Leo nimeabudu katika kanisa la winners chaplel lililoko Ukonga Banana DSM.... tumefundishwa jinsi ya kuzikataa laana za ukooo .... kumbe laana ziko katika njia mbali mbali... yule mchungaji amefundisha kwamba laana inatembea vizazi hadi vizazi kumbe kuna laana katika familia mbali mbali kwa mfano
- Kuna familia ambayo huwa hawaoi/hawaolewi na wakiolewa/wakioa ndoa kuvunjika ni kitu cha kawaida ni laana
- Kuna familia ambayo ndoa ni matatizo yaani ndoa hazina amani ni magomvi kila kukicha nayo ni laana
- Kuna familia ambayo ukoo mzima hakuna msomi hata mmoja aliyefika hata chuo kikuu nayo ni laana
- Kuna familia ambayo watu haafikishi miaka zaidi ya 45 wanakufa nayo ni laana
- Kuna familia ambayo mtu akitoka kwao harudi anaishia huko huko nayo ni laana
- Kuna familia ambayo ukoo mzima hakuna mwenye uwezo japo kidogo la sivyo mmoja akiwepo mkoo mzima unamwangalia yeye nayo ni laana.
- Kuna familia ambayo watu wanakufa kwa aina moja vifo nayo ni laana .....
- Kuna familia ambayo ukoo mzima ni walevi kiasi cha kukosa mwelekeo nayo ni laana
- kuna familia mbayo inaabudu ndumba na uchawi kwao ni jadi nayo ni laana...
- orodha ni ndefu ya laana hizi na zile .... yule mchungaji ametufundisha kuzikataa na kwa kupitia neno la MUNGU na katika JINA LA YESU. ...... Nakutakia Jumapili njema