha ili kutekeleza mpango mzima.
Serikali hupanga bajeti huku ikitegemea karibu asilimia 40 kutoka kwa wahisani,na yenyewe ikitegemea makusanyo makubwa huku inaruhusu tax exemption na tax holidays kwa wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji....hivyo inashindwa kupata fungu kulingana na bajeti ilivyoainisha.
Bajeti haimaanishi uwepo wa fedha tayari...its just a quantified statement of plan.
 
Mkuu,

Mimi nilishaacha kuangalia bunge la bajeti zamani sana. Upuuzi huu wa kupigania kisichokuwapo niliona sio sawa. Angalau katika kila bunge la bajeti kungekuwa na kuwakilisha "yatokanayo" na bajeti ya mwaka uliopita ingekuwa tofauti. Walio serikalini wanasema pesa wanayopata kwa mwaka ni takriban 40% (ukibahatika) ya ile waliyopangiwa kwenye bajeti. Ukiuliza unaambiwa hatukufikia lengo la ukusanyaji! Lakini kila siku tunaelezwa TRA wamevuka lengo na kujipa bonus kubwa kubwa tu.

Sasa kwa nini Waziri wa fedha asichukuliwe hatua kwa kilidanganya taifa mwaka nenda, mwaka rudi?? Siri ya mtungi aijuaye ni kata!

Ni kweli implimetation ya ya budget yetu ni vigumu sana, kwani tunatumia what we call Cash budget, i.e what you collect is what you are going to spend, sasa assume umekusanya 10bln nmwezi huu wa April, katika mwezi may ndiyo pesa ya kutumia katika wizara zote.
Lakini pia na TRA hawsemi ukweli wanaiba kutumia budget yaani tunaita budget slack, you budget less while you know you are going to collect more. Kwa mfano wakati wanafanya ile estimate exchange rate ilikuwa 1$= 1,200TZS sasa 1$= 1,600 TZS wanapata hapa kwenye exchange rate, while purchasing power pia inakuwa inapungua sana.
"NCHI INATISHA WAZEE" noamba kutoa hoja.
 
Mkuu,

Mimi nilishaacha kuangalia bunge la bajeti zamani sana. Upuuzi huu wa kupigania kisichokuwapo niliona sio sawa. Angalau katika kila bunge la bajeti kungekuwa na kuwakilisha "yatokanayo" na bajeti ya mwaka uliopita ingekuwa tofauti. Walio serikalini wanasema pesa wanayopata kwa mwaka ni takriban 40% (ukibahatika) ya ile waliyopangiwa kwenye bajeti. Ukiuliza unaambiwa hatukufikia lengo la ukusanyaji! Lakini kila siku tunaelezwa TRA wamevuka lengo na kujipa bonus kubwa kubwa tu.

Sasa kwa nini Waziri wa fedha asichukuliwe hatua kwa kilidanganya taifa mwaka nenda, mwaka rudi?? Siri ya mtungi aijuaye ni kata!

Hapo ndipo watz tunapigwa changa la macho.
 
Back
Top Bottom