PreGE2025 Julius Mwita: Chama hakijatujibu waraka wetu, wapambe wanatuita waasi

PreGE2025 Julius Mwita: Chama hakijatujibu waraka wetu, wapambe wanatuita waasi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
2,786
Reaction score
7,567
Wakuu,

"Serikali na Bunge wamepaka rangi sheria ya uchaguzi kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa tume huru ya Taifa ya uchaguzi na ndio maana sisi tunaunga mkono No reforms ili kuwe na chaguzi huru, za haki na za amani ili kila mmoja akigombea aone anaweza kushinda.

Sisi hatupingani na chama, tunakishauri chama kama wajibu wetu na ushauri una hiyari wa kupokea ama kutopokea sasa Katibu Mkuu hajatujibu kwamba kapokea, kausoma ushauri wetu na hauna mantiki ama una mantiki.

Soma Pia: CHADEMA yamng'oa Katibu wa Sekretarieti wa chama, Julius Mwita baada ya kuibuka mzozano kwenye kundi sogozi

Na sisi kwenye waraka wetu tumeandika kuwa iwapo chama hakitakubali ushauri wetu tunaendelea kuheshimu maamuzi ya Chama kwa mapenzi yetu yote.

Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025

Mpaka leo, siyo Mwenyekiti wa Chama, sio Katibu Mkuu aliyesema tumepokea na hatukubaliani na nyie fuateni msimamo wa chama na wala hajatuandikia kwasababu sisi tumemuandikia Katibu Mkuu na tukaona waraka upo mtandaoni ukipotoshwa na wapambe na hata Press yetu ya juzi imebidi tuzungumze ili watu waelewe kwamba sisi tunakishauri chama na ningetegemea Mwenyekiti angesema tumepokea ushauri wa G55 na ninawaagiza warudi tukajenge chama kwani msimamo wa Chama ni hivi na hivi lakini wapambe huko nje ndiyo wanatuita waasi na wasaliti lakini sisi hatujapinga msimamo wa Chama." - Julius Mwita
 
Katibu Mkuu anajibuje waraka unaopingana na maamuzi halali ya vikao?

Kwamba ajipe mamlaka zaidi ya vikao vya kamati kuu, baraza kuu na mkutano Mkuu.

Kiufupi watajibiwa kwa njia waliyoupelekea. Wao kwanza wameanza na kuunda kundi ndani ya Chama na kujipa jina kabisa kinyume na Chama na Taasisi zilizo chini ya Chama mfano mabaraza ya Chama.

Sasa kwa mtindo huu kama wakijibiwa kama G55 hawaoni watafanya kila watu ndani ya Chama wakiwa na agenda yao waunde kakikundi kao?

Utajibuje kikundi ambacho hakitambuliki wala kusajiriwa hata kwenye serikali ya mtaa?

Kuwajibu ni kuhalalisha utovu wao wa nidhamu na kutambua kundi la kihuni ambalo halijulikani na mamlaka zinazohusika na vikundi.

Sasa akiwajibu address yao inapatikana wapi na ofisi zao zinapatikana wapi?
 
Back
Top Bottom