JWTZ Ikabidhiwe TPA

Jenerali Ambamba

JF-Expert Member
Joined
Sep 8, 2014
Posts
3,344
Reaction score
2,537
Naomba kumpa ushauri Rais Magufuli, kwa muda mrefu wafanyakazi wa Bandari wametuzingua sana, sasa ikibidi kabidhi Bandari kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania angalau kwa miaka 2-3 walete ufanisi na kukusanya kodi na ushuru inavyostahili.
 
Sasa hapo shida ni TPA au TRA. mchawi wa maendeleo ya hii nchi ni TRA.
 
Kama nikibahatika kuonana na rais ushauri wangu wa kwanza kwake JWTZ alitumie katika kila nyanja kama ni Muhimbili basi uongozi utoke JWTZ kadhalika kwa TPA,TRA,CCPB,MASHIRIKA YA UMMA,BOT,TCRA,TANROAD, NK. Yaani hapo kuna faida kubwa sana kuliko kuendelea kuwatumia raia.
 
Dhana kwamba JWTZ wanafanya kazi kwa weledi haina msingi. Hukupita JKT? Huoni jeshi lilivyokosa nidhamu kiasi cha kuthubutu kupiga raia mara kwa mara?

Nani kakwambia jeshi wanajua namna ya kuongoza kazi za bandari? They don't have the managerial competence needed to run a port.

Kuna mpangilio jeshini, lakini sio nidhamu. Mpangilio wenyewe uliopo jeshini unaletwa na woga na wala sio nidhamu.
 
Jeshini hakunaga ufisadi, hawanaga siasa ooh! Sijui nini mara ivi mara iv wao ni Offensive kwa kwenda mbele. Safi sana kama ingepewa JWTZ.
 
Kulihusisha jeshi katika mambo ya kiutawala moja kwa moja ni kujiandalia mazingira ya mapinsuzi ya kijeshi ktk nchi. Raisi aweke tu utawala bora ktk haya mashirika sio kuruhusu jesho loshike hatam
 
Naomba kumpa ushauri Rais Magufuli, kwa muda mrefu wafanyakazi wa Bandari wametuzingua sana, sasa ikibidi kabidhi Bandari kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania angalau kwa miaka 2-3 walete ufanisi na kukusanya kodi na ushuru inavyostahili.
Sikubaliani na wewe hata kidogo,watu waliosomea fani zao wanaweza kufanya vizuri chini ya usimamizi wa JPM na PM
 


Hata maeneo yote yenye utata wa migogoro isiyokwisha kama vile mabonde yaliyotengwa kwa shughuli maalumu kama Ihefu, maeneo hatarishi nyakati za mafuriko kama bonde la Msimbazi lote, ile milima inayochomwa moto kila kukicha bila kujali kuwa ni chanzo cha maji ya mto Ruvu unaonywesha Dar na Pwani pale Morogoro, mapori yote ya hifadhi ambako miti inakatwa kwa kasi kubwa kwa ajili ya kuchoma mkaa na kuwaneemesha maafisa mali asili etc,
 


jeshi ni serikali kamili.wana kila kitengo unachokiona serikalini.hata ukienda embassy utakuta kuna mwambata,wana timu za michezo,walimu,madokta,managers,accountants,n.k lipo pale tayari kwa lolote.

kuhusu weledi sijui,ila hamna sehemu huwezi litumia jeshi.
 
Wakifanya ufisadi nani atawahoji ? Wakipewa hiyo kazi nani atalinda nchi ? Waendelee na kazi yao ya "KULINDA NCHI" basi. Pendekezo lako nilakijinga.
 
Naunga mkono hoja.

Wapewe kazi hii kwa miaka miwili TUUU. Aidha system ya TPA iunganishwe na TRA na Rais ateue watendaji watano wa TISS wawe na access ktk kufatilia nini kimeingia, kimetoka na kulipiwa nini. System iwe na uwezo wa ku attach picha hata Kama ni kidogo ya KILICHOMO ndani ya container siku ya kuingia, kikioana na doc na kile kitakachokuwemo siku ya kutoka kikioana na doc. Sio tu kuzuia wizi Hii pia itaonesha ufanisi wa utendaji kazi TPA na huko TRA.

Mhe. Rais na Wairi Mkuu pia wawe na access na hiyo system hata Kama wataingia humo kusoma tu mara moja kwa mwaka.

Queen Esther

katika taasisi zenye nidhamu na maadili JWTZ wanaongoza katika nchi hii
 
Naomba kumpa ushauri Rais Magufuli, kwa muda mrefu wafanyakazi wa Bandari wametuzingua sana, sasa ikibidi kabidhi Bandari kwa Jeshi la Wananchi wa Tanzania angalau kwa miaka 2-3 walete ufanisi na kukusanya kodi na ushuru inavyostahili.
Kabla ya hapo tujikumbushe ufisadi wa meremeta kule kwa wanajeshi.
 
Jmani ndiyo taaluma yao hiyo? Mbona tunakurupuka tu.Kwa hiyo jeshi wakikabidhiwa TPA au TRA umeambiwa huko kuna Rigwaride na kupiga mizinga.Tutoe mawazo yenye akili kdg siyo pumba
 

Uko vzr
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…