Juma Abdul aonyesha ubabe kwa Banda wa Simba

rodrick alexander

JF-Expert Member
Feb 12, 2012
15,191
20,161
Juma Abdul aonyesha umbo lake dogo halimzuii kutembeza ubabe, apambana na Banda wa Simba..

juma%2Babdul%2Bvs%2Bbanda.jpg


Beki Juma Abdul wa Yanga ndiye amekuwa gumzo zaidi mitandaoni kutokana na kuonyesha ubabe wake.

Abdul anaonekana kwenye picha akijaribu kumkaba beki wa Simba, Abdi Banda licha ya kwamba ana umbo kubwa kuliko yeye.

Beki huyo wa Yanga, alivaana na Banda wakati wa mechi hiyo ya watani hatua ya nusu fainali ya Kombe la Mapinduzi kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, jana.

Vurugu lilianza baada ya Banda kumuangusha Kaseke ambaye alionekana kuumizwa kutokana na hali hiyo, Abdul akamvaa Banda na kuanza kumvinya usoni.

Hata hivyo, baadaye mwamuzi wa mchezo huo aliwaramba kadi za njano wote wawili kwa hatua hiyo.

Ukiangalia inaonekana Abdul ana umbo sana ukimlinganisha na Banda. Lakini inaonekana hakujali na alitaka kuonyesha yeye ni ‘msela’ wa Tandale na hataki mchezo hata kidogo.

Mechi hiyo iliisha kwa suluhu ndani ya dakika 90. Mwisho Simba ikashinda kwa mikwaju 4-2 ya penalti na kusonga fainali.

My Take:
Ukiisoma hii habari ndio unajua upeo wa waandishi wetu ukoje. Badala ya kuonya tabia mbovu za wachezaji hapa wanamsifia Juma Abdul akisoma hii habari ataona kama kafanya kitu cha maana atarudia tena akipigwa red card ataona kaonewa wakati Abdul Banda akisoma hii habari atakuwa anapanga kulipiza kisasi.

Waandishi wetu wanapaswa kuwa makini na kile wanachoandika.
 
Unategemea nini tofauti mkuu?Wengi wao hawajaenda kwenye kozi yeyote ya journalism. Hivyo hawajui ethics zake. Wao kazi yao kutumia kalamu kuuza magazeti yao ya udaku na blogg uchwara. Unaposomea journalism kuna kozi ya law.Katika mengi unayofundishwa ni innuendo,Pia eneo lingine lenye udhaifu mkubwa ni balancing ya story.Makanjanja wetu wanamhoji mtu mmoja au upande mmoja na huo ndio unakuwa ukweli. Fanya utafiti kidogo kwa waandishi wa habari wa Kenya utaona tofauti kubwa sana. Hasa kuhusu maswali wanayouliza.
 
Na hao ndo waandishi wa mpira
uhuni kwao ndo sifa

Mechi ile angekuwa refa kutoka nje kadi nyekundu nyiingi zingetembea
 
Kuna kipindi fulani cha Tv kinazungumzia maswala ya soka. Kwenye clips za kupromote hicho kipindi, kuna clip ya wachezaji wakimpiga refa na kumkimbiza. Na maneno yanayoambatana na ile clip yanaashiria ni jambo fulani la kusifiwa. Yaani ni aibu, na mamlaka za michezo zipo na hivyo vitu vinafanyika. Sijui kama kile kipindi kinaendelea na hiyo jingle yao isiyo ya kiungwana. Wenzetu upuuzi kama huo hata ku-replay kwenye live match ni ukakasi. Watanzania tuna safari ndefu halafu bado hatujaianza.
 
Bongo mambo ya kipuuzii puuzii ndo yanasifiwa sanaa..alafu kesho mnataka akacheze EPL akamkabe wenger au????
 
Kwani boti mmeshapanda kurudi dar? Sisi bado tunakula bata zenj tukisubiri tunywe juice za mango tusepe tutawakuta.
 
Back
Top Bottom